Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Katika Mji Mdogo wa Mbalizi kuna ardhi ya ukubwa wa zaidi ya ekari 5,000 iliyotengwa kwa ajili ya Tanganyika Packers ambayo haijaendelezwa kwa zaidi ya miaka 30 iliyopita. (a) Je, ni lini Serikali itawarudishia wananchi wa Mji Mdogo wa Mbalizi eneo hilo kwa lengo la kuliendeleza kwa kubadili matumizi kutokana na kukua kwa kasi kubwa kwa Mji wa Mbalizi? (b) Pamoja na kubadili matumizi ya ardhi hiyo, je, Serikali ina mpango gani kwa wananchi wanaotumia ardhi hiyo hasa ikizingatiwa kuwa wengi wao hawakupewa fidia yoyote?

Supplementary Question 1

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Naomba niishukuru Serikali kwa majibu mazuri, na ni nia ya wananchi kuona kuwa eneo hilo linatengwa na kunakuwepo na viwanda ili wananchi wa Mbeya waweze kupata ajira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hiyo mikakati mizuri, ninaomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Je, ni lini sasa Serikali itapeleka pesa kwa ajili ya kumalizia Kiwanda cha Kuchakata Nyama ambacho kimejengwa na Halmashauri ya Mbeya na ambacho vyombo vyote, vifaa vyote zaidi ya miaka miwili sasa viko mle ndani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa vile kuna wafugaji wengi katika Kata ya Mjele na tatizo lao kubwa ni mabwawa ya maji, je, ni lini Serikali sasa itapeleka miundombinu ya mabwawa ya maji kwa ajili ya mifugo na binadamu? Nakushukuru.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru kwamba amekubaliana na majibu ya Serikali kwenye swali la msingi na katika maswali yake mawili ya nyongeza, la kwanza, kuhusu mradi wa kiwanda cha kusindika nyama pale Mbalizi ambao uliwasilishwa na Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya Vijijini TAMISEMI kwa ajili ya kufikiriwa kupewa fedha ni miongoni mwa miradi ya kimkakati katika halmashauri hiyo ambayo imeombewa fedha kwenye dirisha maalum la miradi ambayo ni miradi ya kibiashara.
Kwa hiyo, mchakato wake bado unaendelea, kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha miradi hiyo yote bado inafanyiwa upembuzi maalum ili utakapokamilika miradi ile ambayo itapatiwa fedha wahusika wa Halmashauri wataarifiwa. Hata hivyo ninaamini mradi huo ni mzuri na una faida na miradi kama hiyo Mbeya haipo mingi, kwa hiyo, ninaamini utapewa kipaumbele unaostahili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili ni kuhusu bwawa kwenye eneo la wafugaji. Najua Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi alitembelea eneo hilo na akatoa ahadi. Mimi nataka nimwambie kwamba Serikali hii ni moja, nitafuatilia mimi mwenyewe kwa Wizara ya Mifugo ili kuhakikisha kwamba Halmashauri na wakazi wa eneo hilo wafugaji wanapata kile ambacho Mheshimiwa Naibu Waziri alikiahidi. Ahsante.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Katika Mji Mdogo wa Mbalizi kuna ardhi ya ukubwa wa zaidi ya ekari 5,000 iliyotengwa kwa ajili ya Tanganyika Packers ambayo haijaendelezwa kwa zaidi ya miaka 30 iliyopita. (a) Je, ni lini Serikali itawarudishia wananchi wa Mji Mdogo wa Mbalizi eneo hilo kwa lengo la kuliendeleza kwa kubadili matumizi kutokana na kukua kwa kasi kubwa kwa Mji wa Mbalizi? (b) Pamoja na kubadili matumizi ya ardhi hiyo, je, Serikali ina mpango gani kwa wananchi wanaotumia ardhi hiyo hasa ikizingatiwa kuwa wengi wao hawakupewa fidia yoyote?

Supplementary Question 2

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, matatizo yaliyoko huko Mbalizi yanafanana kabisa na yaliyoko katika Halmashauri ya Itigi ambapo shamba la Tanganyika Packers eka 45,000 ambalo lipo pale kwa miaka mingi limetelekezwa na Serikali imekuwa na kauli tata juu ya shamba hili wakati tukiliomba lirudishwe kwa wananchi au kuanzishwe mradi mwingine, kwamba litarudishwa, baadae Serikali inasema italichukua. Sasa nini kauli sahihi ya Serikali kwa shamba la Tanganyika Packers ambalo limeachwa na limetelekezwa kwa muda mrefu katika Halmashauri ya Itigi?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nisisitize kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi, kwamba maeneo kama lile la Tanganyika Packers Mbeya na maeneo mengine ya aina hiyo Serikali haina nia ya kubadilisha matumizi ya msingi yaliyokusudiwa kwa ajili ya kuendeleza maeneo hayo katika sekta ya viwanda.
Kwa hiyo, maeneo hayo ni lazima yaendelee kutengwa na kutunzwa kwa ajili ya maendeleo ya sekta ya viwanda. Kwa hiyo, maeneo hayo ni ya uwekezaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ndugu yangu Mheshimiwa Yahaya naomba tushirikiane na Halmashauri ya Wilaya ya Itigi kuhakikisha kwamba eneo hilo linaendelea kulindwa na miongoni mwa maeneo ambayo ni ya halmashauri ya wilaya ambayo mnatakiwa myalinde kikamilifu kwa ajili ya sekta ya viwanda na uwekezaji kwa ujumla ni eneo hilo, kwa hiyo, naomba sana tushirikiane katika hilo.

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Katika Mji Mdogo wa Mbalizi kuna ardhi ya ukubwa wa zaidi ya ekari 5,000 iliyotengwa kwa ajili ya Tanganyika Packers ambayo haijaendelezwa kwa zaidi ya miaka 30 iliyopita. (a) Je, ni lini Serikali itawarudishia wananchi wa Mji Mdogo wa Mbalizi eneo hilo kwa lengo la kuliendeleza kwa kubadili matumizi kutokana na kukua kwa kasi kubwa kwa Mji wa Mbalizi? (b) Pamoja na kubadili matumizi ya ardhi hiyo, je, Serikali ina mpango gani kwa wananchi wanaotumia ardhi hiyo hasa ikizingatiwa kuwa wengi wao hawakupewa fidia yoyote?

Supplementary Question 3

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, moja kati ya maeneo ambayo kulikuwa kuna viwanda vya Tanganyika Packers ni Jimbo la Kawe, Kata ya Kawe ambayo miaka sita iliyopita kwa kushirikiana na Serikali ya Awamu ya Nne tulifanikiwa kuliokoa eneo husika kutoka kwa waliokuwa wawekezaji uchwara na hatimaye Shirika la Nyumba la Taifa likakabidhiwa kupewa jukumu la kujenga Kawe Mpya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tokea Awamu ya Tano imeingia madarakani…
Mheshimiwa Mwenyekiti, tokea Awamu ya Tano imeingia madarakani, mradi ule ambao ulikuwa unahusisha nyumba zaidi ya 50,000 ni kama vile umekwama, matokeo yake eneo lile linakuwa kama sehemu ya genge la majambazi na wahalifu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ninataka Serikali iniambie, ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba ujenzi wa Kawe Mpya ya kisasa unafanyika kama ambavyo ilikuwa ni katika mpango wa miaka mitano na mwaka mmoja mmoja wa Serikali?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli mpango wa Serikali kujenga nyumba kama ilivyokuwa imepangwa kwa National Housing ulikuwa umepangwa na ulikuwa unaendelea vizuri, lakini mpango ule ulisimama baada ya kuja kuongeza nguvu katika ujenzi wa nyumba za Makao Makuu hapa Dodoma. Hata hivyo, kwa sababu suala zima la ujenzi wa nyumba za hapa Dodoma unaendelea vizuri, miradi mingine yote iliyokuwa imesimama sasa hivi wataanza kuitekeleza kwa sababu utaratibu tayari umeshawekwa vizuri.

Name

Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Katika Mji Mdogo wa Mbalizi kuna ardhi ya ukubwa wa zaidi ya ekari 5,000 iliyotengwa kwa ajili ya Tanganyika Packers ambayo haijaendelezwa kwa zaidi ya miaka 30 iliyopita. (a) Je, ni lini Serikali itawarudishia wananchi wa Mji Mdogo wa Mbalizi eneo hilo kwa lengo la kuliendeleza kwa kubadili matumizi kutokana na kukua kwa kasi kubwa kwa Mji wa Mbalizi? (b) Pamoja na kubadili matumizi ya ardhi hiyo, je, Serikali ina mpango gani kwa wananchi wanaotumia ardhi hiyo hasa ikizingatiwa kuwa wengi wao hawakupewa fidia yoyote?

Supplementary Question 4

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu linakuja kwenye haya mashamba. Katika Jimbo la Mlimba, Kata ya Namwawala, Vijiji vya Idandu, Miomboni na Namwawala sasa hivi kuna hekaheka kubwa kuzuia wananchi kwenda kulima mashamba yaliyokuwa eneo la Ramsar na matokeo yake na huku kijijini kwenyewe wanasema kuna uwekezaji wa sukari, lakini mpaka sasa Serikali hawasemi chochote kuhusu wananchi hao na Waziri Mkuu anajua, aliniahidi atakuja kutatua hiyo migogoro ili wananchi wawe kama outgrowers.
Je, lini sasa Waziri atakwenda Jimbo la Mlimba katika maeneo haya kuhakikisha kwamba wananchi hawa wanapata mahali salama pa kulima na pa kuishi katika Kata ya Namwawala na Mofu?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama alivyosema yeye mwenyewe, maeneo ambayo ni mashamba halafu hapohapo akataja jambo kubwa kabisa katika mazingira duniani linaitwa Ramsar, maeneo ambayo yametengwa kama Ramsar Sites ni maeneo ambayo hayastahili kuvamiwa au kutumiwa kwa maendeleo ya aina yoyote, yanatakiwa kulindwa, kuhifadhiwa kwa ajili ya mazingira. Mimi nadhani suala hili tutaendelea kushirikiana na Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira kuhakikisha kwamba maeneo hayo yanatunzwa vizuri. Ahsante sana. (Makofi)

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, (MUUNGANO NA MAZINGIRA): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuongeza katika majibu mazuri kabisa yaliyotolewa na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Ni sahihi kabisa kwamba uhai wa ikolojia ya Mto Rufiji unategemea sana afya ya maeneo haya yaliyohifadhiwa kwa mujibu wa Mkataba wa Kimataifa wa Ramsar. Kwa hiyo matumizi ya maeneo yale lazima yawe uangalifu na Serikali kabla ya kuruhusu kazi za kilimo, ufugaji na matumizi ya kibinadamu, lazima ifanye utafiti wa kutosha na wa kujiridhisha ili tusije tukaharibu mifumo ya ki-ikolojia ya nchi yetu kwa kuruhusu shughuli za kibinadamu kwenye maeneo ambayo hayastahili kabisa kufanyika shughuli hizo.