Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Primary Question

MHE. RHODA E. KUNCHELA aliuliza:- a) Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa ardhi kati ya Hifadhi na wananchi katika Kata ya Kapalamsenga, Isengule na Ikola? b) Kwa kuwa migogoro hiyo imechukua muda mrefu bila suluhu hivyo kusababisha usumbufu na hasara kwa wananchi; Je, Serikali haioni kuwa migogoro hiyo imesababisha umaskini mkubwa kwa wananchi kushindwa kuendeleza shughuli za kiuchumi kwenye maeneno yao hivyo ifanye haraka kutafuta ufumbuzi?

Supplementary Question 1

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa majibu haya inaonesha kabisa dhahiri kwamba Mheshimiwa Waziri amedanganywa na uhalisia wa wananchi wa Jimbo la Mpanda Vijijini, kutokana na swali hili kwa sababu imekuwa ni mara ya tatu nauliza swali hili, lakini pia Serikali imeshindwa kutatua migogoro pamoja na mauaji yanayoendelea katika kata hizi, Kata ya Kapalamsenga, Ikola, Isengule, Iteteme pamoja na Kalema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika vijiji hivi wananchi wamekuwa wanateswa na askari wa Wanyamapori na mwaka jana wamekufa zaidi ya vijana wawili kwa kupigwa risasi na askari wa wanyamapori. Ni nini tamko la Serikali kutokana na vifo na manyanyaso yanayoendelea katika Jimbo hili la Mpanda Vijijini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; katika majibu haya ndiyo maana nikasema kwamba Mheshimiwa Waziri, amedanganywa. Hakuna ushirikishwaji wowote kati ya Vijiji, Vitongoji pamoja na wananchi. Ni kwa nini Serikali inatumia nguvu wakati wananchi wanatakiwa wapewe elimu, washirikishwe kuliko kulazimishwa kupeleka hizo GN kwenye maeneo ambayo vijiji hawajapewa ramani husika kujua na kutambua mipaka yao? (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niseme tu kwamba siyo azma ya Serikali kuhakikisha kwamba wananchi wake wanateswa, hiyo haturuhusu. Haturuhusu kabisa, lakini pale ambapo wananchi wale ambao wanaenda kuingia katika maeneo ya hifadhi bila kufuata taratibu, hatua za kisheria lazima zichukuliwe. Kuchukuliwa siyo kuwatesa wala kuwapiga, lazima wanakamatwa wanapelekwa katika mikondo ya sheria na hapo wanashitakiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kwenye maeneo ya Mheshimiwa kuna tatizo la namna hiyo, basi nitaomba tuwasiliane baadae ili unipe baadhi ya watu ambao wamepata matatizo hayo, kusudi tuweze kuwachukulia hatua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wote tunafahamu tunapoenda katika mipango ya matumizi bora ya ardhi hasa katika vijiji lazima mipango iwe shirikishi kwa sababu wanaotakiwa kupanga ni wananchi wenyewe wote wanahusika, sasa akiniambia kwamba wananchi hawakushirikishwa kwa kweli nashindwa kuelewa. Huo mpango lazima upitishwe na mkutano wa Kijiji. Sasa ulipitishwaje kama wananchi hawakushirikishwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kama kuna changamoto hizo, basi nitakapokwenda katika hilo eneo basi tukae wote kama Serikali pamoja na wananchi tuone kama kweli hawakushirikishwa au kuna tatizo lingine la mahitaji ya ardhi. (Makofi)

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. RHODA E. KUNCHELA aliuliza:- a) Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa ardhi kati ya Hifadhi na wananchi katika Kata ya Kapalamsenga, Isengule na Ikola? b) Kwa kuwa migogoro hiyo imechukua muda mrefu bila suluhu hivyo kusababisha usumbufu na hasara kwa wananchi; Je, Serikali haioni kuwa migogoro hiyo imesababisha umaskini mkubwa kwa wananchi kushindwa kuendeleza shughuli za kiuchumi kwenye maeneno yao hivyo ifanye haraka kutafuta ufumbuzi?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Migogoro kati ya hifadhi zetu na wananchi itaendelea kwa muda, kwa sababu wananchi wanaongezeka, wanyama wanaongezeka, ardhi iko pale pale. Wanyama hawawezi kufanya uzazi wa mpango, lakini sisi tunaweza. Je, ni lini Serikali yetu itakuja na sera na mpango kabambe wa uzazi wa mpango kwa wanadamu ili tuweze kudhibiti ongezeko hili la watu ambalo linaweza likaathiri hata shughuli nyingine za kiuchumi kama afya, elimu na kadhalika? (Kicheko)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba idadi ya wananchi imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka. Wakati tunapata uhuru mwaka 1961 idadi ya Watanzania walikuwa ni milioni 10.3, sasa hivi mwaka 2018 idadi ya Watanzania tunakadiriwa kufika milioni 54.2. Kwa hiyo utakuta kwamba sasa idadi imeongezeka kwa kiwango kikubwa wakati ardhi imebaki vilevile haijaongezeka. Kwa hiyo na hii ina maana gani, ina maana tuje na mipango madhubuti ya kuhakikisha moja, tunadhibiti idadi ya ongezeko la watu lakini la pili, matumizi bora ya ardhi yetu tuliyonayo, ndiyo maana tumeweka mkazo katika hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu hili wazo la mpango wa uzazi wa mpango, naomba nilichukue kama Serikali tutalifanyia kazi kuhakikisha kwamba tunawahimiza Watanzania wote tuwe na uzazi wa mpango ili kusudi tuzae idadi ya watoto inayolingana na ardhi ile tuliyonayo. (Makofi)

Name

Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Primary Question

MHE. RHODA E. KUNCHELA aliuliza:- a) Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa ardhi kati ya Hifadhi na wananchi katika Kata ya Kapalamsenga, Isengule na Ikola? b) Kwa kuwa migogoro hiyo imechukua muda mrefu bila suluhu hivyo kusababisha usumbufu na hasara kwa wananchi; Je, Serikali haioni kuwa migogoro hiyo imesababisha umaskini mkubwa kwa wananchi kushindwa kuendeleza shughuli za kiuchumi kwenye maeneno yao hivyo ifanye haraka kutafuta ufumbuzi?

Supplementary Question 3

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa majibu haya inaonesha kabisa dhahiri kwamba Mheshimiwa Waziri amedanganywa na uhalisia wa wananchi wa Jimbo la Mpanda Vijijini, kutokana na swali hili kwa sababu imekuwa ni mara ya tatu nauliza swali hili, lakini pia Serikali imeshindwa kutatua migogoro pamoja na mauaji yanayoendelea katika kata hizi, Kata ya Kapalamsenga, Ikola, Isengule, Iteteme pamoja na Kalema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika vijiji hivi wananchi wamekuwa wanateswa na askari wa Wanyamapori na mwaka jana wamekufa zaidi ya vijana wawili kwa kupigwa risasi na askari wa wanyamapori. Ni nini tamko la Serikali kutokana na vifo na manyanyaso yanayoendelea katika Jimbo hili la Mpanda Vijijini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; katika majibu haya ndiyo maana nikasema kwamba Mheshimiwa Waziri, amedanganywa. Hakuna ushirikishwaji wowote kati ya Vijiji, Vitongoji pamoja na wananchi. Ni kwa nini Serikali inatumia nguvu wakati wananchi wanatakiwa wapewe elimu, washirikishwe kuliko kulazimishwa kupeleka hizo GN kwenye maeneo ambayo vijiji hawajapewa ramani husika kujua na kutambua mipaka yao? (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niseme tu kwamba siyo azma ya Serikali kuhakikisha kwamba wananchi wake wanateswa, hiyo haturuhusu. Haturuhusu kabisa, lakini pale ambapo wananchi wale ambao wanaenda kuingia katika maeneo ya hifadhi bila kufuata taratibu, hatua za kisheria lazima zichukuliwe. Kuchukuliwa siyo kuwatesa wala kuwapiga, lazima wanakamatwa wanapelekwa katika mikondo ya sheria na hapo wanashitakiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kwenye maeneo ya Mheshimiwa kuna tatizo la namna hiyo, basi nitaomba tuwasiliane baadae ili unipe baadhi ya watu ambao wamepata matatizo hayo, kusudi tuweze kuwachukulia hatua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wote tunafahamu tunapoenda katika mipango ya matumizi bora ya ardhi hasa katika vijiji lazima mipango iwe shirikishi kwa sababu wanaotakiwa kupanga ni wananchi wenyewe wote wanahusika, sasa akiniambia kwamba wananchi hawakushirikishwa kwa kweli nashindwa kuelewa. Huo mpango lazima upitishwe na mkutano wa Kijiji. Sasa ulipitishwaje kama wananchi hawakushirikishwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kama kuna changamoto hizo, basi nitakapokwenda katika hilo eneo basi tukae wote kama Serikali pamoja na wananchi tuone kama kweli hawakushirikishwa au kuna tatizo lingine la mahitaji ya ardhi. (Makofi)

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. RHODA E. KUNCHELA aliuliza:- a) Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa ardhi kati ya Hifadhi na wananchi katika Kata ya Kapalamsenga, Isengule na Ikola? b) Kwa kuwa migogoro hiyo imechukua muda mrefu bila suluhu hivyo kusababisha usumbufu na hasara kwa wananchi; Je, Serikali haioni kuwa migogoro hiyo imesababisha umaskini mkubwa kwa wananchi kushindwa kuendeleza shughuli za kiuchumi kwenye maeneno yao hivyo ifanye haraka kutafuta ufumbuzi?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Migogoro kati ya hifadhi zetu na wananchi itaendelea kwa muda, kwa sababu wananchi wanaongezeka, wanyama wanaongezeka, ardhi iko pale pale. Wanyama hawawezi kufanya uzazi wa mpango, lakini sisi tunaweza. Je, ni lini Serikali yetu itakuja na sera na mpango kabambe wa uzazi wa mpango kwa wanadamu ili tuweze kudhibiti ongezeko hili la watu ambalo linaweza likaathiri hata shughuli nyingine za kiuchumi kama afya, elimu na kadhalika? (Kicheko)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba idadi ya wananchi imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka. Wakati tunapata uhuru mwaka 1961 idadi ya Watanzania walikuwa ni milioni 10.3, sasa hivi mwaka 2018 idadi ya Watanzania tunakadiriwa kufika milioni 54.2. Kwa hiyo utakuta kwamba sasa idadi imeongezeka kwa kiwango kikubwa wakati ardhi imebaki vilevile haijaongezeka. Kwa hiyo na hii ina maana gani, ina maana tuje na mipango madhubuti ya kuhakikisha moja, tunadhibiti idadi ya ongezeko la watu lakini la pili, matumizi bora ya ardhi yetu tuliyonayo, ndiyo maana tumeweka mkazo katika hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu hili wazo la mpango wa uzazi wa mpango, naomba nilichukue kama Serikali tutalifanyia kazi kuhakikisha kwamba tunawahimiza Watanzania wote tuwe na uzazi wa mpango ili kusudi tuzae idadi ya watoto inayolingana na ardhi ile tuliyonayo. (Makofi)

Name

Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Primary Question

MHE. RHODA E. KUNCHELA aliuliza:- a) Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa ardhi kati ya Hifadhi na wananchi katika Kata ya Kapalamsenga, Isengule na Ikola? b) Kwa kuwa migogoro hiyo imechukua muda mrefu bila suluhu hivyo kusababisha usumbufu na hasara kwa wananchi; Je, Serikali haioni kuwa migogoro hiyo imesababisha umaskini mkubwa kwa wananchi kushindwa kuendeleza shughuli za kiuchumi kwenye maeneno yao hivyo ifanye haraka kutafuta ufumbuzi?

Supplementary Question 5

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa majibu haya inaonesha kabisa dhahiri kwamba Mheshimiwa Waziri amedanganywa na uhalisia wa wananchi wa Jimbo la Mpanda Vijijini, kutokana na swali hili kwa sababu imekuwa ni mara ya tatu nauliza swali hili, lakini pia Serikali imeshindwa kutatua migogoro pamoja na mauaji yanayoendelea katika kata hizi, Kata ya Kapalamsenga, Ikola, Isengule, Iteteme pamoja na Kalema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika vijiji hivi wananchi wamekuwa wanateswa na askari wa Wanyamapori na mwaka jana wamekufa zaidi ya vijana wawili kwa kupigwa risasi na askari wa wanyamapori. Ni nini tamko la Serikali kutokana na vifo na manyanyaso yanayoendelea katika Jimbo hili la Mpanda Vijijini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; katika majibu haya ndiyo maana nikasema kwamba Mheshimiwa Waziri, amedanganywa. Hakuna ushirikishwaji wowote kati ya Vijiji, Vitongoji pamoja na wananchi. Ni kwa nini Serikali inatumia nguvu wakati wananchi wanatakiwa wapewe elimu, washirikishwe kuliko kulazimishwa kupeleka hizo GN kwenye maeneo ambayo vijiji hawajapewa ramani husika kujua na kutambua mipaka yao? (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niseme tu kwamba siyo azma ya Serikali kuhakikisha kwamba wananchi wake wanateswa, hiyo haturuhusu. Haturuhusu kabisa, lakini pale ambapo wananchi wale ambao wanaenda kuingia katika maeneo ya hifadhi bila kufuata taratibu, hatua za kisheria lazima zichukuliwe. Kuchukuliwa siyo kuwatesa wala kuwapiga, lazima wanakamatwa wanapelekwa katika mikondo ya sheria na hapo wanashitakiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kwenye maeneo ya Mheshimiwa kuna tatizo la namna hiyo, basi nitaomba tuwasiliane baadae ili unipe baadhi ya watu ambao wamepata matatizo hayo, kusudi tuweze kuwachukulia hatua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wote tunafahamu tunapoenda katika mipango ya matumizi bora ya ardhi hasa katika vijiji lazima mipango iwe shirikishi kwa sababu wanaotakiwa kupanga ni wananchi wenyewe wote wanahusika, sasa akiniambia kwamba wananchi hawakushirikishwa kwa kweli nashindwa kuelewa. Huo mpango lazima upitishwe na mkutano wa Kijiji. Sasa ulipitishwaje kama wananchi hawakushirikishwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kama kuna changamoto hizo, basi nitakapokwenda katika hilo eneo basi tukae wote kama Serikali pamoja na wananchi tuone kama kweli hawakushirikishwa au kuna tatizo lingine la mahitaji ya ardhi. (Makofi)

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. RHODA E. KUNCHELA aliuliza:- a) Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa ardhi kati ya Hifadhi na wananchi katika Kata ya Kapalamsenga, Isengule na Ikola? b) Kwa kuwa migogoro hiyo imechukua muda mrefu bila suluhu hivyo kusababisha usumbufu na hasara kwa wananchi; Je, Serikali haioni kuwa migogoro hiyo imesababisha umaskini mkubwa kwa wananchi kushindwa kuendeleza shughuli za kiuchumi kwenye maeneno yao hivyo ifanye haraka kutafuta ufumbuzi?

Supplementary Question 6

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Migogoro kati ya hifadhi zetu na wananchi itaendelea kwa muda, kwa sababu wananchi wanaongezeka, wanyama wanaongezeka, ardhi iko pale pale. Wanyama hawawezi kufanya uzazi wa mpango, lakini sisi tunaweza. Je, ni lini Serikali yetu itakuja na sera na mpango kabambe wa uzazi wa mpango kwa wanadamu ili tuweze kudhibiti ongezeko hili la watu ambalo linaweza likaathiri hata shughuli nyingine za kiuchumi kama afya, elimu na kadhalika? (Kicheko)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba idadi ya wananchi imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka. Wakati tunapata uhuru mwaka 1961 idadi ya Watanzania walikuwa ni milioni 10.3, sasa hivi mwaka 2018 idadi ya Watanzania tunakadiriwa kufika milioni 54.2. Kwa hiyo utakuta kwamba sasa idadi imeongezeka kwa kiwango kikubwa wakati ardhi imebaki vilevile haijaongezeka. Kwa hiyo na hii ina maana gani, ina maana tuje na mipango madhubuti ya kuhakikisha moja, tunadhibiti idadi ya ongezeko la watu lakini la pili, matumizi bora ya ardhi yetu tuliyonayo, ndiyo maana tumeweka mkazo katika hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu hili wazo la mpango wa uzazi wa mpango, naomba nilichukue kama Serikali tutalifanyia kazi kuhakikisha kwamba tunawahimiza Watanzania wote tuwe na uzazi wa mpango ili kusudi tuzae idadi ya watoto inayolingana na ardhi ile tuliyonayo. (Makofi)