Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Marwa Ryoba Chacha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. MARWA R. CHACHA aliuliza:- Kumekuwepo na tabia ya askari wa SENAPA kuwakamata wananchi ndani ya hifadhi na wakati mwingine wasipouawa huwapeleka mbali na Mahakama za Wilaya ya Serengeti. (a) Je, ni lini vitendo vya mauaji ya watu wanaozunguka Hifadhi ya Serengeti vitakoma? (b) Je, ni lini askari wa SENAPA wataacha kuwapeleka watuhumiwa waliokamatwa ndani ya hifadhi nje ya Mahakama za Wilaya?

Supplementary Question 1

MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Waziri, wananchi wa vijiji vya Merenga, Machochwe, Nyamakendo, Mbalibali, Tamkeri, Bisarara, Mbilikili, Bonchugu, Miseke na Pakinyigoti wamenituma nimwombe Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli aende akawasikilize matatizo yao, lakini Mheshimiwa Rais, Dkt. Magufuli wa Wizara ya Maliasili na Utalii ni Mheshimiwa Waziri.
Je, uko tayari baada ya Bunge hili kuambatana na mimi kwenda kusikiliza matatizo yao? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Wananchi wa vijiji vilivyopo kando kando ya Hifadhi ya Serengeti, mapori ya akiba ya Ikorongo na Gurumeti pamoja na Ikoo na WMA kazi yao kubwa ilikuwa ni uwindaji, ufugaji na kilimo. Uwindaji sasa hivi hawawindi, maana wakienda kuwinda hawarudi; mifugo yao imetaifishwa; mazao yao ya kilimo tembo wanakula; ninyi kama Wizara, nini mbadala mnaowasaidia wananchi wa maeneo haya ili waweze kujikimu kiuchumi? (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kwamba kwanza naomba nimhakikishie tu kwamba niko tayari wakati wowote pale ambapo muda utaruhusu tutapanga, lazima twende tukatembelee katika yale maeneo. Hiyo inatokana na kwamba sasa hivi tuna mpango kabambe wa kuhakikisha kwamba maeneo yote yanayopakana na Hifadhi za Taifa, lazima vijiji vyote vile vipimwe vizuri, tuweke mipaka vizuri lakini pia tuimarishe ule ulinzi katika yale maeneo hasa kule ambako kumekuwa na changamoto nyingi ambapo wanyamapori wamekuwa wakiharibu mazao na shughuli za wananchi wanazofanya katika yale maeneo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, pia tutaweka minara, pamoja na kutumia ndege zisizokuwa na Rubani. Kwa hiyo, mambo mengi tutayafanya kuhakikisha kwamba haya yanafanyika. Ili kufanya hayo, lazima tufike na tuone kwamba wananchi wanaondokana na hizi changamoto.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu hatua mbadala; sasa hivi tunatoa elimu ni nini kinaweza kufanyika katika yale maeneo yaliyo jirani na hifadhi? Kwa sababu ukipanda yale mazao ambayo wanyamapori wanayapenda, ni wazi kabisa kwamba yataliwa na wanyamapori. Ukipanda yale mazao ambayo wanyamapori hawayapendi, wanayaogopa, basi kidogo hii itasaidia.
Mheshimiwa Naibu Spika, tutakwenda kukaa pamoja na Mheshimiwa Mbunge na wananchi kwa pamoja, tutashauriana kuona ni aina gani ya mazao ambayo wananchi wa maeneo yale watashauriwa kwamba wayapande ili kuondokana na hii migogoro ambayo imekuwa ikijitokeza katika hayo maeneo. (Makofi)

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. MARWA R. CHACHA aliuliza:- Kumekuwepo na tabia ya askari wa SENAPA kuwakamata wananchi ndani ya hifadhi na wakati mwingine wasipouawa huwapeleka mbali na Mahakama za Wilaya ya Serengeti. (a) Je, ni lini vitendo vya mauaji ya watu wanaozunguka Hifadhi ya Serengeti vitakoma? (b) Je, ni lini askari wa SENAPA wataacha kuwapeleka watuhumiwa waliokamatwa ndani ya hifadhi nje ya Mahakama za Wilaya?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza naishukuru Serikali kwa kutoa kifuta machozi takribani milioni nane kwa ajili ya wananchi waliopoteza maisha yao na wale walioathiriwa na wanyama wakali.
Mheshimiwa Naibu Spika, mnamo mwaka 2016 Serikali iliahidi kufanya ziara katika Tarafa ya Daudi na Tarafa ya Ndekoti kwa ajili ya wananchi ambao mali zao na mazao yameharibiwa na wanyama wakali, lakini hadi sasa Serikali haijatimiza ahadi yake hiyo kwa kuwa wale waliokuwa kwenye Wizara walibadilishwa.
Je, ni lini Serikali itafanya ziara katika Tarafa ya Daudi na Tarafa ya Ndekoti kwa ajili ya wananchi ambao mali zao zimeathiriwa na wanyama ikiwemo mazao na hawajapata kufidiwa hadi sasa? Ahsante.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kwamba inawezekana kulikuwa na ahadi ya kwamba viongozi wa Kitaifa wataenda kutembelea katika lile eneo.
Naomba tu nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hata kama viongozi wa kitaifa hawajafika, bado wapo Watendaji wetu ambao lazima wafike katika yale maeneo na wahakikishe kwamba wanahakiki mali zilizopotea, wanahakiki uharibifu uliofanyika kusudi wale wananchi wanaostahili kupewa kile kifuta jasho au kifuta machozi, waweze kulipwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kwa nafasi hii, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba leo hii nitawaagiza watendaji wafike katika lile eneo ili wakutane na hao wananchi, wafanye tathmini na tuone ni kiasi gani wananchi wale wanastahili kulipwa kwa mujibu wa kanuni zetu tulizonazo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu utayari, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutakuwa tayari, tutakuja pia kuhakikisha kwamba haya yote yanatekelezeka na wananchi waweze kuona kwamba Serikali yao inawajali vizuri. (Makofi)

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE. MARWA R. CHACHA aliuliza:- Kumekuwepo na tabia ya askari wa SENAPA kuwakamata wananchi ndani ya hifadhi na wakati mwingine wasipouawa huwapeleka mbali na Mahakama za Wilaya ya Serengeti. (a) Je, ni lini vitendo vya mauaji ya watu wanaozunguka Hifadhi ya Serengeti vitakoma? (b) Je, ni lini askari wa SENAPA wataacha kuwapeleka watuhumiwa waliokamatwa ndani ya hifadhi nje ya Mahakama za Wilaya?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi na mimi niweze kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa matatizo yaliyopo katika Jimbo la Serengeti yanafanana kabisa na matatizo yaliyopo katika Jimbo la Kavuu hasa katika Kata za Chamalendi, Mwamapuli, Majimoto na vitongoji vyake; kumekuwa na matatizo ambayo wananchi hasa wafugaji wamekuwa wakisukumizwa na askari wa wanyamapori ndani ya Mbuga ya Katavi na wamekuwa wakipotea na mara nyingi wakiwa wakitafutwa na ndugu zao ni nguo tu zinapatikana:-
Je, Serikali inasema nini sasa kwa ujumla kuhusu askari wote wa wanyamapori wanaofanya kazi katika mbuga zote za National Park katika kuhakikisha usalama wa wale wanaowaita majangili wakati sio majangili? Kwa sababu tu wanakuwa wameingia kwenye mbuga, kwa hiyo, wataitwa majangili.
Je, Serikali inasema nini kuhusu Askari hao ambao wamekuwa wakiwateka wananchi na kuwapora ng’ombe zao na mali…

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba niseme tu kwamba sina taarifa kamili kwamba askari wetu wamekuwa wakiwakamata watu na kuwaingiza kwenye hifadhi halafu wanapotea moja kwa moja. Hizo taarifa hatunazo kama Serikali na kama Mheshimiwa Mbunge anazo na anao ushahidi wa namna hiyo, basi nitaomba nikae naye ili aweze kunipa hayo majina ya watu ambao wamepotea kusudi Serikali iweze kuchukua hatua zinazostahili.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu namna ya kuboresha yale maeneo, naomba nitumie nafasi hii kuwaomba wananchi wote wanaopakana na hifadhi zetu kuhakikisha kwamba wanazingatia taratibu, sheria, kanuni na miongozo iliyopo. Hawaruhusiwi kuingia bila kibali kwenye hifadhi. Kwa kawaida ukiingia kwenye hifadhi bila kibali, ni vigumu sana kujua yupi ni jangili, yupi sio jangili. Kwa hiyo, ili kuweza kuondokana na hilo, ni kuwaomba wananchi kutoingia katika maeneo ya hifadhi ili kusudi tuondokane na hilo tatizo.