Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA (K.n.y. MHE. KEMILEMBE J. LWOTA) aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kumalizia ujenzi wa maboma ya Zahanati yaliyoanzishwa kwa juhudi za wananchi pamoja na kuyawekea vifaa tiba?

Supplementary Question 1

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Wizara wanakiri kwamba kumekuwa na changamoto kutokana na maboma mengi ambavyo yamekuwa katika Halmashauri zetu, lakini pamoja na mkakati wao, walipofanya utafiti waligundua kwamba Halmashauri hazina uwezo wa kukamilisha maboma yote yanayojengwa kule kwenye Majimbo yetu; na ni ukweli usiopingika kwamba Mfuko wa Pamoja bado hauwezi kutosheleza:-

Sasa ni nini mkakati thabiti hasa wa Serikali kuhakikisha aidha kuwe na mkakati wa kusema kiasi cha maboma kinachopaswa kujengwa kwenye kila Halmashauri ili wao waweze kumalizia au tuendelee na kusubiri ujenzi wa Vituo vya Afya na Zahanati kutoka Mfuko wa Pamoja?

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimetoa majibu kwenye majibu yangu ya msingi; na Mheshimiwa Mbunge naye atakubaliana name kuhusu azma njema ya Serikali ambayo anaiona jinsi ambavyo tunapambana kuhakikisha kwamba tunapeleka huduma kwa maana ya kujenga Vituo vya Afya, Hospitali za Wilaya na Zahanati. Ndiyo maana katika majibu yangu ya msingi nimejibu kwamba ni vizuri tukafungua avenue pale ambapo Halmashauri zile ambazo ambazo zina uwezo, lakini pia kwa kushirikisha wananchi na wadau wengine tuendelee kujenga kwa kushirikiana na Serikali.

Mheshimiwa Spika, ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba tunasogeza huduma za matibabu karibu kabisa na wananchi, lakini pia vipaumbele ni vingi. Kwa hiyo, ni vizuri tukashirikiana pale bajeti inaporuhusu, Serikali inapeleka lakini pia na Halmashauri na wadau wengine ni vizuri wakashiriki katika suala hili muhimu sana kwa wananchi wetu.