Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Primary Question

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM (K.n.y. MHE. MGENI JADI KADIKA) aliuliza:- Katika baadhi ya maeneo hapa nchini ikiwemo Dodoma wapo watoto ambao hutoa huduma ya kubeba mizigo na kupewa ujira mdogo. Kutokana na kufanya kazi hizo ni wazi wanakosa haki za msingi kama elimu na malezi bora. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuondoa tatizo hilo?

Supplementary Question 1

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Nina maswali mawili madogo ya nyongeza. Mheshimiwa Naibu Waziri katika majibu yake kwa swali la msingi la Mheshimiwa Mgeni Jadi Kadika, nataka niwahakikishie tu kwamba bado kuna ongezeko kubwa la watoto hawa katika Barabara ya Sita, Barabara ya Tisa hapa Dodoma na katika Soko la Dodoma la Matunda na Mboga Mboga.

Mheshimiwa Spika, nataka nikuhakikishie kwamba hali hii Jiji la Dodoma wanaifahamu. Sasa utuambia mwarobaini au mkakati madhubuti ama mkakati mahususi wa kuweza kuwasaidia watoto hawa, kwa sababu kila siku ongezeko hili kidogo linatisha.

Mheshimiwa Spika, swali la pili Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kwamba baadhi ya watoto hawa wazazi wao tayari wamefariki kwa maradhi mbalimbali, lakini kuna baadhi ya watoto hawa wazazi wao wako hai na wako katika maeneo ya karibu katika maeneo mbalimbali. Sasa wanasema kwamba watatoa elimu, atuambie mkakati wa ziada kuhakikisha kwamba wale watoto ambao wazazi wao wapo hai wanachukua hatua gani ya dharura kuhakikisha wazazi hawa wanapatikana na suala hili kulikomesha?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, kwanza suala kwamba kuna ongezeko, hiyo inakuwa kidogo ni relative term, kwa sababu ongezeko hilo unalipima kuanzia lini? Kama nilivyojibu katika swali langu la msingi, kwa mujibu wa sheria ni wajibu kuhakikisha kwamba mtoto analelewa katika mazingira mazuri. Jitihada zimefanywa na Serikali kwanza kuwatambua hawa watoto.

Kwa mfano, kwa Mkoa wa Dodoma na hasa Jiji la Dodoma, jitihada za makusudi zimefanyika kwanza kuhakikisha kwamba wale watoto ambao wana wazazi wao wanarudishwa na kuunganishwa na familia kwa sababu wajibu wa kwanza wa kumlea mtoto ni wa familia.

Mheshimiwa Spika, kuna cases kama ambazo watoto wanalazimika kuondoka katika mazingira na kwenda katika mazingira hayo kwa sababu aidha, wameondokewa na wazazi wao kwa magonjwa masuala kama hayo, ndiyo maana katika jibu langu la msingi nimesisitiza kwamba ni wajibu wetu sisi kama jamii kwa ujumla kuhakikisha kwamba watoto ambao wanatakiwa kwenda shule waende shule na kuna mpango wengine wanaweza kupelekwa VETA. Ni jitihada za Serikali kuhakikisha kwamba watoto hawaishi katika mazingira magumu.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM (K.n.y. MHE. MGENI JADI KADIKA) aliuliza:- Katika baadhi ya maeneo hapa nchini ikiwemo Dodoma wapo watoto ambao hutoa huduma ya kubeba mizigo na kupewa ujira mdogo. Kutokana na kufanya kazi hizo ni wazi wanakosa haki za msingi kama elimu na malezi bora. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuondoa tatizo hilo?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa watoto hawa wadogo hawatumiki katika kubeba mizigo tu, lakini kuna wengine ambao hutumika kuwaongoza baadhi ya wazazi au walezi na watu wazima katika kwenda kuombaomba.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwanusuru watoto hawa?

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Toufiq kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, sisi kama Wizara tumefanya sensa ya kubaini watoto ambao wanaishi mitaani au wanaoishi katika mazingira hatarishi katika baadhi ya Majiji na tumebaini idadi na wale ambao tuliwabaini na vyanzo vyao ambavyo vimewasababisha wao kuwa mitaani wengine tumeweza kuwaunganisha na wazazi wao, lakini vile vile, tunaendelea kuchukua hatua mbalimbali kuhakikisha kwamba wale ambao tunawabaini hawana wazazi kabisa, tunawatunza katika nyumba zetu za kuwalelea watoto.

Name

Abdallah Majurah Bulembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Primary Question

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM (K.n.y. MHE. MGENI JADI KADIKA) aliuliza:- Katika baadhi ya maeneo hapa nchini ikiwemo Dodoma wapo watoto ambao hutoa huduma ya kubeba mizigo na kupewa ujira mdogo. Kutokana na kufanya kazi hizo ni wazi wanakosa haki za msingi kama elimu na malezi bora. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuondoa tatizo hilo?

Supplementary Question 3

MHE. ALHAJ ABDALLAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na aliyejibu swali sasa hivi, Jiji ambalo lina watoto wengi kuliko hili, moja ya nane ya Dodoma ni Jiji la Dar es Salaam. Hao wa Dar es Salaam ambao sasa limeitwa Jiji la Utalii, lina wageni wengi na ni wengi, yaani ni wengi kuliko; hatua zipi za makusudi zinachukuliwa kulifanya Jiji la Dar es Salaam kuondoa ombaomba ili hawa watalii wanaonyang’anywa, wanaoibiwa waweze kuwa na raha katika Jiji la Dar es Salaam?

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, sina takwimu za papo kwa papo, lakini kwa ujumla najua katika sensa yetu tuliyofanya, tulibaini kama watoto zaidi 6,000, lakini nahitaji nifanye uhakiki kujua katika Majiji haya ya Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya, Arusha, Dodoma na maeneo mengine ni wapi ambapo takwimu zipo nyingi.

Mheshimiwa Spika, nimwahidi tu Mheshimiwa Mbunge kwamba hiyo taarifa tutampatia. Sisi kama Wizara, tumeendelea kulifanyia kazi suala hili, lakini kama alivyosema katika jibu la msingi la Mheshimiwa Kandege ni kwamba jukumu la malezi ya mtoto ni la familia. Pale inaposhindikana ni jamii ambayo inaizunguka na mwisho pale inapoonekana kabisa hakuna wa kuwasaidia wale watoto, sisi kama Serikali tunachukua majukumu hayo.

Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii kutoa rai kwa jamii kuhakikisha kwamba tunatimiza majukumu yetu ya msingi ya kuwalea watoto kama ilivyoainishwa katika sheria.