Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. PAULINE P. GEKUL (K.n.y. MHE. GODFREY W. MGIMWA) aliuliza:- Tatizo la ukosefu wa nyumba za Walimu kwenye maeneo mengi ya Jimbo la Kalenga kumesababisha Walimu kuhama na hivyo kudhoofisha ukuaji wa elimu kwa ujumla: - (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuisaidia Halmashauri ya Iringa Vijijini ili kuhakikisha inajenga nyumba za kutosha kwa Walimu? (b) Mapato ya ndani ya Halmashauri hii hayatoshi kujenga nyumba za Walimu. Je, nini mkakati wa Serikali juu ya tatizo hili?

Supplementary Question 1

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Spika, nakushukuru naomba niulize maswali mawili ya nyongeza, swali la kwanza Mheshimiwa Naibu Waziri, ukweli ni kwamba halmashauri nyingi hasa za Mijini wamesha exhaust karibia vyanzo vyote vya mapato. Sasa nilifikiri kwamba Serikali ingetusaidia kuweka mpango wa haraka kwa ajili ya nyumba za walimu.

Ni lini Serikali itaweka kwenye bajeti kuu fedha za ujenzi wa nyumba za walimu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili nishukuru kwanza Serikali ilitupatia fedha milioni 152 kwa ajili ya kukamilisha bweni la Sekondari ya Nakwa katika Halmashauri ya Mji wa Babati lakini ujenzi umefika katika upauzi bado finishing, niombe serikali itupatie fedha kwa sababu tatizo la vyanzo vya mapato kuwa vichache kati Halmashauri ya Kalenga ina fafana pia Halmashauri ya Mji wa Babati.

Ni lini Serikali itatupatia fedha kwa ajili ya finishing ya bweni la Sekondari ya Nakwa?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, ni kweli tungependa kuona nyumba za walimu katika maeneo ya jirani ili walimu wetu wasiweze kupata shida wnapotoa huduma na kuhudia vijana wetu katika maeneo mbalimbali na hasa Vijijini. Vilevile tungependa pia kuwa na mabweni ya kutosha kwa watoto wa kike ili kuwapunguzia majanga ya kupata mimba na wakati mwingine mazingira magumu kuplekea kufanya vibaya katika mitihani yao.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba tuko kwenye bajeti ya mwaka huu tumetenga fedha ya kukamilisha nyumba zaidi ya 364 katika maeneo mbalimbali, pia kumalizia mabweni na kumbi mbalimbali. Ningependa niseme tu kwa mfano fedha hizi ambazo zinazungumzwa hapa ambazo tungeweza mkopo ambayo wenzetu humu ndani wametuhujumu kwa kufanya hizi fedha zisiweze kuchelewa zingeweza kunufaisha vijana, watanzania wazalendo wenzetu zaidi ya milioni sita, tungeweza kujenga matundu ya vyoo kwenye mashule ya Sekondari, 1000, tungejenga matundu ya vyoo 2000 katika maeneo mbalimbali, kutengeneza kumbi za mikutano, mabwalo na hosteli mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, naomba tu niseme katika jambo hili ni jambo la mkakati la pamoja Serikali, Waheshimiwa Wabunge na wadau mbalimbali tushirikiane tunapoona kutafuta vyanzo mbalimbali vya mapato wenzetu wanapokula kitumbua wasitie mchanga ili fesha ije katika eneo hili na watanzania wapate huduma kama ambavyo imetupasa kufanya, ahsante.

Name

Justin Joseph Monko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. PAULINE P. GEKUL (K.n.y. MHE. GODFREY W. MGIMWA) aliuliza:- Tatizo la ukosefu wa nyumba za Walimu kwenye maeneo mengi ya Jimbo la Kalenga kumesababisha Walimu kuhama na hivyo kudhoofisha ukuaji wa elimu kwa ujumla: - (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuisaidia Halmashauri ya Iringa Vijijini ili kuhakikisha inajenga nyumba za kutosha kwa Walimu? (b) Mapato ya ndani ya Halmashauri hii hayatoshi kujenga nyumba za Walimu. Je, nini mkakati wa Serikali juu ya tatizo hili?

Supplementary Question 2

MHE. JUSTIN J. MONKO: Mheshimiwa Spika, kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, kwa kuwa Serikali imetueleza kwamba ina mikakati mbalimbali ya kuongeza nyumba za walimu na tatizo hili lililopo katika Jimbo la Kalenga linafafana sana na Jimbo la Singida Kaskazini.

Je, Serikali haioni umuhimu sasa katika bajeti hii ya mwaka 2020/2021 kuanza kutenga fedha kwa ajili kutoa posho maalum kwa walimu ili waweze kukodisha nyumba na waishi katika maeneo ambayo yanastahili, ahsante sana.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, ni mapenzi ya Serikali hii ya Awamu ya Tano kwamba tuwe na uwezo wa kuwawezesha walimu wetu wafanye kazi katika mazingira raisi sana na lipokee ushauri wake na kwa sababu yeye ni Mheshimiwa Mbunge na mchakato huo bahati nzuri unaanzia kwenye ngazi ya halmashauri.

Kwa hiyo, ningeomba Waheshimiwa katika halmashauri zetu pale mchakato unaondelea sasa tunatengeneza bajeti tuangalie uwezekano wa kupunguza adha hii kwa walimu wetu; na sisi kama Serikali ngazi ya TAMISEMI tutalipokea na kuanza kulifanyia kazi.

Mheshimiwa Spika, lakini nitoe wito kwa watanzania tunaoishi katika maeneo ambayo tunatoka hata Waheshimiwa Wabunge na wadau mbalimbali wa elimu hata tukijenga zile nyumba za kawaida na kuweza kuwapangisha walimu kwa bei nafuu walimu wataishi karibu maeno ya shule wataweza kutoa huduma mbalimbali. Tushirikiane pamoja kuweza kupunguza changamoto ya walimu, walimu wafundishe katika maeneo salama, rafiki pia na kodi ambayo ni affordable ili waweze kufanya kazi katika urahisi wake, ahsante sana.

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PAULINE P. GEKUL (K.n.y. MHE. GODFREY W. MGIMWA) aliuliza:- Tatizo la ukosefu wa nyumba za Walimu kwenye maeneo mengi ya Jimbo la Kalenga kumesababisha Walimu kuhama na hivyo kudhoofisha ukuaji wa elimu kwa ujumla: - (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuisaidia Halmashauri ya Iringa Vijijini ili kuhakikisha inajenga nyumba za kutosha kwa Walimu? (b) Mapato ya ndani ya Halmashauri hii hayatoshi kujenga nyumba za Walimu. Je, nini mkakati wa Serikali juu ya tatizo hili?

Supplementary Question 3

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona pamoja na ukosefu wa nyumba za walimu katika Jimbo la Kalenga ni mwaka wa nne sasa walimu hawa hawajapandishwa madaraja na wamekuwa wakipata adha kubwa sana katika masuala hayo ya nyumba.

Ni lini sasa Serikali itawapandisha madaraja walimu hawa ili waweze kuongeza morale katika utendaji kazi wao? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba tuna malalamiko mbalimbali mengi ya walimu katika maeneo mbalimbali ya nchi wakionesha kukerwa na kutopandishwa madaraja.

Niwaombe pia katika jambo hili pia kwa sababu ya mchakato wa kupandisha madaraja unaanzia kule ngazi ya halmashauri zetu ambako kila Mbunge pale yupo, mchakato unaanzia pale ngazi ile inaenda kwa Afisa Utumishi inakuja kwa Mkurugenzi mpaka maeneo mengine. Tupeane taarifa tumeshatoa maelekezo tumekutana walimu wote na mawakilishi wao kwa maana Maafisa Elimu wa Wilaya na Mikoa na Wakurugenzi na Makatibu Tawala, juzi walikuwa hapa Dodoma, tukaagiza kwamba tupate taarifa.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu unakuta, mwalimu yupo kwenye halmashauri yako Mheshimiwa Mbunge, lakini mwenzake yeye kapanda mara ya kwanza, mara ya mwisho 2013 mpaka leo hajapanda, lakini kuna wengine wamekuwa wakipandishwa. Kwa hiyo, tukipata taarifa mahusui katika maeneo haya tutazifanyiakazi haraka sana. Walimu wanalalamika na wanakwazwa, tungependa tuwaondolee adha, yale mambo ambayo yapo ndani ya uwezo tuyaondoe ili tuondoe kero kwa walimu wetu waendelee kufundisha kwa moyo. Ahsante sana.