Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa ardhi kati ya hifadhi ya Mpanga na wananchi wa Wilaya ya Wanging‟ombe?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri. Nina swali moja tu la nyongeza, nataka kujua katika hifadhi ya Kitulo iliyokuwepo Makete kuna migogoro mikubwa sana pale kati ya hifadhi ya Kitulo na Vijiji vinavyozunguka hifadhi hiyo. Je, Serikali imejipangaje kuhakikisha kwamba, matatizo ya mipaka kati ya wanavijiji wanaozunguka hifadhi ya Kitulo na hifadhi ya Kitulo ya Taifa?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la Kitulo na migogoro ya ardhi inayotokana na wananchi wanaoishi katika Vijiji vinavyozunguka hifadhi hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, jana wakati tukiwa tunatoa ufafanuzi wa hoja nzima ya migogoro ya ardhi katika maeneo ya hifadhi na yanayopakana nayo, tulitoa ufafanuzi kama ifuatavyo na ambao unahusisha pia hifadhi ya Kitulo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imejipanga kwa ajili ya migogoro yote ya ardhi ikiwemo ile inayohusisha hifadhi. Kwa hiyo, kwa hifadhi ya Kitulo tunakwenda kuijumuisha hifadhi ya Kitulo kwenye orodha ya hifadhi zote ambazo zina migogoro kwenda kushughulikia migogoro hiyo kwa kuitazama inahusisha Wizara zipi kati ya zile Wizara sita zilizotajwa. Kwamba, tunakwenda kutazama migogoro hiyo chanzo chake ni nini, inahusu nini na suluhisho lake ni nini kwa kushirikisha Serikali katika Wizara zote zitakazohusika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema jana wakati tunapokwenda kupitia migogoro hiyo tunakwenda kuzingatia maslahi ya Taifa zaidi.

Name

Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa ardhi kati ya hifadhi ya Mpanga na wananchi wa Wilaya ya Wanging‟ombe?

Supplementary Question 2

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2002 mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro ilifanya uhakiki wa mipaka yake na ndipo hapo ilipochukua maeneo ya wananchi katika Vijiji vya Endamaga na Lostete na tangu mwaka huo hadi wa leo kuna migogoro ambayo haiishi ni lini maeneo hayo ya wananchi sasa yatarudishwa kwao?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, jambo moja ambalo napenda labda lieleweke vizuri hakuna mahali ambapo Serikali inatwaa ardhi bila kufuata utaratibu. Utaratibu wa Serikali kutwaa ardhi kwa ajili ya maslahi ya Taifa uko wazi, kwa upande wa hifadhi utaratibu huu ni shirikishi na unaanzia kwenye ngazi ya Vijiji vinavyohusika, Halmashauri zinazohusika, vikao vya Mkoa mpaka kufikia vikao vya maamuzi vya Kitaifa ndipo ardhi itatwaliwa kwa ajili ya matumizi kwa maslahi ya Taifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo pale ambapo kumetokea sababu yeyote ile ya kutokea kwa mgogoro labda kutoelewana au tafsiri tofauti ya sheria, tafsiri ya GN au matumizi yanayokiuka yale makubaliano ya awali. Hizo ni kasoro ambazo Serikali imekiri na ndiyo maana nimesema awali kwamba tunakwenda kupitia upya.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimeshajibu swali kama hili hapo nyuma na ninataka kusisitiza tena kwamba, tunakwenda kupitia mgogoro mmoja baada ya mwingine kuangalia ukweli wa mgogoro huo na ufumbuzi wake utapatikana kwa kushirikisha taasisi zote zitakazohusika ndani ya Serikali.

Name

Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa ardhi kati ya hifadhi ya Mpanga na wananchi wa Wilaya ya Wanging‟ombe?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, katika ziara yake Mkoani Simiyu Mheshimiwa Waziri Mkuu alitoa maelekezo, kuna mgogoro mkubwa wa hifadhi na wananchi wa Wilaya za Busega, Wilaya ya Bariadi, Wilaya ya Itilima na Wilaya ya Meatu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama Waziri Mkuu alitoa maelekezo na maagizo kwamba, Mawaziri wanne wakutane mara moja, leo ni miezi mitatu imepita hakuna kinachoendelea.
Je, Mheshimiwa Naibu Waziri lini sasa mtatii agizo la Waziri Mkuu la kukutana na kutatua migogoro hii?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Serikali kupitia Waziri Mkuu akiwa Mkoani Simiyu alitoa maelekezo. Maelekezo aliyoyatoa Mheshimiwa Waziri Mkuu akiwa Simiyu yamekwishaanza kutekelezwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, tayari tunayo taarifa iliyoandaliwa ya undani wa orodha ya migogoro yote inayohusika katika vijitabu ambavyo tayari vimeshagawiwa kwa Waheshimiwa Wabunge wote, nia ya Serikali imekwishaelezwa mara kadhaa hapa kwamba umefika wakati sasa baada ya kukusanya taarifa za awali tunakwenda kukusanya Wizara zote.
Mheshimiwa Naibu Spika, kila mmoja anafahamu, Waheshimiwa Wabunge wanafahamu na wananchi wote kwa ujumla wanafahamu kwamba sasa tuna vikao muhimu vya bajeti ambavyo vinakamilika mwisho wa mwezi wa sita, mara tu baada vikao vya bajeti tunakwenda kutekeleza ahadi hiyo ya Serikali ya kwenda kupitia upya migogoro yote hiyo kwa kushirikisha Wizara zote zinazohusika, lakini baada ya kukamilisha jukumu hili lililoko mbele yetu la Bajeti ya Taifa.