Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Wilaya ya Lushoto ni miongoni mwa Wilaya kubwa na Kongwe nchini ambapo ina takribani watu laki tatu lakini haina Mahakama ya Ardhi hivyo Wananchi hufuata huduma hiyo hadi Wilaya ya Korogwe licha ya kwamba majengo tunayo:- Je, ni lini Serikali itaanzisha Mahakama hiyo katika Wilaya ya Lushoto ili kuwapunguzia adha wananchi wake wanaofuata huduma hiyo Wilayani Korogwe?

Supplementary Question 1

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika ahsante, kwanza kabisa nimpongeze Waziri Lukuvi na timu yake kwa kunifungulia Baraza hili la Ardhi na hata watu wa Wilaya ya Lushoto sasa walimuombea dua maalum Lukuvi na timu yake kwamba kama kuna gagaziko basi liondolewe Mungu awaletee wepesi liweze kuondoka. Sasa naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza;
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kwamba Waziri amekuja kutufungulia Baraza la Ardhi lakini bado tuna migogoro mikubwa ya ardhi kati ya kijiji cha Nywelo na msitu wa Shume; kati ya Shamba la Mkonge Mnazi na vijiji vya Kwemng‟ongo na kijiji cha Kwemkwazu; kijiji cha Kwetango na kijiji cha Kweulasi; kijiji cha Kwemashai na kijiji cha Kilangwi.
Je, ni lini Serikali itakuja kutatua migogoro hiyo?
Swali la pili; Kwa kuwa, Wilaya ya Lushoto yenye Tarafa za Lushoto, Mlola, Mlalo, Mtae, Umba, Bumbuli, Soni na Mgwashi. Je, ni lini sasa Serikali itapima maeneo yao kwa kuwapatia hati za kimila ili wapate fursa za kukopa kwenye mabenki kuinua uchumi wao?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na hilo la mgogoro wa ardhi kati ya Mkonge Mnazi Estate na vijiji vya Kwemkwazu na Kwemhong‟o, Kwemlazi na Kwetango, Kwemashai na Kilangwi kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, unajua haya majina ya watani wangu kidogo ni magumu kutamka usipoangalia unaweza ukakosea, lakini nadhani nimeyataja vizuri. Kwa sababu tulikwishatoa maelekezo na kwenye kitabu cha migogoro, mgogoro huu umetajwa na hatua za kuanza kwenda kutatua au kutwaa tena lile eneo kuna hatua za kupitia ikiwemo na kutoa notes kwa mhusika, tayari Halmashauri wamekwishatoa notes kwa huyu Mmiliki wa Mnazi Estate, kwa hiyo mara muda wa notes zile siku 90 zitakapokuwa zimekwisha, basi hatua zingine zitachukuliwa ili kuweza kumaliza kabisa mgogoro huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, niwaombe sana ndugu zangu, watani zangu wa Kwemashai, Kilangwi, Kwaulasi, Kwetango na Kwemkwizu na Kwemng‟ongo kwamba notes zikikamilika hatua kamili zitachukuliwa kama atakuwa ameshindwa kujitetea kama tunavyotarajia.
Swali lake la pili ameulizia habari ya upimaji katika Tarafa za Lushoto, Mlalo, Mlola, Mtae, Umba, Bumbuli, Soni na Mgwashi. Naomba tu nimhakikishie kwamba iwapo tutapitisha pia bajeti ambayo ndiyo inakwenda kupitishwa leo, tayari kule tumetenga pesa kwa ajili ya upimaji, takribani bilioni 8.8 ambazo zinakwenda kununua vifaa na vifaa hivi vitagawiwa katika ofisi zetu za Kanda ili watu waweze kupima katika maeneo kwenye Kanda zao ikiwemo haya maeneo ya Lushoto, Mlalo, Mtae, Umba, Bumbuli na maeneo mengine kama nilivyotaja hizi Tarafa.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia kwenye suala la umilikishaji ardhi ambapo tunataka watu wote wawe na umiliki halali kwa maana ya kuwa na hati, tayari katika bajeti yetu tumetenga bilioni 13.8 ambazo zinakwenda kufanya kazi ya umilikishaji wa ardhi. Kwa hiyo haya yote yatakwenda kufanyika mara bajeti yetu itakapokuwa imepita, pia ni jukumu la Halmashauri zetu kuwa tayari katika suala hilo kwa sababu suala la upimaji pamoja na kwamba Wizara inafanya kazi hii, pia Halmashauri zinapaswa kujipanga vizuri kuweza kuona ni namna gani wanafanya matumizi bora ya ardhi katika baadhi ya vijiji vyao. Kwa sababu kiasi hiki bado kinaweza kisikidhi upimaji katika maeneo yote. Hivyo, kila Halmashauri inakumbushwa pia waone nao ni jukumu lao pamoja na kwamba Wizara itafanya kazi hiyo kupitia hizi pesa zilizotengwa, lakini bado Halmashauri wanao wajibu wa kupima maeneo yao.

Name

Stephen Hillary Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Wilaya ya Lushoto ni miongoni mwa Wilaya kubwa na Kongwe nchini ambapo ina takribani watu laki tatu lakini haina Mahakama ya Ardhi hivyo Wananchi hufuata huduma hiyo hadi Wilaya ya Korogwe licha ya kwamba majengo tunayo:- Je, ni lini Serikali itaanzisha Mahakama hiyo katika Wilaya ya Lushoto ili kuwapunguzia adha wananchi wake wanaofuata huduma hiyo Wilayani Korogwe?

Supplementary Question 2

MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Naibu Spika ahsante. Kwanza nikupongeze kwa kuzaliwa juzi Muhimbili na Mama Ulega, Mungu akubariki sana.
Swali langu ni kwamba, kwa kuwa baraza la ardhi la Wilaya ya Korogwe linafanya kazi katika mazingira magumu. Kuna kesi nyingi za kutoka mwaka 2009 mpaka leo hazijamalizika.
Je, ni lini Serikali itaongeza Watumishi pale ili kesi zile ambazo zimekaa kwa muda mrefu katika Baraza la Ardhi la Korogwe ziwe zimepata ufumbuzi wa haraka ili wananchi waone umuhimu wa Serikali yao?

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, hii ndiyo sababu tumetenganisha yale Mabaraza na kuunda Baraza jingine la Lushoto, kwa sababu kesi nyingi zilizokuwa zinakuja Korogwe ni za Lushoto na Wilaya nyingine. Kwa hiyo tumeunda Baraza la Lushoto, tutakwenda kuunda Baraza jingine la Kilindi. Kwa kufanya hivyo tutakuwa tumepunguza mzigo wa Korogwe na hivyo Baraza lile litakuwa limepunguziwa mzigo wa kuhudumia.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tukichukua hatua hizo Baraza lile litahudumia watu wachache zaidi na hasa wananchi wa Korogwe.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Wilaya ya Lushoto ni miongoni mwa Wilaya kubwa na Kongwe nchini ambapo ina takribani watu laki tatu lakini haina Mahakama ya Ardhi hivyo Wananchi hufuata huduma hiyo hadi Wilaya ya Korogwe licha ya kwamba majengo tunayo:- Je, ni lini Serikali itaanzisha Mahakama hiyo katika Wilaya ya Lushoto ili kuwapunguzia adha wananchi wake wanaofuata huduma hiyo Wilayani Korogwe?

Supplementary Question 3

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Waziri akiwa Mbulu aliwaahidi wananchi wa Mbulu kwamba Halmashauri ya Mbulu itafute jengo kwa ajili ya Mahakama. Namuomba Mheshimiwa Waziri katika mwaka huu wa fedha Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu itafanikiwa kwa kuwa ina kesi nyingi za ardhi ili Baraza hilo liweze kuzinduliwa na tayari Hamshauri imepata jingo.

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, rafiki yangu anajua majibu lakini anataka nirudie ili watu wake wasikie.
Mheshimiwa Naibu Spika, nilishakwenda, nimetangaza kwamba tutazindua Baraza la Mbulu mwaka huu, bahati mbaya sana majengo waliyotupa yalikuwa na „mushkeli‟ kidogo, Katibu Mkuu wangu ameandika barua kuomba majengo mengine, nafikiri yakirekebishwa hayo majengo, nimeshamuahidi na nimeshawaahidi watu wa Mbulu kwa sababu nimekwenda mwenyewe na Serikali hii haifanyi longo longo inafanya mambo ya uhakika, kwa hiyo tutazindua hilo Baraza mwaka huu la Mbulu.

Name

Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Wilaya ya Lushoto ni miongoni mwa Wilaya kubwa na Kongwe nchini ambapo ina takribani watu laki tatu lakini haina Mahakama ya Ardhi hivyo Wananchi hufuata huduma hiyo hadi Wilaya ya Korogwe licha ya kwamba majengo tunayo:- Je, ni lini Serikali itaanzisha Mahakama hiyo katika Wilaya ya Lushoto ili kuwapunguzia adha wananchi wake wanaofuata huduma hiyo Wilayani Korogwe?

Supplementary Question 4

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Naibu Spika nashukuru kwa kunipatia nafasi hii.
Kwa kuwa Wilaya ya Mkalama ni miongoni mwa Wilaya mpya ambazo hazina Mahakama ya Ardhi na huduma hiyo inapatikana Kiomboi.
Je, ni lini Wizara itaona umuhimu wa kutupatia Mahakama ya Ardhi na kuteua Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyoeleza katika majibu ya swali la msingi, lengo la Serikali ni kuhakikisha kwamba tunasogeza huduma hizi kwa wananchi kwa kufungua Mabaraza mengi kama ambavyo tumeyataja namna ambavyo nilisema kwamba tayari Mabaraza 47 Gazeti la Serikali lilikwisha yatangaza. Kwa hiyo kwenye suala la kufungua Baraza la Ardhi katika Wilaya ya Mkalama, naomba tu nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba pale ambapo tutakuwa tumehakikishiwa eneo kwa ajili ya Mahakama, ambapo tumeomba pia Wakurugenzi, Wakuu wa Wilaya katika yale maeneo yenye uhitaji mkubwa waweze kutupa maeneo hayo ili kuweza kufanya. Hivyo, tutaweza kuangalia tukiona kama eneo lipo zuri la kuweza kutosha basi tutaweza kufanya hivyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto kubwa tuliyonayo pia, hawa Wenyeviti wa Halmashauri bado ni wachache ukilinganisha na Mabaraza tunayotaka kufungua. Kwa hiyo bado tutakuwa na Wenyeviti ambao watakuwa wanahudumia pengine zaidi ya Baraza moja kulingana na uchache wao. Pale ambapo tutapata ajira mpya basi tutaweza kuwaeneza katika maeneo yao, kwa sasa naomba tu Waheshimiwa Wabunge tuvumiliane katika hilo kwa sababu lengo ni zuri, ni jema lakini bado uhitaji ni mkubwa kwa maana ya Wenyeviti wa kuweza kufanya kazi hiyo. Pale tutakapokuwa tumewapata basi tutafanya kazi hiyo.