Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Primary Question

MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:- Serikali imekuwa ikiahidi kusogeza huduma za afya karibu na wananchi na kuna umuhimu mkubwa wa kuwa na Zahanati kwa kila Kijiji na Kituo cha Afya kila Kata na Hospitali kwa kila Wilaya ili kuwaondolea kero wananchi wanaosafiri umbali mrefu kufuata huduma za afya na wengine kupoteza maisha wakiwa njiani:- Je, ni lini Serikali itatekeleza mpango huo wa kuwa na Zahanati kwa kila Kijiji, Kituo cha Afya kwa kila Kata na Hospitali kwa kila Wilaya?

Supplementary Question 1

MHE. FREDY A. MWAKIBETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa Sera ya Afya inasema, kila Kijiji kijenge Zahanati na kila Kata ijenge Kituo cha Afya; nakumbuka mwaka 2007 tulikuwa na program ya kujenga sekondari kwa kila Kata na kulikuwa na uhaba mkubwa sana wa watumishi; tulikuwa tunasema ni Vodacom ama Voda faster kwa sababu tu walikuwa wanamaliza Form Six na kwenda kufanya kazi. Je, Serikali imejipangaje ukizingatia hii ni afya kwa ajili ya watumishi watakaoajiriwa kwa vituo ama vijiji 12,000 na kitu?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Halmashauri ya Busokelo ni changa sana; tuna Hospitali moja tu, nayo hiyo Hospitali ni CDH kwa maana ya kwamba ni Council Designated Hospital; na tuna Kituo kimoja tu cha Afya. Je, Serikali ipo tayari sasa kushirikiana na wananchi nguvu kazi tunazozifanya ili iweze ku-upgrade Kituo cha Kambasegela, Kituo cha Afya Isange pamoja na Kanyerere?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli sera ya afya ni kwamba kila Kijiji kiwe na Zahanati na kila Kata iwe na Kituo cha Afya. Suala la watumishi ni kweli kuna changamoto, lakini tulivyokuwa katika bajeti yetu ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI), hali kadhalika wiki iliyopita tulikuwa na bajeti ya Wizara ya Afya; na Waziri wa Afya alisema wazi kuhusu mkakati wa kuajiri watumishi takriban 10,000 kwa kipindi hiki ili mradi kwenda kuziba zile gap.
Mheshimiwa Naibu Spika, hili liko katika utaratibu na naamini kwamba, wale watumishi watakapoajiriwa, nimwambie Mheshimiwa Atupele kwamba, tutalipa kipaumbele Jimbo lake ili mradi ile changamoto ambayo inalikabili sasa hivi ya upungufu wa watumishi tuweze kupunguza ile kasi yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo, tunahimiza hata vyuo vyetu vile vile kuongeza idadi ya watumishi, ili mwisho wa siku ile needs assessment tukiweza kuifanya, watu waweze kupatikana, basi katika soko, wawepo watu wa kutosha kuwapeleka katika hivi Vituo vya Afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la kushirikiana na watu wa Jimboni kwa Mheshimiwa Mbunge, kwanza namsifu sana, kwani ni miongoni wa Wabunge aliyenipa proposal mkononi, kwamba mimi nina proposal yangu ya Sekta ya Afya katika Jimbo langu. Kwa hiyo, nampongeza sana Mheshimiwa Mbunge.
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na hilo, naomba nikiri wazi kwamba Ofisi ya Rais, (TAMISEMI) itashirikiana naye, kuhakikisha kwamba changamoto zilizoko katika Jimbo hili, tuone tutazifanyaje kwa pamoja. Najua Jimbo hili hata Profesa alikuwa huko zamani. Kwa hiyo, tutashirikiana kwa pamoja kuona jinsi gani tutafanya ili mradi watu wa Jimboni kwake waweze kupata huduma ya afya hususan katika suala zima la kuongeza miundombinu.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:- Serikali imekuwa ikiahidi kusogeza huduma za afya karibu na wananchi na kuna umuhimu mkubwa wa kuwa na Zahanati kwa kila Kijiji na Kituo cha Afya kila Kata na Hospitali kwa kila Wilaya ili kuwaondolea kero wananchi wanaosafiri umbali mrefu kufuata huduma za afya na wengine kupoteza maisha wakiwa njiani:- Je, ni lini Serikali itatekeleza mpango huo wa kuwa na Zahanati kwa kila Kijiji, Kituo cha Afya kwa kila Kata na Hospitali kwa kila Wilaya?

Supplementary Question 2

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa jibu zuri. Swali langu ni kwamba, kuna maeneo ya Wilaya ambayo hata Hospitali za Wilaya hakuna. Je, Serikali inasemaje?
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri atakuwa tayari kufika maeneo kama ya Kilolo, kuja kuona anafanyaje ili kuhakikisha angalau vile Vituo vya Afya na Zahanati ambazo zimeanzishwa na wananchi, kuzipa msukumo ili angalau wapate matibabu na wao wajue kwamba ilani yao wanaitekeleza vizuri?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikiri kwamba niko tayari na bahati nzuri Mheshimiwa Mwamoto Jimboni kwake wanakuja hapa Ihula karibu kilometa 100. Kwa hiyo, wana changamoto kubwa na matatizo haya tunayafahamu vizuri sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikiri wazi, Mheshimiwa Mwamoto kwamba tutajitahidi kwa kadiri iwezekanavyo. Tutafika, tukiangalia tutapata jawabu kwa pamoja. Kama kuna Vituo vya Afya ambavyo vime-advance vizuri zaidi, tutaangalia jinsi gani tuvipe nguvu vile Vituo vya Afya, ili mradi wataalam kutoka Wizara ya Afya wakija kukagua, vituo vile viweze kupanda, basi viweze kutoa huduma kwa wananchi kwa hadhi ya Hospitali; kwa kadri itakavyoonekana kama mahitaji ya kuwahamisha kutoka katika Kituo cha Afya, kwenda Hospitali.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Mwamoto naomba nikiri wazi, nitafika Jimboni kwakE tutabadilishana mawazo na wananchi wakE, lengo ni kuboresha huduma ya afya katika nchi yetu.

Name

Saumu Heri Sakala

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:- Serikali imekuwa ikiahidi kusogeza huduma za afya karibu na wananchi na kuna umuhimu mkubwa wa kuwa na Zahanati kwa kila Kijiji na Kituo cha Afya kila Kata na Hospitali kwa kila Wilaya ili kuwaondolea kero wananchi wanaosafiri umbali mrefu kufuata huduma za afya na wengine kupoteza maisha wakiwa njiani:- Je, ni lini Serikali itatekeleza mpango huo wa kuwa na Zahanati kwa kila Kijiji, Kituo cha Afya kwa kila Kata na Hospitali kwa kila Wilaya?

Supplementary Question 3

MHE. SAUMU H. SAKALA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Matatizo ya ukosefu wa Zahanati na Vituo vya Afya yapo kila sehemu. Jimbo la Pangani ni moja kati ya Majimbo ambayo yana Kituo cha Afya kimoja tu, lakini kituo chenyewe pia hakina wahudumu wa kutosha, hakina vifaa vya kutosha. Je, Serikali ina mpango gani, kuhakikisha Kituo kile cha Afya kinaboreshwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kama sikosei amesema Pangani na bahati nzuri nilifika Pangani pale na kuona mahitaji, japokuwa sikwenda katika zoezi la kufanya assessment ya Sekta ya Afya. Bahati nzuri Mbunge wa Pangani ndugu yangu pale alikuwa kila siku ananikorofisha katika hili; na nikijua kwamba watu wa Pangani wana changamoto hii, kwa hiyo, naomba nikiri wazi kwamba, lengo letu kubwa ni kwamba, kwa watu wa Pangani siyo afya peke yake, Jimbo la Pangani ukiangalia lina changamoto kubwa hata ya miundombinu yake ya barabara.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kwa pamoja mimi nitakwenda na Waheshimiwa Wabunge huko, tutashirikiana kwa pamoja kubaini sasa nini tutafanya kwa pamoja? Kwa sababu jambo hili lazima tushirikiane kwa pamoja, lazima tubaini pamoja, halafu tuweke vipaumbele. Ndiyo maana jana nilimwita mtaalam wangu pale TAMISEMI aniandikie special proposal, lengo langu ni kwamba, mwakani inawezekana tukaja na sura nyingine hasa kutatua tatizo la afya. Nikawaambia waandike proposal maalum tutafanyaje kutatua tatizo la Zahanati na Vituo vya Afya na Hospitali za Wilaya, kama special project ya five years kuangalia tutafanya vipi, tuje na mtazamo mpya.
Mheshimiwa Naibu Spika, tukisema kwamba tunatenga Halmashauri peke yake, lakini centrally kama Ofisi ya Rais (TAMISEMI), tunafanyaje kuhakikisha ili tunakuwa na global program ya kupambana kwenye suala la afya katika Tanzania yetu hii. Kwa hiyo ,Mheshimiwa Mbunge nimelichukua hilo suala, tutapanga kwa pamoja kuona ni jinsi gani tutafanya ili mradi kuboresha maisha ya wananchi.

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. FREDY A. MWAKIBETE aliuliza:- Serikali imekuwa ikiahidi kusogeza huduma za afya karibu na wananchi na kuna umuhimu mkubwa wa kuwa na Zahanati kwa kila Kijiji na Kituo cha Afya kila Kata na Hospitali kwa kila Wilaya ili kuwaondolea kero wananchi wanaosafiri umbali mrefu kufuata huduma za afya na wengine kupoteza maisha wakiwa njiani:- Je, ni lini Serikali itatekeleza mpango huo wa kuwa na Zahanati kwa kila Kijiji, Kituo cha Afya kwa kila Kata na Hospitali kwa kila Wilaya?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona. Kwa kuwa Serikali ilianzisha mpango huu wa MMAM miaka kadhaa iliyopita na ukizingatia kwamba wanawake wajawazito na watoto ndio waathirika wakubwa; nataka kujua, nini mkakati wa Serikali katika kutoa vifaa tiba kwa akinamama wajawazito na watoto hususan katika suala zima la misoprostol wakati wa PPH? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nikifahamu Mheshimiwa Mary Mwanjelwa ni Daktari, kwa hiyo, najua anaguswa sana katika hilo. Vile vile mkakati uliopo, kwanza niseme lazima sisi Watanzania tujipe faraja wenyewe, kwa sababu jana kama wale watu walikuwa wanafuatilia katika mitandao ya kijamii, walimwona Rais Mstaafu Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akiwa katika harakati mbalimbali za watu wanaomtunuku kwamba ameshughulikia suala kubwa sana la vifo vya akinamama na watoto.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kama Watanzania lazima tujivunie kwa kazi kubwa aliyoifanya Rais wetu mstaafu. Harakati za sasa ni nini? Maana yake ni kujielekeza katika kila eneo katika kuboresha Sekta ya Afya. Ndiyo maana hapa nimezungumza mara kadhaa, kwamba sasa hivi tunakwenda kuhakikisha tunatekeleza mradi mkubwa na wenzetu wa kutoka Uholanzi, kuhakikisha mradi karibuni wa shilingi bilioni zipatazo 46. Katika hili maana yake nini? Tutakwenda kufanya mapinduzi makubwa katika Sekta ya Afya, hasa katika Hospitali yetu ya Kanda kuipatia vifaa tiba, lengo kubwa ni kupunguza vifo vya akinamama na watoto.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, mkakati wa Serikali ni huo kwa upana, kushirikisha the own source, kushirikisha income ambazo ziko ndani ya nchi, lakini halikadhalika fursa kutoka maeneo mbalimbali. Lengo kubwa ni kwamba Tanzania iwe ni icon kuhakikisha tunapambana na vifo vya akinamama na watoto katika Bara la Afrika.