Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Ujenzi wa Barabara ya Njombe – Ludewa – Itoni hadi Manda kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi kuweza kuuliza swali la nyongeza. Barabara ya Njombe – Itoni, watu bado hawajalipwa compensations nilipenda kujua lini watalipwa fidia wakazi hao? Lakini kibaya zaidi Mawengi – Mlangali tayari barabara imejengwa lakini kuna baadhi ya watu bado hawajalipwa fidia lini watalipwa? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili naomba kujua barabara ya Makete – Mbeya mkandarasi ameisha saini mkataba lakini mpaka hivi sasa tunavyozungumza hajafika site lini atafika site na ujenzi wa barabara hii ukaendelea? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Neema William Mgaya Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nataka nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi ambao ameuliza kwamba hawajalipwa fidia kwa eneo la Mawengi – Mlangali nataka nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imeisha andaa na kukamilisha Jedwali la malipo ya hao watu wenye fidia wa Mawengi pamoja na hawa wa Itoni – Lusitu na zoezi la kuwalipa nataka nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge litafanyika muda si mrefu.

Mheshimiwa Spika, nakuhusu suala la barabara ya Makete – Isyonje mkandarasi alishapatikana ameisha onyeshwa site lakini kinachosumbua kwasasa kuanza yupo kwenye mobilizations ni hali halisi ya hewa kwa maana ya mvua nyingi inayoendelea lakini tayari mkandarasi ameishapatikana na ameisha kabidhiwa site, ahsante.

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Ujenzi wa Barabara ya Njombe – Ludewa – Itoni hadi Manda kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa kuwa usanifu wa ujenzi wa barabara ya Kenyatta kutoka Mwanza Mjini kwenda Buhongwa – Usagara na Airport – Nyanguge zimeishakamilika ni lini ujenzi huu utaanza mara moja?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mabula Mbunge wa Nyamagana kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Serikali hazma yake ni kuijenga hii barabara na kuipanua lakini tayari tumeisha kamilisha usanifu na sasa hivi tunaendelea kutafuta fedha. Nimuombe Mheshimiwa Mbunge avute subira kwa sababu ndiyo tunaelekea kwenye bajeti tuone Serikali imepanga nini kwenye hiyo barabara, ahsante. (Makofi)

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Ujenzi wa Barabara ya Njombe – Ludewa – Itoni hadi Manda kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. DAVID M. KIHENZILE: Mheshimiwa Spika, ahsante, pamoja na kupitisha kwenye bajeti hii inayoendelea lakini bado barabara ya Mafinga – Mgololo na Mgololo – Mtwango hazijaanza kujengwa. Je, ni lini sasa Serikali itaanza ujenzi wa barabara hizi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa David Kihenzile Mbunge wa Mufindi Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii ilipangiwa bajeti. Nataka nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge pamoja na wananchi wa Jimbo la Mufindi Kusini kwamba tayari mkandarasi alishapatikana na kinachomsumbua pia kuanza hii kazi ni kwa sababu tu ya hali ya hewa na Mheshimiwa Mbunge nilishamuhakikishia yeye mwenyewe kwamba tayari tumeisha mpata mkandarasi na tayari ameishaandaa vifaa lakini hawezi kuanza kwa kweli ujenzi kwa mazingira ya Jimbo lake lina mvua nyingi sana lakini mara tu mvua itakapokatika mkandarasi ataanza kujenga kwa kiwango cha lami kwa bajeti ambayo tulikuwa tumeipanga kwa mwaka huu unaoendelea, ahsante sana.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Ujenzi wa Barabara ya Njombe – Ludewa – Itoni hadi Manda kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa spika, ahasante sana, kwa kuwa marudio ya upembuzi yakinifu wa barabara inayotoka Bulyanhulu kwenda Kahama umekamilika, vikao vya tathimini vimekamilika, vikao vya Kata zote vimekamilika, fedha zipo cash.

Ni lini sasa Wizara itaanza ujenzi wa barabara hiyo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Idd Kassim Mbunge wa Msalala kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara ya Bulyanhulu kwenda Kahama kama alivyosema nikweli usanifu ulishakamilika na fedha ipo sasa hivi kinachoandaliwa ni makabrasha tu kwa ajili ya kuanza kuitangaza hiyo barabara ili ianze kujengwa kwa kiwango cha lami ikiwa ni pamoja na kusaidiana na wenzetu wa Twiga kwa maana ya Barrick, ahsante.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Ujenzi wa Barabara ya Njombe – Ludewa – Itoni hadi Manda kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi niulize swali la nyongeza. Barabara kutoka Mji wa Namanyere – Bandari ya Kipili ni lini itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aida Khenani Mbunge wa Nkasi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja amekuwa anaulizia mara kwa mara na mwaka huu tuliipangia fedha na tulishawaambia mameneja wa Mkoa watangaze kwa gharama ile ambayo imepangiwa ili ianze kujengwa hata kama itajengwa kilomita moja, mbili lakini wazitangaze. Kwa hiyo, nataka nichukue nafasi hii kumkumbusha meneja wa Mkoa wa Rukwa aweze kufanya kama alivyopokea maagizo ya kuzitangaza hizi barabara, ahsante. (Makofi)

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Ujenzi wa Barabara ya Njombe – Ludewa – Itoni hadi Manda kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 6

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, barabara ya Handeni – Kiberashi – Singida ni barabara muhimu sana na barabara hii nashukuru mkandarasi alikwisha ripoti site lakini kinachoendelea sasahivi ni kwamba kama vile kazi aiendelei Je, tatizo liko wapi? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kigua Mbunge wa Kilindi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, bahati nzuri wiki iliyopita nimetembelea barabara hii kuangalia changamoto ni nini? Mkandarasi yupo site ameishaanza kazi anakamilisha majengo ya Muhandisi mshauri na kulikuwa na changamoto ndogo ambazo tumeisha zi-sort out na tayari nataka nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuanzia wiki inayoanza hii kasi itaongezeka kwa hiyo barabara inaendelea. Ahsante. (Makofi)

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Ujenzi wa Barabara ya Njombe – Ludewa – Itoni hadi Manda kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 7

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Spika, ahsante, barabara ya Dareda – Dongobesh – Usariva usanifu wa kina umeishafanyika na zabuni kutangazwa Je, ni lini barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sillo Mbunge wa Babati Vijijini kama Ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara imeishatangazwa na ipo kwenye hatua ya manunuzi kwa hiyo, sasa hivi kuna majadiliano yanayoendelea na mkandarasi ambazo ni taratibu za kawaida za manunuzi. Kwa hiyo, nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge barabara hii mara tutakapokamilisha hayo majadiliano mkandarasi tukishakubaliana atakabidhiwa site ili aendelee na ujenzi, ahsante.

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Ujenzi wa Barabara ya Njombe – Ludewa – Itoni hadi Manda kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 8

MHE. HASSAN Z. KUNGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itapeleka fedha za kujenga barabara kwa kiwango cha lami katika Wilaya ya Tunduru ambapo taasisi zote za Serikali zipo katika barabara hiyo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kungu Mbunge wa Tunduru Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ni barabara za TANROADS zinapita tuna mpango wa kuhakikisha katika kila Miji hasa ya Makao Makuu ya Wilaya, ambapo barabara zetu zinapita basi zijengwe kwa kiwango cha lami. Nimuombe Mheshimiwa Mbunge mara baada ya hapa tuweze kuonana kama barabara zetu zipo zinapita katikati ya taasisi hizo ambazo amezisema ili tuweze kuona utaratibu wa namna ya kuzijenga kwa kiwango cha lami katika hayo maeneo aliyoyataja, ahsante.

Name

Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Ujenzi wa Barabara ya Njombe – Ludewa – Itoni hadi Manda kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 9

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwakunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Barabara ya Kibiti – Dimani – Mloka iko ndani ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM); je, lini Serikali wataanza mchakato wa kuitengeneza barabara hiyo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Twaha Mpenbenwe Mbunge wa Kibiti kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama alivyosema ipo kwenye Ilani na Serikali kwakweli inaendelea kutafuta fedha kwa barabara hii ili iweze kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Ujenzi wa Barabara ya Njombe – Ludewa – Itoni hadi Manda kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 10

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwetu tuna barabara ya Mtwara – Pachani – Mkongo – Lusewa – Magazini – Nalasi na Mheshimiwa Naibu Waziri ulikuja kuitembelea na ina hali mbaya sana mpaka sasa hivi na uliwahaidi wazee wale kwamba itatengenezwa kwa kiwango cha lami Je, unawaeleza nini leo Mheshimiwa Naibu Waziri? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Vita Kawawa Mbunge wa Namtumbo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tulitembelea hii barabara ndefu yenye kilomita 300 tumemuagiza meneja wa Mkoa wa Ruvuma kwanza kuhakikisha anaainisha maeneo yote korofi ili yaweze kupata bajeti wakati Serikali inaendelea kutafuta fedha kuijenga hii barabara kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari tumeishaongea na meneja wa Mkoa aangalie maeneo yote ambayo ni korofi ambayo tunaweza tukayadhibiti kwa muda wakati tunatafuta fedha ya kuijenga barabara yote kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Ujenzi wa Barabara ya Njombe – Ludewa – Itoni hadi Manda kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 11

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, barabara ya Chekeleni – Kahe – TPC – na Mabogini iko kwenye Ilani awamu hii na awamu iliyopita na pia ni ahadi ya Viongozi Wakuu wa Serikali. Nataka kujua ni lini Serikali itaanza sasa kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami kama ilivyoahidiwa? Natumaini hatasema kwamba ni mpaka hela ipatikane.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kimei Mbunge wa Vunjo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama alivyosema ni ahadi ya viongozi lakini pia iko kwenye ilani naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kujenga barabara zote ambazo imeziaidi kuzijenga kwa kiwango cha lami ikiwa ni pamoja na barabara ambayo Mheshimiwa Mbunge wa Vunjo ameitaja.

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Ujenzi wa Barabara ya Njombe – Ludewa – Itoni hadi Manda kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 12

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi barabara ya Utegi – Shilati – Kilongwe yenye kilomita 56 upembuzi yakinifu umekwisha kamilika Mheshimiwa Waziri ni lini sasa barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jafari Chege Mbunge wa Rorya kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja nikweli ipo kwenye Ilani na imeahidiwa kujengwa kwa kiwango cha lami. Naomba nimuombe Mheshimiwa Mbunge asubiri bajeti hii tutakayosoma tutakuwa tumependekeza nini kuhusu barabara hii ya kutoka Mika – Utegi – Ruari hadi Kirongwe, ahsante.

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Ujenzi wa Barabara ya Njombe – Ludewa – Itoni hadi Manda kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 13

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona, Barabara ya Nyoni – Mlima mkali wa Mawono – Mapela – Maguu kilomita 25 ipo kwenye Ilani ni lini sasa barabara hii itaanza ujenzi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kapinga Mbunge wa Mbinga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja ipo kwenye miinuko na tunachofanya kwa sasa nikuhakikisha kwamba inapitika kwa muda wote wakati tukifanya hivyo Serikali inaendelea kutafuta fedha ili kuweza kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante.