Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Michael Mwita Kembaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Mjini

Primary Question

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza: - Je, ni lini chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Wilaya ya Tarime TC kitaanza kufanya kazi?

Supplementary Question 1

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali ningependa kujua maana katika Hospitali yetu Kuu ya Wilaya Bomani, jokofu lake limekuwa likiharibika mara kwa mara.

Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha kwamba Jokofu lile linafanya kazi ili watu wapate huduma ambayo inastahili?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwita Kembaki Michael, Mbunge wa Jimbo la Tarime Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli jokofu la Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Tarime ni la siku nyingi ni chakavu na linaleta usumbufu wa kuharibika mara kwa mara, lakini Serikali imeshatenga fedha katika mwaka wa fedha ujao 2023/2024 kwa ajili ya kununua jokofu lingine kwa ajili ya Hospitali ya Mji wa Tarime. Ahsante.

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza: - Je, ni lini chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Wilaya ya Tarime TC kitaanza kufanya kazi?

Supplementary Question 2

MHE. JAFARI W CHEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Vituo vya Afya vitatu kwa maana ya Kinesi, Changunge na Kituo cha Nyamagaro havina chumba cha kuhifadhia maiti. Nataka nijue mpango wa Serikali wa ujenzi wa vyumba hivi kwa ajili ya kunusuru na kusaidia wananchi maeneo haya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jafari Wambura Chege, Mbunge wa Jimbo la Rorya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba vituo hivi ambavyo vingine ni vipya havina majengo ya kuhifadhia maiti, lakini mpango wa Serikali ni kuendelea kujenga vituo hivi kwa awamu. Tumejenga majengo awamu ya kwanza, tumejenga awamu ya pili na sasa tunakwenda awamu ya tatu kwa ajili ya kujenga majengo mengine yakiwemo majengo haya ya kuhifadhia miili. Ahsante.