Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: - Je, Serikali ipo tayari kufanya mapitio ya tathmini kwa wananchi wanaopisha mradi wa kuboresha Bonde la Mto Msimbazi?

Supplementary Question 1

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Spika, kwanza nashukuru kwa majibu ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa mradi huu unapita katika Kata za Kigogo, Mzimuni, Magomeni, na Hananasifu. Je, Serikali sasa iko tayari kutoa Tarehe au muda lini mapitio hayo yataenda kufanyika ili wananchi wa maeneo yale waweze kufahamu?

Swali langu la pili, ningependa kama ikiwezekana Serikali itoe tangazo mapema ili wananchi wale wote waweze kuwepo wakati tathmini hizo zikifanyika. Ahsante sana.

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Tarimba Abbas kwa maswali yake mawili.

Mheshimiwa Spika, naomba tu nimfahamishe kwamba katika mradi ambao unaendelea sasa pamoja na Kata alizozitaja mpaka sasa wananchi waliofikiwa ni 2,217 kati ya 2,432 ambao watafikiwa. Katika hao ambao wamefikiwa sasa katika ule mradi, asilimia 92 ni wananchi 2,057 wameshakubali wamefanyiwa uhakiki na kati yao ni 160 tu ambao hawajafikiwa. Kwa hiyo, kaya ambazo hazijafikiwa ni
215 na nadhani zipo katika yale maeneo ambayo umeyasema, hivyo wakifikiwa nadhani nao pia watapata huduma ile ile ambayo wamepatiwa wengine.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili kuhusu kutoa tangazo, inawezekana likatoka, lakini huwezi ukalitoa kwa sasa kwa sababu procedure hiyo bado inaendelea. Kampuni iliyopewa kufanya kazi hiyo bado ipo uwandani inafanya kazi. Kwa hiyo, pale itakapokuwa imefikia kwenye hatua ambayo ni ya mwisho, kwa sababu maeneo yanayotwaliwa yote yanafahamika, basi wataambiwa wananchi, lakini kwa sasa huwezi kutoa tangazo kwa sababu bado pia tupo kwenye utaratibu wa kukamilisha.