Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

George Natany Malima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaweka taa za barabarani katika Mji wa Mpwapwa ili kuongeza usalama nyakati za usiku?

Supplementary Question 1

MHE. GEORGE N. MALIMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza: Katika Mji wa Mpwapwa kuna eneo dogo sana ambalo liliwekwa taa zamani, lakini taa hizi muda mwingi hazifanyi kazi: Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati taa hizi ili ziweze kufanya kazi angalau katika eneo hilo dogo?

Mheshimiwa Spika, swali la pili: Mheshimiwa Rais amejenga daraja kubwa la TANESCO katika Mji wa Mpwapwa; daraja hili limejengwa katika eneo lenye miti mingi, kwa hiyo, husababisha giza nene wakati wa usiku. Mazingira hayo yanahatarisha usalama wa watumiaji. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri atakubaliana nami kwamba jambo la kuweka taa katika eneo hili ni la dharura lisilohitaji kusubiri taratibu za manunuzi? Kama jibu ni ndiyo; ni lini wataweka taa katika daraja hilo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa George Natany Malima, Mbunge wa Mpwapwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, taa tunazoweka ni kwenye Barabara ambazo ni za TANROADS na kilometa 2.5 naamini tutakuwa tumepita pia kwenye maeneo hayo anayoyasema na hata tutayawekea lami na kuweka taa. Kwa hiyo, nina hakika kwa kilometa mbili na nusu tutakuwa tumekamilisha taa katika Mji wa Mpwapwa. Kama kutakuwa na changamoto ya hizo taa, nitaomba Mheshimiwa Mbunge tuweze kuonana ili tulichukue kama ni jambo la namna yake ili tuweze kuangalia kama hizo taa zinarekebishika ama tutaweka taa nyingine.

Mheshimiwa Spika, kwenye swali lake la pili, kama nimemsikia kuhusu daraja ambalo liko katika Mji wa Mpwapwa; limeshakamilika na tunatambua kwamba kuna mmomonyoko mkubwa ambao unaendelea. Sisi kama TANROADS kwa maana ya ujenzi, linahusisha watu wengi; watu wa mazingira, watu wa bonde la maji, na pia TAMISEMI kwa maana ya kwamba ni wadau. Sisi tunaweza tukajenga lakini kwa kushirikiana na hao wadau, na Mheshimiwa Mbunge tulishaongea naye kwamba Serikali imelichukua kwa wadau wote, tuone namna ya kuweza kudhibiti mmomonyoko ambao unaendelea ambao pia utahatarisha hilo daraja.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba liko, linafanyiwa kazi na Wizara zinazohusika kuweza kulijenga hilo daraja, kwa maana ya kurekebisha hizo kingo za daraja la huo Mto Mpwapwa.