Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza: - Je, ni lini wananchi wa Kata ya Sitalike waliopisha ujenzi wa barabara ya Sitalike hadi Mpanda Hotel watalipwa fidia?

Supplementary Question 1

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunpa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa wananchi hawa wamesubiri muda mrefu, wamepisha barabara hii takribani sasa tokea 2012 ina maana sasa hivi takribani miaka 11 mpaka leo hawajapata fidia zao na kuna wengine wamefariki. Je, kupitia hii kero Waziri yuko tayari kuja kuzungumza na wananchi wa Kata ya Sitalike?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa hii imekwisha kuwa shida. Je, Serikali inajipangaje sasa kupitia tatizo hili la fidia kuhakikisha kabla hawajawatoa watu wahakikishe wamewalipa kwanza ili isiwe kero kupitia Serikali?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Anna Richard Lupembe, Mbunge wa Nsimbo yote kwa pamoja kwa ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala hili la fidia hasa kwa mita 7.5 limekuwa linajitokeza mara kwa mara, na mimi napenda tu nitumie nafasi hii kuwajulisha Waheshimiwa Wabunge kwamba hii ni Sheria ya kuongeza upana wa barabara kutoka Mita 45 kwenda mita 60 ya mwaka 2007. Kufanyika huku kulikuwa ni kuhakikisha kwamba tunakuwa na hifadhi kubwa ya barabara ili tunapotaka kufanya shughuli zozote ikiwa ni pamoja na kuongeza upana wa barabara ama kupitisha mifumo mingine yote iwe ya maji, ya mikongo ya mawasiliano tuweze kuwa na hifadhi kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ilikuwa ni kuhakikisha kwamba tunakuwa na hifadhi kubwa ya barabara ili tunapotaka kufanya shughuli zozote, ikiwa ni pamoja na kuongeza upanda wa barabara, ama kupitisha mifumo mingine yoyote iwe ya maji, na mikongo ya mawasiliano, tuweze kuwa na hifadhi kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali tutakuja na taarifa sahihi ya utaratibu ambao tutaufanya kwa sababu ni nchi nzima ambapo tumeongeza huo upana wa barabara, namna bora na sahihi ya kuweza kuchukua hayo maeneo na kuwalipa fidia, ama kama kutakuwa na maelekezo mengine ambayo Serikali itakuja kuyatoa. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Anna Lupembe pamoja na Wabunge wengine wote ambao wana changamoto hizo kwenye majimbo yao kwamba, Serikali itakuja na utaratibu mzuri wa namna bora ya kufidia wananchi ambao barabara imewafuata, ahsante.

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza: - Je, ni lini wananchi wa Kata ya Sitalike waliopisha ujenzi wa barabara ya Sitalike hadi Mpanda Hotel watalipwa fidia?

Supplementary Question 2

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Je, ni lini Serikali italipa fidia kwa wananchi waliopisha barabara ya Bypass ambayo ni mpya ya Uyole mpaka Songwe?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara aliyotaja Mheshimiwa Njeza Mbunge wa Mbeya Vijijini, ni mpya, inajengwa. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba taratibu zinaendelea na barabara ambazo tunazijenga wananchi watafanyiwa tathmini na wakati tunaanza ama kabla hatujaanza, wananchi hawa watalipwa fidia zao, ahsante.

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza: - Je, ni lini wananchi wa Kata ya Sitalike waliopisha ujenzi wa barabara ya Sitalike hadi Mpanda Hotel watalipwa fidia?

Supplementary Question 3

MHE. REGINA N. QWARAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi wa Ngoni, Himiti, Singe hadi Komoto ambao wamepisha ujenzi wa Bypass katika Mji wa Babati? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Regina, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema katika majibu mengine, ni kwamba wananchi hawa wameshafanyiwa tathmini na Serikali inaendelea kutafuta fedha ili kuweza kuwalipa fidia yao wananchi ambao wamepisha mradi huu wa barabara wa Bypass katika Mji wa Babati, ahsante.

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza: - Je, ni lini wananchi wa Kata ya Sitalike waliopisha ujenzi wa barabara ya Sitalike hadi Mpanda Hotel watalipwa fidia?

Supplementary Question 4

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa kuwa mradi wa bypass unaanzia Kata ya Kisaki - Nyamikumbi - Unyambwa mpaka Utipa umeshafanyiwa upembuzi yakinifu: Ni lini ujenzi huu utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Serikali ilishafanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa Bypass ya Singida. Kitakachofanyika sasa ni kufanya mapitio upya na kupata gharama ya sasa ya ujenzi. Kwa hiyo, barabara hii baada ya fedha kupatikana tutaanza kuijenga ili kupunguza msongamano katika Mji wa Singida, ahsante. (Makofi)

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza: - Je, ni lini wananchi wa Kata ya Sitalike waliopisha ujenzi wa barabara ya Sitalike hadi Mpanda Hotel watalipwa fidia?

Supplementary Question 5

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Serikali imekuwa na changamoto kubwa sana ya ulipaji wa fidia kwa wananchi wanaopisha miradi mbalimbali ya maendeleo. Je, Serikali haioni sasa kuna umuhimu wa kufanya tathmini baada ya kuwa mmepata fedha ili kuondoa usumbufu kwa wananchi ambao wanapisha miradi kwa hiari?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hawa Mwaifunga Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapofanya miradi ya barabara, fidia inakuwa ni sehemu ya gharama ya ujenzi wa hiyo barabara. Kwa hiyo, tunapokuwa tunafanya ujenzi ni pamoja na fidia. Kwa hiyo, tunaposema gharama ya barabara hii, ni pamoja na fidia ya wananchi ambao wanapisha hiyo miradi, ahsante.

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza: - Je, ni lini wananchi wa Kata ya Sitalike waliopisha ujenzi wa barabara ya Sitalike hadi Mpanda Hotel watalipwa fidia?

Supplementary Question 6

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa fursa ya swali dogo la nyongeza. Kutokana na mvua kubwa inayonyesha Bonde la Ziwa Rukwa, madaraja takribani sita yamesombwa na mafuriko: Je, ni lini kauli ya Serikali juu ya kurudisha mawasiliano kwa dharura katika eneo hili la Bonde la Ziwa Rukwa ambalo na Mheshimiwa Naibu Waziri unalijua fika?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Sangu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba katika kipindi cha mvua, barabara nyingi huharibika na madaraja mengi kusombwa likiwemo daraja la Mheshimiwa Sangu ambalo ni eneo la bondeni. Naomba tu nichukue nafasi hii kumjulisha ama kumpa maelekezo Meneja wa TANROADS Mkoa wa Rukwa ahakikishe kwamba anapeleka timu ya wataalam kuanza kufanya tathmini na ikiwezekana kurudisha mawasiliano ya muda na pia aweze kuleta taarifa Makao Makuu kuomba uwezesho wa fedha ili kurejesha mawasiliano haya ya kudumu, ahsante.