Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA K.n.y. MHE. SHANIF J. MANSOOR aliuliza: - Je, ni lini Chuo cha VETA Ngudu Kwimba kitakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. JUSTINE L. NYAMOGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, Ujenzi wa chuo hiki pamoja na kwamba umefikia hatua hizo lakini kuna shida ya huduma ya maji na gharama yake ni shilingi milioni 90. Je, ni lini Wizara itapeleka fedha milioni 90 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa chuo hicho na ili huduma ziweze kutolewa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; tunaishukuru Serikali kwa kutoa fedha kwa ajili ya kujenga chuo katika Wilaya ya Kilolo. Je, ni lini ujenzi huo utaanza katika Wilaya ya Kilolo ili wananchi waweze kunufaika na huduma za chuo cha VETA.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Justin Nyamoga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza anataka kufahamu swala la maji katika Chuo cha Ngudu. Ni kweli tumepeleka fedha kwa ajili ya ukamilishaji kwa maana ya majengo lakini kwa maana ya uunganishwaji wa maji bajeti ile iliyokuja baada ya kuifanyia tathmini tuliona kwamba iko kubwa sana, ilikuwa inflated kwa kiasi kikubwa. Kwa hiyo, tumeifanyia maboresho na sasa fedha zimekuja kama milioni 57 hivi kipindi kifupi kijacho tutapeleka fedha hiyo kwa ajili ya ukatishaji wa maji katika eneo lile.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini katika swali lake la pili anataka kufahamu ujenzi wa chuo cha VETA Kilolo. Nimuondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge tayari timu ya wataalam imeshafika Kilolo na tumeshafanya topographical survey, geotechnical survey pamoja na environmental and social impact assessment na baada sasa ya matokeo haya ya vipimo hivi tutakwenda kuanza ujenzi mara moja, nakushukuru sana.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA K.n.y. MHE. SHANIF J. MANSOOR aliuliza: - Je, ni lini Chuo cha VETA Ngudu Kwimba kitakamilika?

Supplementary Question 2

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Waziri, Wilaya ya Busekelo tunaomba sana Serikali itujengee chuo cha VETA na Mheshimiwa Mbunge yuko tayari kusaidia kupata eneo kwa ajili ya kujenga chuo hiko. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Sophia Mwakagenda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa vyuo vya VETA unajengwa katika kila wilaya na wilaya zote zilizobaki ambazo hazina vyuo vya VETA katika kipindi hiki cha 2023/2024, tunakwenda kujenga katika wilaya zote zilizobaki. Kwa hiyo, kama Busekelo ni wilaya ambayo haikuwa na chuo cha VETA nimuondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge tunakwenda kufanya kazi hiyo haraka iwezekanavyo. (Makofi)

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA K.n.y. MHE. SHANIF J. MANSOOR aliuliza: - Je, ni lini Chuo cha VETA Ngudu Kwimba kitakamilika?

Supplementary Question 3

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Je, ni lini Chuo cha VETA kilichojengwa Wilayani Lushoto Eneo la Mlola kitaanza udahili?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shekilindi, Mbunge wa Lushoto, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa Chuo cha VETA Lushoto ni miongoni mwa vile vyuo 25 vya awamu ya kwanza, ambapo ujenzi wake umeshakamilika kwa asilimia 100. Nimuondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kama nilivyokwishajibu kwenye majibu ya swali la msingi vyuo hivi vyote 25 vya awamu ya kwanza, tunapeleka samani, vifaa vya kufundishia pamoja na kuandaa rasilimali watu. Ni matumaini yetu katika mwaka wa fedha 2023/2024 vyuo hivi vyote 25 vya wilaya na vile vinne vya mikoa vinaenda kuanza kutoa mafunzo rasmi.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA K.n.y. MHE. SHANIF J. MANSOOR aliuliza: - Je, ni lini Chuo cha VETA Ngudu Kwimba kitakamilika?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Kigamboni katika Hotuba ya Bajeti ya Mwaka jana ilitajwa kwamba ni moja ya wilaya ambayo mtakwenda kujenga chuo cha VETA na imebakia miwezi miwili. Ni lini sasa ujenzi ule utaanza ili wananchi wa kigamboni waweze kunufaika na chuo hicho?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Ndugulile, Mbunge wa Kigamboni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Kigamboni ni miongoni mwa wilaya 64 zilizobaki katika ujenzi wa vyuo 64 zilizobaki. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba geotechnical survey, topographical survey, environmental impact assessment tayari tumeshafanya. Tunasubiri majibu kwa maana ya results ya tafiti hizo na baada tu ya majibu hayo, tunaenda kuanza ujenzi katika mwaka huu wa fedha, nimuondoe wasiwasi kazi hiyo inakwenda kufanyika.

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA K.n.y. MHE. SHANIF J. MANSOOR aliuliza: - Je, ni lini Chuo cha VETA Ngudu Kwimba kitakamilika?

Supplementary Question 5

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naipongeza Serikali kwa kujenga vyuo vya VETA lakini kwenye vyuo hivi vingi vya VETA vilivyopita, masomo yanayotolewa mengi hayana soko kubwa kwenye ajira ya sasa lakini kuna masoma kama ufundi bomba, ufundi umeme wa magari, umeme wa majumbani unakuta kozi nyingi hazipo kwenye vyuo vya VETA mathalani Makete. Ni lini Serikali itaanza kuongeza masomo hayo ambayo yanaajira nyingi kwa vijana wetu ili waweze kupata kusoma?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Sanga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimejibu katika swali nadhani namba 96 la kuhusiana na suala la upitiaji wa mitaala. Tumeanza upitiaji wa mitaala katika elimu yetu ya msingi lakini tunafanya mapitio ya mitaala katika elimu ya sekondari, vyuo vya ualimu, vyuo vikuu pamoja na vyuo vya VETA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mapitio hayo ya mitaala vile vile katika maeneo haya ya vyuo vya VETA tunakwenda kuongeza idadi ya masomo lakini vile vile kufanya review ya hata hayo masomo yote tunayoyatoa kuhakikisha kwamba tunakwenda kweli kujibu changamoto za wananchi zile ambazo katika maeneo yao ambao wanahitaji.