Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Mbuyu wa Mjerumani hadi Mbulu?

Supplementary Question 1

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili. Swali la kwanza; je, Serikali iko tayari sasa kuongeza fedha 2023/2024, walau kuanza kilometa 10 za barabara hiyo?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kilometa nane kwa ajili ya ujenzi wa Barabara ya Dareda – Dongobesh imetangaza zabuni mwezi Machi, sasa ni lini kazi hii itaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Daniel Baran Sillo, Mbunge wa Babati Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Barabara hii ya kutoka Mbuyu wa Mjerumani – Mbulu tumeshaanza kuijenga kwa kiwango cha lami kwenye maeneo ya escarpment na tutaendelea. Tumeshajenga kilometa nne lakini pia tumetenga fedha ili kuendelea kujenga eneo hilo la muinuko mkali kwa kiwango cha lami wakati Serikali sasa inaendelea kutafuta fedha kuijenga barabara yote ya Mbuyu wa Mjerumani – Mbulu.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Barabara ya Dareda – Dongobesh, tulitangaza tenda wakandarasi wakakosa sifa. Tumetangaza tena na sasa hivi tupo kwenye evaluation. Ahsante.

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Mbuyu wa Mjerumani hadi Mbulu?

Supplementary Question 2

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Barabara ya kutoka Iringa Mjini kwenda katika Hifadhi ya Taifa Ruaha ambayo imetengewa fedha miaka mingi lakini hazitoshi na hazitoki na upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ulishafanyika; je, ni lini sasa hii barabara itakwenda kujengwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Grace Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Barabara ya Iringa – Ruaha (Iringa Msembe), kilometa 104, inafadhiliwa na World Bank na hivi tunavyoongea iko kwenye hatua ya manunuzi kuijenga barabara yote kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Mbuyu wa Mjerumani hadi Mbulu?

Supplementary Question 3

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Je, ni lini eneo la Nyangoye katika Barabara ya Uganda – Bukoba Mjini litarekebishwa, ahadi ya Mheshimiwa Makamu wa Rais, ili kuondoa ajali zinazotokea mara kwa mara? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Oliver Semuguruka, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Kagera, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, lilikuwa agizo la Makamu wa Rais na sasa hivi kinachoendelea ni kufanya usanifu wa namna ya kuijenga barabara hiyo. Ahsante.