Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza: - Je, ni Watanzania wangapi wamejitokeza na kupata fursa ya mafunzo maalum ya ujuzi yaliyotangazwa kupitia VETA kote nchini?

Supplementary Question 1

MHE. BONNAH L. KAMOLI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nilikuwa na maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; je, Serikali imejipangaje kutokana na miradi mikubwa ambayo inaendelea hapa kama Bwawa la Mwalimu Nyerere lakini pia na Miradi ya SGR; ili kuhakikisha vijana wetu wa Tanzania wanaenda kusimamia hii miradi pindi itakapokamilika? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili: Ili kuendana na Uchumi wa Bluu; je, Serikali imejipangaje kufundisha vijana wetu kwenye mambo ya uvuvi? (Makofi)

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Bonnah Ladislaus Kamoli, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tayari Serikali ilimeshaliona hilo na kwa maagizo ya Mheshimiwa Rais na maelekezo mahususi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, ile miradi wakati inaanza tayari tulishatambua vijana ambao walipaswa kuchukuliwa na kwenda kupata mafunzo zaidi. Katika Mradi wa Reli ya Kisasa, vijana 3,526 tayari walishaajiriwa. Kati ya hao, tumewatambua vijana 1,916 ambao wataenda kwenye vyuo vyetu mbalimbali na ndio watakaofanya succession plan kwenye maeneo hayo kwa ajili ya masuala ya teknolojia na ufundi.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, likiwa sambamba na Bwawa la Mwalimu Nyerere ambapo ni zaidi ya vijana wa Kitanzania 10,228 ambao tumewaajiri, kati hao 146 tumeshawatambua na tutawasajili kuweza kuwajazia na kuwajengea ujuzi na skills za kuweza kuendelea hata baada ya watalamu wa kigeni wale kuondoka.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala hili katika succession plan; sheria yetu inaendelea kusimamia seccession plan ya local content ili ilete faida zaidi kwa Watanzania hasa katika kununua bidhaa za ndani na pia kupata wafanyakazi wa Kitanzania kwenye miradi hii ya maendeleo na kuweza kujeza kujenga uchumi wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho kuhusiana na Blue Economy, tayari kupitia Wizara yetu ya Uvuvi, wapo vijana ambao wanapata mafunzo na ufugaji wa samaki umeshaanza, ufugaji wa vizimba kule Mkoa wa Mwanza, pia tunafanya kwenye maeneo ya bahari ikiwa ni pamoja na Tanzania Zanzibar, tayari programu hii ipo, imeshaanza kufanya kazi na Mheshimiwa Rais ameendelea kutoa fedha kwa ajili ya kuwawezesha vijana hawa kwa kujiandaa na uchumi wa kisasa, ahsante. (Makofi)