Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaondoa makato yaliyopo kwenye Vyama vya Msingi kwa Wakulima wa Kahawa Mbozi?

Supplementary Question 1

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza; tatizo ni muda, mwezi Juni na mwezi Mei mwishoni wakulima wa kahawa wanaanza kuvuna kahawa yao kupeleka kwenye hivyo Vyama vya Msingi, sasa Waziri anaposema mwezi ujao, kwa nini hili suala lisifanyike mapema kabla ya msimu wa kuuza haujaanza ili hayo makato yaondolewe na wakulima wapate chao?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; niipongeze Serikali kwa uamuzi wa kuwafutia leseni mawakala wa mbolea 700. Kwa kweli hii ni hatua nzuri na naomba wasirudi nyuma wakaze buti, hatuwezi kutishwa na watu wasiokuwa waaminifu, ahsante. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri wakati naingia hapa Bungeni taarifa imekwishafika Wizarani, kwa hivyo tutaanza kulifanyia kazi mwezi huu ili kuuwahi msimu.

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaondoa makato yaliyopo kwenye Vyama vya Msingi kwa Wakulima wa Kahawa Mbozi?

Supplementary Question 2

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Naomba sasa kuiuliza Serikali swali la nyongeza. Je, Wizara ya Kilimo ina mkakati gani wa kuhakikisha wakulima wa kahawa wa Wilaya ya Ngara wanaendelea kuuza kahawa yao kwa bei nzuri kama ilivyokuwa kwenye msimu uliopita? Ahsante sana.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze Mbunge kwa kazi nzuri ambayo anaifanya kwenye zao hili la kahawa, nataka tu nimhakikishie kwamba utaratibu ambao tulioanza nao ulimpa mkulima bei nzuri, tutaendelea nao. Vilevile tutahakikisha kwamba tunamsaidia mkulima kupata masoko ya uhakika na azalishe kahawa yenye ubora ili iweze kumpatia bei nzuri sokoni. Kwa hiyo nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba wakulima wa kahawa Mkoa wa Kagera na maeneo mengine wataendelea kunufaika na utaratibu ambao tumeuweka hivi sasa.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaondoa makato yaliyopo kwenye Vyama vya Msingi kwa Wakulima wa Kahawa Mbozi?

Supplementary Question 3

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Kama ilivyo kwa zao la kahawa kuwa na tozo nyingi; je, ni lini, Serikali itafanya marejeo tena kwa zao la parachichi hasa katika Mikoa ya Njombe na Wilaya ya Rungwe?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kwanza ambalo tumelifanya kwenye parachichi ni kukaa na wadau na kutengeneza mwongozo wa pamoja wa zao ambao pia ndani yake tutajadili makato yote na namna ya uendeshaji wa zao hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba na lenyewe pia tumelipa kipaumbele kwa sababu parachichi ndio dhahabu yetu ya kijani, kwa hiyo tunaiangalia katika jicho la kipekee sana.

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaondoa makato yaliyopo kwenye Vyama vya Msingi kwa Wakulima wa Kahawa Mbozi?

Supplementary Question 4

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Wakulima wa tumbaku wamekatwa makato makubwa sana ya upandaji wa miche ya miti ambapo ni zaidi ya shilingi 813 kwa kila mche mmoja.

Sasa kwa nini, Serikali isiondoe kabisa makato haya kwa wakulima wa tumbaku ili waweze kupanda miti kwa hiari yao bila makato yoyote?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tumepokea ushauri wa Mheshimiwa Mbunge na tuna kikao cha wadau ambacho tutajadili mambo haya na kuweza kukubaliana kwa pamoja. Kwa hiyo tumeuchukua ushauri wa Mheshimiwa Mbunge.