Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Minara ya simu katika Kata za Kikolo, Mbangamao, Kitanda na Kagugu - Mbinga?

Supplementary Question 1

MHE. JONAS W. MBUNDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwanza naishukuru Serikali kwa kuanza kutekeleza mradi wa kujenga mnara katika Kata ya Kitanda, kupitia mradi wa Tanzania ya Kidigitali. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, Serikali imetoa maelezo kwamba, Kata za Kikolo, Mbangamao na Kagugu zitafanyiwa tathmini; na maeneo hayo watu wakati mwingine wanapanda kwenye miti kutafuta mawasiliano: Nataka nijue sasa ni lini tathmini hiyo itaanza kufanyika? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; katika Kata ya Mpepai ulijengwa mnara ambao unaendeshwa na Kampuni ya Airtel, na wakati mwingine kunakuwa na changamoto ya mawasiliano, mtandao huwa haupatikani. Ninataka nijue ni lini sasa Serikali itafanya marekebisho katika eneo hilo? Ahsante. (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Jonas William Mbunda, Mbunge wa Jimbo la Mbinga Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, alitoa fedha kwa ajili ya kufanya tathmini katika vijiji 2,116. Na katika upande wa Mbinga, Vijiji vya Luanda, Muhongozi, Matili na Kitanda zilifanyiwa tathmini hiyo.

Mheshimiwa Spika, lakini katika mwaka wa fedha huu wa 2023/2024, Kata za Kikolo na Kagugu zitaingizwa katika utaratibu wa kufanyiwa tathmini na baada ya hapo fedha zitakapopatikana zitaweza kufikishiwa huduma ya mawasiliano.

Mheshimiwa Spika, kwa kipengele cha pili kuhusu mnara wa Airtel uliopo katika Kata ya Mpepai; changamoto ya mnara huu ni kwamba unatumia nguvu ya jua (solar energy) na tumeshakubaliana na watoa huduma kufanya mambo mawili yafuatayo; la kwanza ni kwamba pale ambapo umeme wa Gridi ya Taifa umeshafika wafanye juhudi za kuhakikisha kwamba wanaunganishwa na umeme wa Gridi ya Taifa.

Mheshimiwa Spika, na pale ambapo umeme wa Gridi ya Taifa haujafika basi wahakikishe kwamba wanaweka jenereta ili iwe njia mbadala pale ambapo solar inakuwa imezidiwa. Na hayo tayari tumeshakubaliana na hatua zimeshaanza kuchukuliwa, ni pamoja na katika eneo hili ambalo Mheshimiwa Mbunge amelitaja. Ahsante.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Minara ya simu katika Kata za Kikolo, Mbangamao, Kitanda na Kagugu - Mbinga?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Kata za Kijirishi na Nyaruhande, Wilaya ya Busega, kuna changamoto sana ya mawasiliano ya simu.

Je, ni lini Serikali itajenga minara ya simu katika kata hizo? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Midimu, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Simiyu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, eneo ambalo amelitaja Mheshimiwa Esther Midimu ni katika vijiji 2,116 ambavyo tayari vimeshafanyiwa tathmini. Hivyo, Serikali iko katika mchakato wa kutafuta fedha ili kuhakikisha kwamba tunafikisha mawasiliano katika maeneo hayo. Ahsante.

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Minara ya simu katika Kata za Kikolo, Mbangamao, Kitanda na Kagugu - Mbinga?

Supplementary Question 3

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Spika, ahsante, Wilaya ya Ngorongoro bado ina changamoto kubwa ya mawasiliano, na Mheshimiwa Naibu Waziri analifahamu hili suala vizuri.

Je, ni lini sasa mnara wa Simu wa Jema utawashwa ili basi wananchi wa Oldonyosambu na maeneo jirani waweze kupata mawasiliano ya kutosha? Ahsante.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zaytun Swai kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa Mheshimiwa Zaytun alishalifikisha jambo hili katika Wizara yetu na tayari tumeshachukua hatua. Jambo ambalo linafanyika sasa hivi ni technical audit na ikishakamilika mnara utawashwa. Ahsante.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Minara ya simu katika Kata za Kikolo, Mbangamao, Kitanda na Kagugu - Mbinga?

Supplementary Question 4

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Kuna changamoto ya mawasiliano kwenye Kata za Makanya, Malibwi, Kwai na maeneo mengine katika Jimbo la Lushoto: -

Je, ni lini mawasiliano yatapelekwa katika kata hizo?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shabani Shekilindi, Mbunge wa Lushoto, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba inafikisha huduma ya mawasiliano nchini kote na tunakwenda kwa awamu. Hivyo, nalipokea ili wataalam wetu waende wakafanye tathmini katika maeneo hayo na tujiridhishe changamoto yenyewe iko katika upande upi ili tuweze kuchukua hatua stahiki.

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Minara ya simu katika Kata za Kikolo, Mbangamao, Kitanda na Kagugu - Mbinga?

Supplementary Question 5

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Spika, je, ni lini Serikali itapeleka wakandarasi kwenye Vijiji vya Bokomnemera, Kimalamisale na Mpiji ambapo wana shida ya mawasiliano?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Michael Mwakamo, Mbunge wa Kibaha Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mwakamo tayari ameshalifikisha jambo hili na tulishaongea na tayari hatua zimeshaanza kuchukuliwa ili kufikisha huduma ya mawasiliano katika eneo hilo.

Name

Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Minara ya simu katika Kata za Kikolo, Mbangamao, Kitanda na Kagugu - Mbinga?

Supplementary Question 6

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kuna matatizo makubwa na ya muda mrefu ya mawasiliano katika Mapori ya Kasindaga na Kimisi Mkoa wa Kagera: -

Je, ni lini Serikali itamaliza matatizo hayo?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Conchesta kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba nipokee changamoto hii ili tukaifanyie kazi.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Minara ya simu katika Kata za Kikolo, Mbangamao, Kitanda na Kagugu - Mbinga?

Supplementary Question 7

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, viko Vijiji vya Mtawatawa, Ndapata, Ndunyungu na Ndinda, ambavyo havina mawasiliano kabisa. Ni lini Serikali itaona umuhimu wa kupeleka mawasiliano kwenye vijiji hivyo?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, wataalam wetu wameshafika katika maeneo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyataja, na tayari katika orodha ya vijiji 2,116 tukitoka hapa Mheshimiwa Kuchauka tuonane ili niweze kukuonesha maeneo ambayo tayari umeyataja, yamo tayari kwenye utaratibu.

Name

Muharami Shabani Mkenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Minara ya simu katika Kata za Kikolo, Mbangamao, Kitanda na Kagugu - Mbinga?

Supplementary Question 8

MHE. MUHARAMI S. MKENGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Katika Jimbo la Bagamoyo, Kata ya Magomeni, maeneo ya Sanzale, Kata ya Makurunge, Kamata ya Fukayosi maeneo ya Kijiji cha Mkenge, hakuna kabisa mawasiliano, ni ya shida sana. Ni lini sasa Serikali itapeleka wataalam kule kwenda kuweka minara mawasiliano yapatikane?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Muharami Mkenge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimesema kwamba tulianza na vijiji 2,116 ambapo ni katika mwaka wa fedha 2022/2023 na sasa katika awamu inayofwatia ambayo ni 2023/2024 vijiji na kata za Jimbo la Bagamoyo zitaingizwa katika utaratibu wa kufanyiwa tathmini na baadaye Serikali itatenga fedha kwa ajili ya kwenda kufikisha huduma ya mawasiliano, ahsante sana.