Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: - Je, lini Serikali italigawa Jimbo la Kilindi?

Supplementary Question 1

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nitumie nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri tu. Lakini pia nitumie nafasi hii kukupongeza wewe Mheshimiwa Mwenyekiti wangu wa Kamati ya Bajeti, hakika uko vizuri kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina maswali madogo mawili kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli usiopingika kwamba maeneo madogo ya utawala ni tofauti na maeneo makubwa ya utawala. Sasa je, nini mpango wa Serikali wa kuhakikisha kwamba maeneo madogo hayapewi rasilimali nyingi na watumishi wengi kuliko maeneo makubwa ya utawala? Swali la kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; nini mpango mkakati wa kuhakikisha kwamba maeneo yote makubwa ambayo yako sawa na Kilindi ambayo yanahitaji kugawanywa yanafanyiwa mkakati wa haraka ili yaweze kugawanywa? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Ummy Hamisi Nderiananga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE NA URATIBU): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Omari Mohamed Kigua, Mbunge wa Kilindi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwanza kumpongeza sana Mheshimiwa Omari Kigua kwa kazi nzuri anazofanya jimboni, lakini pia niendelee kumhakikishia kwamba Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, tunatambua uwepo wa maeneo haya makubwa na madogo ya kiutawala. Na kama nilivyojibu katika swali la msingi alilouliza, tutaendelea kufanya kazi kuona namna ambavyo tunaendelea kufikisha huduma karibu na wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme kwa ufafanuzi zaidi, vigezo tunavyovizingatia katika nchi za SADC ikiwemo na Tanzania tutaangalia pia ukubwa wa jimbo husika, mipaka ya kiutawala, hali ya kiuchumi na hali ya kijiografia pamoja na suala la idadi ya watu katika eneo husika, pamoja na uwezo pia wa Ukumbi wetu wa Bunge na idadi ya Wabunge wa Viti Maalum; yote hayo tutayaangalia katika mchakato huu alioulizia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, anasema pia maeneo makubwa; tunatambua na tunafahamu na nimelijibu swali hili hii ni mara ya pili ndani ya Bunge lako Tukufu. Maeneo haya ambayo ni makubwa tume kama ilivyopewa majukumu na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tutafanyia kazi maeneo hayo na tutaomba tuendelee kupata ushirikiano wa kutosha kwa Waheshimiwa Wabunge wote kwa pamoja na wadau wote wa masuala ya uchaguzi, ahsante. (Makofi)

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: - Je, lini Serikali italigawa Jimbo la Kilindi?

Supplementary Question 2

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri, Jimbo la Mbeya Mjini ni kubwa sana na lina kata zaidi ya 36 na wapigakura wengi; ni lini Serikali mtaamua kuligawa jimbo jilo ili liweze kumpa urahisi Mbunge husika waweze kugawa namna ya kulitumikia jimbo hilo?

Name

Ummy Hamisi Nderiananga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE NA URATIBU): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sophia Hebron Mwakagenda, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge, nimesema Serikali tunatambua lakini nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Mbeya Mjini ambaye ni Mheshimiwa Spika wetu, Mheshimiwa Dkt. Tulia, ameshawasilisha suala hili na lipo Mezani. Kwa hiyo, muda utakapofika Tume ya Taifa ya Uchaguzi itatazama pia Jimbo la Mbeya Mjini, ahsante. (Makofi)

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: - Je, lini Serikali italigawa Jimbo la Kilindi?

Supplementary Question 3

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Jimbo la Kishapu lina jumla ya kata 29, lina square kilometers 48,000; lina vijiji 117. Eneo hili kiutawala ni kubwa sana; ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba jimbo hili linagawanywa?

Name

Ummy Hamisi Nderiananga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE NA
URATIBU): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Boniphace Nyangindu Butondo, Mbunge wa Kishapu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan inatambua uwepo wa maeneo makubwa, kama alivyosema huku Kishapu kata 26 na vijiji 117. Mheshimiwa Mbunge, kwa kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi inaendelea na maandalizi ya Uchaguzi Mkuu ujao, muda utakapofika tutaangalia vigezo na masharti ili kuona kama jimbo hili linafaa kugawanywa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwa niaba ya Serikali niwatoe hofu Waheshimiwa Wabunge wote, kwenye eneo hili yapo majimbo mengi, kwa hiyo tutayafanyia kazi Waheshimiwa Wabunge. Karibu tuungane pamoja na wadau wengine wa Uchaguzi tutoe maoni na nina imani tutafanya vizuri tu, ahsante. (Makofi)

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: - Je, lini Serikali italigawa Jimbo la Kilindi?

Supplementary Question 4

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Tabora Mjini lenye kata
29 na wakazi sasa katika sensa hii nadhani hawatapungua 500,000 kwenye jimbo moja, na tulishawasilisha maombi ya kuligawa jimbo hilo kwa muda mrefu: -

Lini Serikali itaweza kuligawa jimbo hilo ili liweze kuwa na majimbo angalau mawili? Ahsante.

Name

Ummy Hamisi Nderiananga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE NA
URATIBU): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Emmanuel Adamson Mwakasaka, Mbunge wa Tabora Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, tunatambua ukubwa pia wa Jimbo la Tabora Mjini. Lakini vilevile niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge wote na Mheshimiwa Mwakasaka kwamba muda utakapofika, tume tayari tumeanza maandalizi ya uchaguzi wa mwaka 2025, tutashirikiana kwa ukaribu kuona namna ambavyo tunaweza tukagawa majimbo hayo kwa mujibu wa vigezo na masharti. Na niwaambie kwamba tutazingatia pia suala la idadi ya watu, hususan iliyotokana na Sensa yetu ya Watu na Makazi, itaendelea pia kutuongoza kwenye kipengele hicho namna ambavyo tunaweza kufanya, ahsante.