Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Wilayani Kilombero baada ya wanachi kutenga eneo la hekari 30?

Supplementary Question 1

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Spika, tunaishukuru Serikali walau Wilaya ya Kilombero sasa inapata chou cha VETA. Swali la kwanza, mtalifanyia nini eneo Kata ya Kisawasawa mlilopewa na wananchi na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara, maana wataalam wameshaenda na wameshalichukua hilo eneo?

Swali la pili, kule shamba Nakaguru Mchombe ambako mnakwenda kujenga hicho chuo cha VETA hakuna hata barabara, na fedha milioni 45 ni ndogo sana. Je, ni lini fedha zingine zitaongezwa?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Asenga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyokwisha eleza kwenye majibu ya swali la msingi, wajibu wa kutambua au kuamua ni eneo gani chuo kiende kujengwa ni mamlaka za wilaya pamoja na mikoa. Kwa hiyo nimwondoe wasiwasi kwanza Mheshimmiwa Asenga na Bunge lako Tukufu, kwamba eneo hili la Kisawasawa alilolitaja ambalo labda lilitengwa awali na mamlaka za wilaya au na mkoa na kukabidhiwa Wizara ya Elimu nimwondoe shaka na wasiwasi, Serikali bado ina mipango mingi na mikubwa eneo hili bado tuna uhitaji nalo na tutapanga utaratibu mwingine na miradi mingine ya kimaendeleo inaweza kupelekwa katika eneo hilo.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na swali lake la pili, kwamba fedha iliyopelekwa ni ndogo ni kweli, tumepeleka fedha milioni 45 kwa ajili ya kazi zile za awali ambayo ilikuwa ni masuala ya geotechnical survey, topographical survey pamoja na environmental and social impact assessment. Hivi sasa tayari fedha kwa ajili ya kazi zile za substructure pamoja na superstructure ela zake tayari tumeshazipata. Nadhani ndani ya wiki hii au wiki ijayo fedha hizo zitakwenda kule kwa ajili ya kuanza rasmi ujenzi huo wa majengo yale tisa kama tulivyoweka kwenye mpango wetu.

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Wilayani Kilombero baada ya wanachi kutenga eneo la hekari 30?

Supplementary Question 2

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Je, ni lini Serikali itakikarabati Chuo cha Ufundi Music ambacho kiko Korogwe ambacho ni kikongwe na kimechakaa sana?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Timotheo Paul Mnzava Mbunge wa Korogwe kama ifuatavyo:
-

Mheshimiwa Spika, tunafahamu uwepo wa chuo hiki cha FDC pale Korogwe, na katika nchi yetu tuna vyuo 54 vya FDC ambavyo vingi sana ni vya muda mrefu. Tumeanza kufanya ukarabati tangu mwaka 2020/2021 katika bajeti ile na tumeweza kuvikia vyuo 35 kufanya ukarabati pamoja na upanuzi. Nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge, katika bajeti yetu hii ya 2023/2024 tunakwenda kuvifikia vyuo 21 vilivyobaki kikiwemo na hiki cha Korogwe.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Wilayani Kilombero baada ya wanachi kutenga eneo la hekari 30?

Supplementary Question 3

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Chuo cha VETA Nyasa kina course mojawapo ambayo ni ya udereva lakini chuo hicho hakina gari kabisa ikiwemo ya utawala.

Je, nini mpango wa Serikali kukisaidia chuo hicho?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Manyanya Mbunge wa Nyasa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika bajeti yetu ya mwaka huu 2023 tuliweka azma ya ununuzi wa vifaa vya kufundishia pamoja na samani kwa ajili ya vile vyuo 25 vya Wilaya vipya pamoja na vyuo vine vya mikoa. Nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Manyanya, katika bajeti yetu ijayo ya 2023/2024 tutaendelea kuweka bajeti kwa ajili ya ununuzi wa vifaa ikiwemo na magari ya kufundishia pamoja na vifaa mbalimbali vya kujifunzia kwa ajili ya vyuo vyetu vile vya zamani lakini pamoja na hivi vipya.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Wilayani Kilombero baada ya wanachi kutenga eneo la hekari 30?

Supplementary Question 4

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona. Jimbo la Kilwa kusini halina chuo cha VETA na hakuna mpango wowowte wa Serikali kujenga chuo hicho isipokuwa tuna Chuo cha Maendeleo ya Wananchi pale Kilwa Masoko ambapo miundo mbinu yake ni ya muda mrefu na imechakaa. Sasa hivi kipaumbele chetu ni kujenga bwalo na tulishaomba.

Je, lini Serikali italeta fedha hizi kwa ajili ya ujenzi wa bwalo pale chuo cha wananchi Kilwamasoko?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Kassinge Mbunge wa Kilwa Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kama nilivyokwisha eleza kwamba mpango wa Serikali ni ujenzi wa vyuo 64 katika wilaya ambazo hazina, miongoni mwa Wilaya hizo ni pamoja na Wilaya ya Kilwa. Sasa utaratibu gani wa eneo gani linakwenda kujengwa, aidha ni Kilwa Kusini au ni Kilwa Kaskazini ni maamuzi ya Wilaya au Mkoa wa Lindi kuamua chuo hicho kinakwenda kujengwa wapi. Tunatambua uwepo wa Chuo cha FDC pale kulwa Kusini na mimi nakifahamu chuo hiki na tunajua kwamba tunauhitaji wa bwalo pamoja na baadhi ya mabweni. Kama nilivyosema kwa upande wa Korogwe katika mwaka ujao wa fedha tutatenga fedha kwa ajili ya kufanya ukarabati wa vyuo vile, kuongeza miundombinu ya mabweni pamoja na mabwalo, kama alivyoomba Mheshimiwa Mbunge. Kwa hiyo nimwondoe wasiwasi katika bajeti ijayo mambo mazuri yanakuja.

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Wilayani Kilombero baada ya wanachi kutenga eneo la hekari 30?

Supplementary Question 5

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.

Je, ni lini Serikali itajenga karakana ngumu na mabweni katika Chuo cha VETA kilichopo Kitangali ili kuwezesha vija wengi kupata mafunzo?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Hokororo Mbunge wa Viti Maalumu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli na mimi nilishawahi kufika pale Kitangali, majengo yale yaliyokuwepo ni machache. Nakumbuka tuliweka kwenye bajeti yetu ya mwaka huu kwamba tuongeze majengo, madarasa na karakana katika Chuo kile cha Kitangali. Namwomba Mheshimiwa Hokororo mara tu baada ya kipindi hiki cha maswali tuweze kuonana tuweze kuangalia kwa nini fedha zile zaidi ya milioni 200 ambazo tulizitenga katika bajeti yetu ya mwaka huu kwa ajili ya kwenda kuongeza miundombinu katika chuo kile cha Kitangali kama hazijakwenda tuweze kuzipeleka kwa haraka.

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Wilayani Kilombero baada ya wanachi kutenga eneo la hekari 30?

Supplementary Question 6

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa swali la nyongeza. Chuo cha VETA Ulyankulu kimechaka sana na hakina majengo ya kutosha, lakini 2020/2022 kilitengewa bajeti ya shilingi milioni 638; fedha zile zilichukuliwa zikarudishwa Wizarani.

Je, Serikali iko tayari sasa kuzirudisha zile milioni 638 kwa ajili ya kufanya ukarabati wa chuo changu?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rehema Juma Migilla, sina taarifa kamili ya fedha hizi labda baada ya kipindi hiki tuweze kuonana na Mheshimiwa Mbunge.

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Wilayani Kilombero baada ya wanachi kutenga eneo la hekari 30?

Supplementary Question 7

MHE. USSI SALUM PONDEZA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Mimi ningependa nimuulize swali dogo la nyongeza Mheshimiwa Waziri. Campus ya Marine Science ambayo iko Zanzibar nayo imekuwa na uhaba wa madarasa;

Je, nayo imo katika mpango wa vile vyuo 21 vitakavyopata matengenezo makubwa?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Ussi Salum Pondeza, Mbunge wa Chimboni kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, vyuo 64 tunavyo vizungumza hapa ni kwa upande wa Tanzania bara. Kwa upande wa Tanzania Zanzibar tuna utaratibu maalum ambao tunautumia tukishirikiana na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar. Kwa hiyo kwa upande wa ukarabati wakule bajeti itatengwa kwenye Wizara ile ili kuhakikisha maeneo yale ambayo yanahusika na vyuo vya ufundi kwa upande wa Zanzibar yanakwenda kushughurikiwa.

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Wilayani Kilombero baada ya wanachi kutenga eneo la hekari 30?

Supplementary Question 8

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza kama ifuatavyo: -

Pamoja na kuishukuru Serikali kwa kutuanzishia VETA wilayani Irambo, je, ni lini Serikali itatuongezea majengo ili tupate mafunzo ambayo hatuyapati kutokana na uhaba wa majengo? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Margaret Simwanza Sitta Mbunge wa Urambo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, vyuo hivi vya zamani viko zaidi ya vyuo 44, na ni kweli kabisa vina uhitaji mkubwa wa majengo, vifaa vya kufundishia pamoja na rasilimali watu. Nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kama nilivyokwisha kujibu maswali yaliyotangulia. Kwa upande wa pale Urambo tunajua kwamba chuo kile kina majengo machache ikiwemo na uhaba wa karakana pamoja na mabweni. Katika bajeti yetu ijayo tutahakikisha kwamba tunatenga fedha ili kuongeza miundombinu hiyo ya maabara, karakana pamoja na mabweni kwa ajili ya Chuo chetu cha Urambo. Kwa hiyo tuwasilinae tu Mheshimiwa Sitta ili tuliweke vizuri hili, nakushukuru sana.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Wilayani Kilombero baada ya wanachi kutenga eneo la hekari 30?

Supplementary Question 9

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Miongoni mwa Wilaya ambazo hatuna chuo kipya cha VETA ni pamoja na Wilaya ya Bunda;

Je, ni lini sasa Serikali mtatujengea Chuo cha VETA katika Wilaya ya Bunda ili vijana wetu waweze kupata ujuzi na kujiajiri wenyewe?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Bulaya Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyokwisha eleza kwenye majibu ya swali la msingi, katika mwaka wa fedha 2022/2023, yaani huu tunao endelea nao, tunawilaya 64 na mkoa mmoja ambao hauna chuo cha VETA Mkoa huo ni wa Songwe. Wilaya hizi 64 miongoni mwa Wilaya ya Bunda. Kwa hiyo nikuondoe wasiwasi, katika Mkoa wa Mara tuna wilaya nne ambazo ni Serengeti, Bunda, Tarime, ndizo wilaya ambazo hazina vyuo vya VETA. Katika mwaka huu tayari tumeshapeleka fedha zile za awali na sasa tuna peleka fedha awamu ya pili kwa ajili ya kuanza ujenzi rasmi ikiwemo na chuo hiki cha Wilaya ya Bunda. Kwa hiyo nenda kawaambie wananchi Serikali ya Mama Samia iko kazini inawatendea haki wana Bunda.