Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa kiwango cha lami wa barabara ya Singida – Ilongero hadi Haydom?

Supplementary Question 1

MHE. ABEID R. IGHONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana pamoja na majibu hayo mazuri ya Serikali nina maswali madogo mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza; kwa kuwa upembuzi yakinifu sasa umekamilika je, Serikali iko tayari sasa kutenga fedha kwenye bajeti hii tunayoijadili hivi sasa ya 2023/2024 kwa ajili ya kuanza rasmi ujenzi wa barabara hiyo ambayo inakwenda mpaka makao makuu ya halmashauri? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili je, Serikali sasa iko tayari kufanya upembuzi yakinifu kwa kipande kinachounganisha barabara hii cha kutoka hapo Ilongero makao makuu ya halmashauri kupitia Ighanoda kwenda ngamu kilomita 27.1 ambayo inatuunganisha na Wilaya ya Hanang Mkoa wa Manyara? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi, kwamba tumeshakamilisha usanifu wa hii barabara na sasa Serikali inaendelea kutafuta fedha. Na nataka nisiji-commit hapa, kwamba kama bajeti tumeshatenga, lakini itategemea na upatikanaji wa fedha, kwa sababu baada ya kukamilisha usanifu kazi inayofata ni kuijenga hiyo barabara kwa kiwango cha lami; na ndiyo hiyo dhamira ya Serikali kujenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kuhusu barabara aliyoitaja ambayo inaanzia Ilongelo hadi Ngamo ni barabara fupi kama kilomita zisizozidi 27. Naomba nimuagize Meneja wa Mkoa afanye tathmini ya gharama kwa ajili ya kuanza kufanya usanifu kwa barabara hiyo, halafu aipeleke Makao Makuu kwa ajili ya kufikiria kuiweka kwenye mpango wa kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa hicho kipande cha barabara cha Ilongelo kwenda Ngamo, ahsante.