Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA K.n.y. MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua changamoto za mawasiliano ya simu Kata za Milepa, Zimba, Kaengesa na Lusaka?

Supplementary Question 1

MHE BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza. Swali la kwanza; Kata ya Mpui, Ikozi na Lusaka hayana kabisa minara ya simu. Ni lini sasa Serikali itajenga minara ya simu kwenye kata hizo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; minara iliyopo Kata ya Milepa, Zimba, Mfinga na Lusaka minara hiyo haina kabisa internet. Ni lini sasa Serikali itaweza kuweka internet kwenye minara hiyo hili wananchi wasiweze tena kupanda kwenye miti kutafuta internet? Ahsante. (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; kuhusu kata ya Mpui pamoja na Ikoze Serikali iko katika utaratibu wa kufanya tathimini na tathimini hiyo itakapokamilika Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kufikisha huduma ya mawasiliano katika kata hizi.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili maeneo ya Milepa pamoja na Zimba ni azima ya Serikali kupitia Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya kuhakikisha kwamba tunapanua wigo wa matumizi ya internet kutoka asilimia 45 mpaka 80 Serikali imeshaanza na minara 488 katika awamu ya kwanza na katika awamu ya pili tutajumuisha Kata ya Milepa na Zimba ili wananchi wa maeneo hayo wapata huduma ya internet, ahsante.

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA K.n.y. MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua changamoto za mawasiliano ya simu Kata za Milepa, Zimba, Kaengesa na Lusaka?

Supplementary Question 2

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Katika Jimbo la Arumeru Magharibi kuna kata kama tano ambazo hazina mawasiliano Kata ya Bwawani yenye vijiji vinne, Olonyowase yenye vijiji vinne, Oljoro yenye vijiji vitatu, Laroi vijiji vitatu na Mwande vijiji vitatu.

Je, ni lini sasa Serikali itapeleka minara na kuhakikisha kwamba wananchi wale ambao wanateseka kupanda juu ya miti na juu ya milima na vigongo kwa ajili ya kupata mawasiliano ya kuwasiliana?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kupokea changamoto ya mawasiliano katika kata ambao Mheshimiwa Mbunge, amezitaja. Tutazifanyia kazi na baadae tutamrejea kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunafikisha huduma ya mawasiliano.

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA K.n.y. MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua changamoto za mawasiliano ya simu Kata za Milepa, Zimba, Kaengesa na Lusaka?

Supplementary Question 3

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru napenda kujua ni lini wananchi wa Kata ya Masisile, Udekwa, Ilole na Nyanzwa katika Wilaya ya Kilolo watapata mawasilino ya simu na kuacha kupanda miti? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZARI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, Kata ya

Masisiwe, Udekwa, Mahenge, Kimara, Kilolo pamoja na Ebomu tayari Serikali inaenda kuingia mikataba na watoa huduma kesho tarehe 13 kwa ajili ya kufikisha huduma ya mawasiliano katika Jimbo la Kilolo. (Makofi)

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA K.n.y. MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua changamoto za mawasiliano ya simu Kata za Milepa, Zimba, Kaengesa na Lusaka?

Supplementary Question 4

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa kuwa kumekuwa na changamoto kubwa ya mawasiliano kwenye Kata ya Jana, Mwalugulu, Kashishi, Chela na maeneo mengine je, ni lini sasa Serikali itaanza rasmi ujenzi wa minara hii katika maeneo hayo? Ahsante. (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshmiwa Naibu Spika, kwa Kata ya Jana tayari tumepata mtoa huduma Vodacom, Kata ya Mwalugulu tumepa mtoa huduma tigo na kata zingine na uhakika kwamba Mheshimiwa Mbunge akishatoka hapa tutawasiliana ili ajue watoa huduma gani wanaenda kutoa huduma katika maeneo hayo.

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA K.n.y. MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua changamoto za mawasiliano ya simu Kata za Milepa, Zimba, Kaengesa na Lusaka?

Supplementary Question 5

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru Kata ya Kapele pamoja na Kata ya Mkomba katika Jimbo la Momba ni miongoni mwa kata ambazo zenye shida kubwa sana ya mawasiliano. Naomba kufahamu ni lini Serikali itapeleka mawasilino katika kata hizo? Ahsante.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, kata ambazo amezitaja Mheshimiwa Mbunge zipo katika vijiji 2,116 ambavyo tunasubiri Serikali ipate fedha ili tuweze kufikisha huduma ya mawasiliano katika maeneo hayo. (Makofi)