Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaweka alama za mipaka kutenganisha maeneo ya hifadhi na vijiji 975 vilivyotolewa kwenye Hifadhi?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali lakini nina maswali mawili ya nyongeza la kwanza baada ya ziara ya mawaziri nane kwenye maeneo yetu ya Wilaya Sikonge. Serikali ilituma timu ya watalamu ambao ilifanya kazi na viongozi wa vitongoji, vijiji na kata na mimi kazi hiyo waliyoifanya narizika. Kwa sababu waliweka mipaka na rangi kwenye hiyo mipaka.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika maeneo ambayo nitayataja Luseseko, Isenga na Manzagata, Misulu, Simbaudenga, Ngakaro, Kawemimbi na Manyanya ya 2,567 zina wakazi 25,000. Sasa swali la kwanza je, ni lini hasa kwenye maeneo haya yenye wakazi wengi watakuja kuweka bikoni ili kuwaondolea wasiwasi wananchi wangu? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili kwa kuwa uamuzi wa Serikali wa mwaka 2019 uliondoa zile mita 500 za bafa zone ambazo zilikuwa chini ya hifadhi kipindi kile sasa zikawa chini ya halmashauri ili waweze wananchi kuzitumia je, hizo mita 500 kuzunguka maeneo yote ya hifadhi wananchi watakabidhiwa lini kwenye halmashauri? (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza suala la lini hasa bikoni zile zinaenda kuwekwa, nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge katika eneo lako watalamu wanakwenda kuendelea na shughuli hizi. Kwa sababu mpaka sasa watu wako uwandani wanaendelea na kazi. Kitu cha msingi kikubwa kuweka msukumo mkubwa ambao watawezesha sasa alama zote katika maeneo husika ziweze kufikiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, niwaombe Waheshimiwa Wabunge wote katika maeneo yenu yanayopitiwa na hii miradi tuwaombe wananchi wawe watulivu sana katika zoezi hili kwa sababu wakati mwingine linapotoshwa katika ile tafsiri halisi wakati utekelezaji umesimama imara kabisa.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; hii bafa zone ambayo tumeiyondoa katika maeneo yetu, wakati zoezi la upimaji wa vijiji unao endelea ndiyo wakati ambao utabainisha hizi mita 500 za eneo ambalo zinatakiwa zirudishwe kwenye halmashauri, naomba tu tuwe watulivu wakati zoezi hili likiendelea, ahsante.