Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Janejelly Ntate James

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANEJELLY J. NTATE K.n.y. MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza: - Je, nini tamko la Serikali kuhusu Kitambulisho cha Taifa kuwekwa ukomo wa kutumika?

Supplementary Question 1

MHE. JANEJELLY J. NTATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; je, wale ambao walipewa namba za NIDA kabla ya tarehe ya GN Namba 96 ya Mwaka 2023, vitambulisho vyao vitatoka vikiwa na ukomo au vitakuwa havina ukomo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, je, Serikali imejipangaje kuleta uelewa kwa wananchi ili wajue kwamba vitambulisho vyao ambavyo vimekaribia kuwa na ukomo na ambavyo vina ukomo havitawaathiri ili kupunguza taharuki iliyo kwa wananchi sasa? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, vitambulisho ambavyo vitakuja baada ya tangazo hili havitakuwa na ukomo lakini hata vile vitambulisho ambavyo vimekuja kabla ya tangazo wataendelea. Kwa sababu lengo la Serikali hii ni kuhakikisha kwamba vitambulisho haviwezi kuwafanya watu wakakosa huduma zao muhimu. Kwa hiyo ndio maana tukasema kwamba vitambulisho ambavyo vitakuja baada ya tangazo hili havitakuwa na ukomo, lakini hata vile ambavyo tunasema vimeshakwisha muda navyo vilevile vitaendelea kutumika kuwapatia wananchi huduma mpaka pale Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi itakapotoa maelekezo mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vipi wananchi watafikiwa na taaluma hiyo. Kwanza kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mheshimiwa Waziri ameshatoa tangazo kupitia vyombo vya habari kama vile televisheni, redio na magazeti. Nadhani wengi ambao wanakwenda kwenye mitandao huko wameona, lakini kikubwa tumeshatoa maelekezo na tupo tayari muda wowote tunaweza tukaanza mafunzo kwa watendaji wote wa NIDA kuwapa maelekezo na mafunzo ili sasa waanze kuwafundisha wananchi ili wananchi waweze kujua huu mchanganuo wa kipi kimekwisha ukomo na kipi hakitakwisha ukomo na kipi kitatumika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.