Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sophia Mattayo Simba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA M. SIMBA (K.n.y. MHE. ANATROPIA L. THEONEST) aliuliza:- Kuna mgogoro wa ardhi baina ya wananchi wa Kipunguni „A‟ na Kipunguni Mashariki dhidi ya Mamlaka ya Uwanja wa Ndege Jijini Dar es Salaam. Wananchi hao wanapinga uthamini uliofanywa na fidia kidogo kwa kikundi cha watu wachache, huku wengine wakizuiwa kuendeleza maeneo yao? (a) Je, ni lini Serikali itaenda kumaliza mgogoro huo uliodumu tangu 2007? (b) Je, Serikali ipo tayari kuwapa fidia ya kiwango cha soko wananchi waliozuiwa kuendeleza maeneo yao na kuendelea kubaki maskini kwa muda wote huo?

Supplementary Question 1

MHE. SOPHIA M. SIMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri na nina maswali mawili ya nyongeza.
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali ni chanzo kikubwa cha migogoro ya ardhi mijini kwa kuangalia wananchi wakijenga maeneo ambayo hayaruhusiwi na wanajenga majengo makubwa, mazuri na matokeo yake Serikali inashindwa kulipa fidia kutokana na gharama kubwa. Je, Serikali itaweka utaratibu gani wa kuwapa nguvu maafisa mbalimbali wa chini
wakiwemo Wenyeviti na Watendaji wa Mitaa kuhakikisha maeneo haya hayavamiwi? (Makofi)
(b) Kwa kuwa wananchi walioamishwa Kipawa kupelekwa Kinyamwezi baadhi yao mpaka leo hawajalipwa fidia. Je, Serikali inasema nini kwa sababu imewaletea wale wananchi umaskini, inabidi wauze vile viwanja na kwa hiyo umaskini unaendelea. Naomba anihakikishie, hawa ambao wako Kinywamwezi siku nyingi, wamepelekwa hawana la kufanya, hawana pesa ya kujengea watalipwa lini sasa? Ahsante.

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza amezungumzia habari ya kupewa nguvu wananchi ili kuweza kuzuia pasiwepo na ujenzi holela kwa sababu watu wanajenga majengo katika maeneo yasiyoruhusiwa na baadaye wanabomolewa. Naomba niseme tu kwamba, nadhani ilikuwa ni Aprili kama sikukosei ambapo Wizara ilichukua hatua mahsusi ya kushirikisha Wenyeviti wa Serikali za Mitaa katika maeneo mbalimbali kwa kuwapatia ramani na tulianzia kwenye Mkoa wa Dar es Salaam. Lengo la Wizara kutoa ramani hizi kwa viongozi wa maeneo hayo ni kutaka pia kuwafanya wao wawe na wajibu wa kuweza kulinda maeneo yao. Kwanza watambue eneo lao na matumizi ya ardhi katika eneo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ni wazi wakishaona ile ramani na kwa sababu walielezewa pia, kwa sababu kumpa ramani peke yake bila kufungua akili na mawazo yake na akajua maana ya michoro ile inakuwa ni kazi bure lakini walielezwa wapi pana maeneo ya wazi, wapi panastahili kujengwa nini na wapi hapastahili kujengwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, lengo la Serikali kutaka kuwapa nguvu kwanza ni kuwapa yale mamlaka yao kamili kuweza kuwa sehemu ya ulinzi wa maeneo yao kuepuka ujenzi holela ambapo wakati mwingine watu wanabomolewa kwa kujenga maeneo yasiyoruhusiwa, maeneo ambayo yanahitaji pengine kuwa na jengo fupi mtu anajenga jengo refu lakini hayo yote tumewawezesha Wenyeviti wa Serikali za Mitaa na Kamati zao waweze kuyatambua. Napenda kusema kwamba tunatakiwa kuendelea kutoa ramani hizo kwa Wenyeviti ili kero ya Dar es Salaam isije ikaenda na maeneo mengine ili tuanze kudhibiti kabla haijafika ingawa kuna maeneno mengine pia yana tatizo hilo hilo.
Kipawa na Kinyamwezi ni lini watalipwa stahiki zao waache kusumbuliwa ili waweze kujenga nyumba zao? Nimesema kabisa kwamba, sheria iliyotumika kipindi kile cha kuwalipa ilikuwa inazungumzia suala zima la Land Acquisition Act ya mwaka 1967.
Mheshimiwa Naibu Spika, ile sheria ilikuwa inataka tu mtu alipwe kwa maendelezo yaliyopo na anapewa kiwanja ili aweze kwenda kujenga tena katika maeneo mengine. Kusema kwamba Serikali pengine itawawezesha ili waweze kujenga, hilo halitawezekana kwa sababu sheria haitaki ifanyike hivyo. Sheria ikishakupa thamani ya maendelezo yako, ikakupa na kiwanja, sasa ni jukumu la wewe kufanya hivyo. Uzuri ni kwamba thamani inayotolewa ni ile iliyoko katika soko. Kwa hiyo, tuna uhakika kwamba pengine inaweza ikamwezesha mwananchi kurudia katika hali yake.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA M. SIMBA (K.n.y. MHE. ANATROPIA L. THEONEST) aliuliza:- Kuna mgogoro wa ardhi baina ya wananchi wa Kipunguni „A‟ na Kipunguni Mashariki dhidi ya Mamlaka ya Uwanja wa Ndege Jijini Dar es Salaam. Wananchi hao wanapinga uthamini uliofanywa na fidia kidogo kwa kikundi cha watu wachache, huku wengine wakizuiwa kuendeleza maeneo yao? (a) Je, ni lini Serikali itaenda kumaliza mgogoro huo uliodumu tangu 2007? (b) Je, Serikali ipo tayari kuwapa fidia ya kiwango cha soko wananchi waliozuiwa kuendeleza maeneo yao na kuendelea kubaki maskini kwa muda wote huo?

Supplementary Question 2

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona. Kwa kuwa wananchi wa Kipunguni Serikali inakiri kabisa kwamba haijawalipa fidia na kwa kuwa Serikali imeonyesha kabisa nia ya wazi kwamba wanalihitaji eneo la Kipunguni kwa upanuzi wa Uwanja wa Ndege, je, Serikali ina mkakati gani sasa wa muda mfupi kuwasaidia wananchi wale wa Kipunguni kwa kuwa hawana maendeleo na wala hawakopesheki?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mariam Kisangi ameuliza Serikali ina mkakati gani wa kuweza kuwawezesha wananchi hao ili waweze kuondokana na adha waliyonayo? Naomba nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kama tulivyoeleza wakati wa bajeti kwamba tunakwenda kupitia taasisi zote ambazo zinadaiwa na wananchi kwa maana wametwaa maeneo yao lakini hawajalipa fidia ili tuweze kuwasisitiza waweze kulipa fidia hizo mapema. Kwa sababu ni kweli imekuwa ni muda mrefu, hata kama utapiga hesabu kwa kuweka 6% bado inakuwa ni ngumu kwa sababu kadri wanavyochelewesha kulipa ndivyo jinsi mwananchi anavyozidi kuumia. Kwa hiyo, Wizara inachukua hatua kwanza kuwabaini wale wote ambao wanadaiwa kwa maana kwamba wametwaa maeneo ya wananchi ili waweze kuwalipa.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia kama hiyo haitoshi, Wizara imetoa Waraka Na. 1 wa mwaka 2015 wa Uthamini na Ulipaji wa Fidia ambao unataka kwa siku za baadaye, iwe taasisi au mtu binafsi akitaka kuchukua eneo la mtu ni lazima alipe kwanza fidia na Wizara lazima ijiridhishe kwamba kuna pesa ambayo ipo itakwenda kulipa watu hao kabla ya maeneo hayo kuchukua ili kuepuka hii migogoro ambayo imekuwa mingi. Kwa hiyo, Waraka Na.1 wa mwaka 2015 sasa hivi tunausimamia na wakati huo huo tunawafuatilia wale ambao wanadaiwa kuweza kuwa-push ili waweze kulipa fidia za watu ambao wanawadai.

Name

Mwantakaje Haji Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Bububu

Primary Question

MHE. SOPHIA M. SIMBA (K.n.y. MHE. ANATROPIA L. THEONEST) aliuliza:- Kuna mgogoro wa ardhi baina ya wananchi wa Kipunguni „A‟ na Kipunguni Mashariki dhidi ya Mamlaka ya Uwanja wa Ndege Jijini Dar es Salaam. Wananchi hao wanapinga uthamini uliofanywa na fidia kidogo kwa kikundi cha watu wachache, huku wengine wakizuiwa kuendeleza maeneo yao? (a) Je, ni lini Serikali itaenda kumaliza mgogoro huo uliodumu tangu 2007? (b) Je, Serikali ipo tayari kuwapa fidia ya kiwango cha soko wananchi waliozuiwa kuendeleza maeneo yao na kuendelea kubaki maskini kwa muda wote huo?

Supplementary Question 3

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Kwa kuwa migogoro ya ardhi hapa nchini ni mingi na kwa kuwa migogoro ya ardhi inafanana, je, Serikali ina mapango gani wa kumaliza tatizo la Tabora Manispaa katika Kata ya Malolo ambalo mpaka Mheshimiwa Waziri wa Ardhi alifika akaona hali halisi na akatoa maelekezo lakini mpaka sasa halijatekelezwa? Je, kwa leo Serikali inatoa tamko gani kwa tatizo la Malolo?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwanne Mchemba ambaye anataka kujua ni lini Serikali itamaliza mgogoro katika Manispaa ya Tabora kama alivyolielezea. Naomba niseme kwamba, Waheshimiwa Wabunge wote ni mashahidi kwamba migogoro ya ardhi imekuwa ni mingi sana kama hivyo amekiri wazi kwamba Mheshimiwa Waziri alikwenda na akatoa maelekezo lakini bado mgogoro ule haujamalizika na hata wakati amekwenda bado kulikuwa na migogoro mingine katika maeneo hayo. Kwa hiyo, tumejikuta kama Wizara pengine unakwenda ku-solve mgogoro mmoja ukirudi unakuta mwingine uko pale pale katika lile eneo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nilichukue hili suala la Mheshimiwa Mchemba kwa sababu tayari maelekezo yapo. Nitakachofanya ni kufuatilia kuweza kujua kwa nini yale maelekezo ya Mheshimiwa Waziri hayakutekelezwa mpaka leo halafu tuweze kuchukua hatua kwa wale ambao walipewa maelekezo hayo. Kwa sababu kwa sehemu kubwa wale Makamishina Wasaidizi katika Kanda ambao wapo wanatakiwa pia maagizo yakishatolewa na Mheshimiwa Waziri waweze kusimamia utekelezaji wake mpaka mwisho. Kama hili halijatekelezwa, ni wazi hata Kamishna Msaidizi wa Kanda ile hajatekeleza wajibu wake kama jinsi anavyopaswa kufanya. Kwa hiyo, tutalifuatilia kuweza kujua ili hatua ziweze kuchukuliwa.

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. SOPHIA M. SIMBA (K.n.y. MHE. ANATROPIA L. THEONEST) aliuliza:- Kuna mgogoro wa ardhi baina ya wananchi wa Kipunguni „A‟ na Kipunguni Mashariki dhidi ya Mamlaka ya Uwanja wa Ndege Jijini Dar es Salaam. Wananchi hao wanapinga uthamini uliofanywa na fidia kidogo kwa kikundi cha watu wachache, huku wengine wakizuiwa kuendeleza maeneo yao? (a) Je, ni lini Serikali itaenda kumaliza mgogoro huo uliodumu tangu 2007? (b) Je, Serikali ipo tayari kuwapa fidia ya kiwango cha soko wananchi waliozuiwa kuendeleza maeneo yao na kuendelea kubaki maskini kwa muda wote huo?

Supplementary Question 4

MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza. Tatizo la ufidiaji liko pia katika Jimbo langu la Morogoro Kusini hasa kwenye Kijiji cha Kivuma. Kuna mwekezaji amekuja pale ameanza kuchimba mawe bila kulipa fidia kwa wahusika. Je, nini kauli ya Serikali kwa mwekezaji huyu ambaye hajalipa fidia kwa wahusika wenye umiliki wa ardhi wa pale Kivuma?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Omary Mgumba amesema kwamba kuna mtu ameanza kuchimba mawe katika eneo ambalo wananchi wake hawajalipwa fidia. Kwa sababu hatuhitaji kuendelea kuwa na migogoro isiyo na msingi na kama hajalipa fidia na huu ni mgogoro mpya pengine ambao umeanza siyo siku nyingi kwa sababu sina uhakika kama uko kwenye ile orodha ya migogoro, nimtake Mkurugenzi wa Halmashauri husika afike kwenye hilo eneo aweze kuangalia mgogoro uliopo na kutoa ufumbuzi wa mara moja kwa sababu ni suala ambalo linahitaji sheria ikamilike katika utekelezaji wake ndipo huyu aendelee na kazi yake ya uchimbaji. Kama hajakamilisha, basi ni lazima Mkurugenzi asimamie hilo kuhakikisha wale watu wanapata haki yao na huyu aweze kuendelea na shughuli yake.