Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Santiel Eric Kirumba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kuhimiza mashirika mengine ya simu kujiunga na mpango wa M-Mama kwani umekuwa msaada kwa wajawazito wengi?

Supplementary Question 1

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA: Mheshimiwa Spika, huduma hii tangu izinduliwe ni mwaka mmoja sasa na Mheshimiwa Rais alishatoa maelekezo kampuni nyingine kuweza kujiunga kutoa huduma hii ya usafiri wa dharura kwa mama mjamzito na watoto.

Nini kauli ya Serikali kukamilisha mchakato huu kwa haraka? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Kutokana na huduma hii kupatikana hasa maeneo ya mjini; je, Serikali imejipangaje kutoa elimu na matangazo ya kutosha kwa maeneo ya vijijini kuhusu huduma hii ya bure ya usafiri wa dharura wa mama mjamzito na mtoto? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Answer

WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Santiel, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba huduma hii toka imezinduliwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni karibia mwaka sasa, na maagizo yake yalikuwa mawili; moja, kuhakikisha tunapeleka nchi nzima. Hivi tunavyoongea, tumeshapeleka nchi nzima kasoro mikoa mitatu na kufikia tarehe 22/9/2023 tutakuwa tumewasha nchi nzima.

Mheshimiwa Spika, la pili, lilikuwa hili la kutoa wito kwa wadau wengine kuendelea kuungana na Serikali katika kuhakikisha mfumo huu unafanya kazi. Wadau wameendelea na mazungumzo na Serikali lakini waliopo wameendelea kuongeza fedha na ndiyo ambayo imetupa uwezo wa kuendelea kusambaza huduma hii maeneo mengine ya nchi.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, ni kweli kwamba huduma hii ni ngeni kwa baadhi ya maeneo na kwa hiyo, kutambulika kwake hakuwezi kwenda kwa mara moja. Tunachokifanya, kila tukipeleka mahali, tunaanza kutoa elimu kwa watendaji na hasa wale wa huduma za afya.

Mheshimiwa Spika, huduma hii inasimamiwa kwa pamoja kati yetu Wizara ya Habari kama watoa teknolojia lakini Wizara ya Afya na TAMISEMI ambao kwa kweli wanafanya kazi nzuri, na idadi inaendelea kuongezeka siku hadi siku. Tunaamini tukishirikiana na Waheshimiwa Wabunge na hasa Wabunge wa Viti Maalum kupeleka hii elimu kwenye maeneo yetu ili akina mama watumie huduma hii kuokoa maisha ya mama na mtoto, itasaidia uelewa lakini pia itaongeza watumiaji wa huduma hii. (Makofi)

Name

Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kuhimiza mashirika mengine ya simu kujiunga na mpango wa M-Mama kwani umekuwa msaada kwa wajawazito wengi?

Supplementary Question 2

MHE. GHATI Z. CHOMETE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Naishukuru Serikali kwa jitihada zake ambazo inazifanya kuhakikisha huduma hii imefika mijini. Swali langu ni kwamba: Je, ni upi mkakati wa kutoa elimu ya kutosha kwa akina mama hasa walioko vijijini ili waweze kujua nini maana ya huduma ya M-mama ili kupunguza vifo vya mama na mtoto hasa kwa maeneo ya vijijini? Ahsante. (Makofi)

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Answer

WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ghati, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza lengo la huduma hii kwa kweli siyo mijini sana, kwa sababu mijini huduma ziko karibu na watu. Lengo letu ni kupeleka vijijini ambako tatizo la upatikanaji wa huduma ni kubwa na hasa pale mama mjamzito au mtoto mchanga anapokosa huduma ya ziada baada ya kusaidiwa kwenye zahanati. Kwa hiyo, lengo letu ni kuwafikia walioko vijijini. Tukipeleka kwenye mkoa, tunataka iende vijijini ambako ndiko mahitaji yalipo.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutoa elimu, lakini kama nilivyosema wakati najibu maswali ya nyongeza, nawaomba Wabunge wa Viti Maalum, tushirikiane tuzungumze tuone namna ya kuifikisha elimu hii kwa akina mama kwenye maeneo yetu ili waweze kuitumia huduma hii kwa sababu ipo, ni bure na inapatikana masaa 24 na inaokoa maisha ya mama na mtoto. (Makofi)