Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. CHARLES M. KAJEGE aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga skimu za umwagiliaji Kata za Kisorya, Igundu, Kwiramba, Namuhura, Butimba na Kasuguti - Mwibara?

Supplementary Question 1

MHE. CHARLES M. KAJEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwanza sikubaliani na majibu ya Serikali kwa sababu kila siku wanajipanga, wanajipanga; wanafanya utafiti, wanafanya utafiti; sikubaliana nayo, lakini nina swali moja la nyongeza. Kwa vile Jimbo la Mwibara linakabiliwa na upungufu wa chakula na mojawapo ya sababu ikiwa ni ukosefu wa skimu za umwagiliaji maji: Je, ni lini Serikali itaanza tena mpango wa kupeleka chakula cha msaada katika Jimbo la Mwibara? Ahsante.

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Serikali inaendelea kufanya kazi kulingana na mipango kama nilivyosema, katika mwaka wa 2023/2024 kuna fedha nyingi zimetengwa kwa ajili ya skimu za umwagiliaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na changamoto ya chakula katika Jimbo la Mwibara, utaratibu ni kwamba pale kunapokuwa na uhitaji wa msaada wa chakula katika maeneo husika, naomba viongozi ikiwemo kupitia Mbunge mweze kuandika barua ya maombi kwa Ofisi ya Waziri Mkuu ili tuweze kuratibu namna ya kupeleka chakula cha msaada katika maeneo husika ili kufidia au kupunguza nakisi ya chakula na adha kwa wananchi katika jimbo lake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Mbunge ashirikiane na viongozi wengine ili kuandika barua na kupata maelekezo kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. CHARLES M. KAJEGE aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga skimu za umwagiliaji Kata za Kisorya, Igundu, Kwiramba, Namuhura, Butimba na Kasuguti - Mwibara?

Supplementary Question 2

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi ili niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Serikali mwaka juzi 2021 ilitenga shilingi milioni 100 kupeleka Skimu ya Lwafi – Katangoro, lakini mpaka sasa hakuna tija yoyote imeonekana kwenye hiyo fedha: Ni upi mkakati wa Serikali wa kuongeza fedha ili kumaliza skimu hiyo na ianze kufanya kazi?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama nilivyosema kwenye jibu la msingi, tayari katika mpango wa mwaka wa fedha huu tunaoenda nao, fedha nyingi zimewekwa kwa ajili ya kukamilisha skimu mbalimbali za miradi ambayo ni mipya na inayoendelea. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge awe na imani kwamba sasa huu mradi utaenda kukamilishwa kwa sababu tayari fedha zimetengwa katika mwaka huu wa 2023/2024 ili kutekeleza pamoja na skimu nyingine ikiwemo na hiyo skimu ya kwa Mheshimiwa Aida Khenani, nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. CHARLES M. KAJEGE aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga skimu za umwagiliaji Kata za Kisorya, Igundu, Kwiramba, Namuhura, Butimba na Kasuguti - Mwibara?

Supplementary Question 3

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Skimu za umwagiliaji wa maeneo ya chai kwenye Tarafa ya Igominyi katika Jimbo la Njombe Mjini: Nini kauli ya Serikali kuhusu utekelezaji katika kipindi hichi cha bajeti? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA (K.n.y. WAZIRI WA KILIMO): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Skimu ya Igominyi na maeneo mengine kama alivyosema, ni skimu muhimu sana kwa ajili ya kuhakikisha kilimo cha chai kinaendelea kuchangia katika uchumi wa nchi. Ni nia ya Serikali kuona skimu zote ambazo ziko kwenye mpango wake zinatekelezwa. Kwa hiyo, fedha zitaendelea kupelekwa katika maeneo ambayo yamepangwa kulingana na mpango wa fedha katika mwaka wa fedha huu wa 2023/2024, nakushukuru. (Makofi)

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. CHARLES M. KAJEGE aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga skimu za umwagiliaji Kata za Kisorya, Igundu, Kwiramba, Namuhura, Butimba na Kasuguti - Mwibara?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni, tuna Skimu ya Udimaa na Skimu ya Ngaiti ambazo zimechakaa sana, lakini zipo kwenye bajeti ya mwaka huu: Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa kujenga hizi skimu mbili ambazo nimezitaja? Nashukuru. (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Ni kweli tunajua katika baadhi ya maeneo skimu nyingi zimechakaa, kwa maana ni za muda mrefu. Ndiyo maana kama nilivyosema kwenye jibu la msingi, tayari tumeshaweka fedha kwenye mwaka huu wa 2023/2024. Kwa hiyo, muda wowote tutaanza kutekeleza skimu hizo ikiwemo ya kwa Mheshimiwa Mbunge kule Manyoni ili kuhakikisha skimu hizo zinaboreshwa ili ziweze kutoa faida kwa wakulima na kuweza kuhakikisha kilimo cha kisasa kinaendelea, nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CHARLES M. KAJEGE aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga skimu za umwagiliaji Kata za Kisorya, Igundu, Kwiramba, Namuhura, Butimba na Kasuguti - Mwibara?

Supplementary Question 5

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Naipongeza sana Serikali kwa jitihada zake za kupanga mipango ya umwagiliaji. Kwa kuwa Serikali ndiyo yenye wataalam, wabobezi katika masuala haya ya umwagiliaji.

Je, ni lini Serikali itapanga mipango ya kuwasaidia wakulima kufanya levelling kufikisha maji kwenye mashamba yao badala ya kuwaachia kazi mkulima mmoja mmoja afanye jambo hilo ambapo hawana utaalamu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inge-copy mambo yanayofanyika Egypt. Egypt wanafanyakazi zote mpaka kuwapeleka watu mashambani, kwa sababu ninyi ndio mna kamera, ninyi ndio mna vifaa vya kupimia: Sasa Serikali mna mpango gani wa kushughulikia wakilima ili maji yaende kwa watu wote?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Ni mawazo mazuri kutoka kwa Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali ndiYo yenye dhamana ya kuhakikisha skimu za umwagiliaji na kuhakikisha maji yanaenda katika mashamba na maeneo mbalimbali ambako wananchi wanafanya shughuli za kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mipango ya Serikali tumesema moja ya maeneo ambayo yameongezwa sana fedha ni kwenye maeneo haya ya umwagiliaji. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mipango ya Serikali ni thabiti na itaendelea kutekelezwa kulingana na fedha ambazo tunazipanga na kuhakikisha tunaenda na vipaumbele katika maeneo ambayo kuna mahitaji haya ya skimu za umwagiliaji. Hivyo, tuwaondoe hofu Waheshimiwa Wabunge na wananchi kwamba Serikali itatekeleza miradi yake na mipango yake kwa kadri ambavyo tunapanga kwenye mipango ya kila mwaka wa fedha wa bajeti, nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CHARLES M. KAJEGE aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga skimu za umwagiliaji Kata za Kisorya, Igundu, Kwiramba, Namuhura, Butimba na Kasuguti - Mwibara?

Supplementary Question 6

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Skimu ya Bukangilija na Masela ni lini itaanza kujengwa Wilaya ya Maswa? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema, skimu zote ambazo ziko kwenye mpango na bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024 na pia hata hizo mpya ambazo tunaendelea kuzipata zitawekwa kwenye mipango ya bajeti na hivyo zitajengwa kwa kadri ambavyo tumepangia kwenye mipango yetu ya Serikali pamoja na skimu aliyoitaja Mheshimiwa Mbunge, nayo pia itaweza kufanyiwa kazi kadri ambavyo Serikali itakuwa imejipanga, nakushukuru sana.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. CHARLES M. KAJEGE aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga skimu za umwagiliaji Kata za Kisorya, Igundu, Kwiramba, Namuhura, Butimba na Kasuguti - Mwibara?

Supplementary Question 7

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi ya swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pale Kijiji cha Makangaga, Kata ya Kiranjeranje Jimbo la Kilwa Kusini, kuna skimu ya umwagiliaji ambayo imetelekezwa kwa muda mrefu: Je, Serikali ipo tayari kupeleka wataalamu pale Makangaga ili wakafanye upembuzi yakinifu na hatimaye skimu hii iweze kufufuliwa mara moja?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Serikali itapeleka wataalam waweze kutathmini hiyo skimu na kuona gharama na mahitaji halisi ili iweze kuboreshwa na iweze kutoa tija kwa wakulima wanaotumia skimu hiyo, nakushukuru sana.

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CHARLES M. KAJEGE aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga skimu za umwagiliaji Kata za Kisorya, Igundu, Kwiramba, Namuhura, Butimba na Kasuguti - Mwibara?

Supplementary Question 8

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Mkoa wa Rukwa, Wilaya ya Kalambo, Tarafa ya Mwimbi kuna mito mingi sana ya kutosha: Je, Serikali ina mpango gani wa kuendeleza kilimo cha umwagiliaji katika tarafa hiyo? Ahsante (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA (K.n.y. WAZIRI WA KILIMO): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Azma ya Serikali ni kutumia vyanzo vyote vya maji vilivyopo, ikiwemo mito ambayo ni muhimu sana kwa ajili ya kuhakikisha skimu za umwagiliaji zinafanya kazi. Kwa hiyo, katika maeneo ambayo tutaendelea pia kuyafanyia kazi ni mito hiyo iliyopo katika Jimbo la Kalambo ili kuhakikisha nayo inatumika kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji katika eneo husika ambalo Mheshimiwa Mbunge amelitaja, nakushukuru sana.

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CHARLES M. KAJEGE aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga skimu za umwagiliaji Kata za Kisorya, Igundu, Kwiramba, Namuhura, Butimba na Kasuguti - Mwibara?

Supplementary Question 9

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa Serikali ilishachukua vipimo vya kujenga Bwawa la Iyongoma na bwawa hili ni muhimu sana kwa ajili ya kumwagilia Skimu ya Ndungu ambayo kwa muda mrefu imekuwa na matatizo: Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga bwawa hili?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kama ambavyo yeye mwenyewe amesema kwamba tayari kuna mipango inaendelea kuhakikisha tunalijenga hilo bwawa na wataalamu kama walishakuja kuangalia. Moja ya maeneo ambayo tutaangalia ni haya ambayo tayari yameshafanyiwa usanifu yakinifu ili yaweze kuanza kutekelezwa kadiri ambavyo tumepanga kwenye bajeti zetu za Wizara na kuhakikisha pia kama kuna miradi mingine ambayo itapelekea kukamilisha mabwawa haya nayo pia tutaangalia. Kwa hiyo, hili bwawa nalo litawekwa katika kipaumbele katika mipango ya Wizara, nakushukuru sana.