Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Janeth Elias Mahawanga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH E. MAHAWANGA aliuliza:- Je, nini mpango wa kuhakikisha Majukwaa ya Kuwezesha Wanawake Kiuchumi yanaleta tija kwenye mikopo ya asilimia 10 ya Halmashauri?

Supplementary Question 1

MHE. JANETH E. MAHAWANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali lakini, nina maswali madogo mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; Vikundi vingi vya Majukwaa bado havina uelewa wa pamoja wa lengo mahsusi la uanzishaji wa majukwaa haya. Sasa nini kauli ya Serikali kuhusu hili?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; ni utaratibu upi unatumika kahakikisha waratibu wa majukwaa haya wanashuka kutoa elimu ya mwongozo wa uratibu wa majukwaa haya katika ngazi ya kata na mitaa?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tunaendelea kutoa mafunzo kwa lengo la kukuza uelewa kwa majukwaa haya ya kuendeleza uchumi kwa ajili ya wanawake. Napenda kutoa rai kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii, kuhakikisha kwamba wanatoa mafunzo kwa lengo la kuwaelewesha wananchi ni nini cha kufanya katika majukwaa haya.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Wizara yangu inafuatilia na kufanya tathmini mbalimbali katika vikundi vyote vya majukwaa ya wanawake kiuchumi na kuhakikisha kwamba tunawatembelea kila baada ya robo ya mwaka wa fedha kuhakikisha vikundi vile vinafanya kazi vizuri na kuhakikisha wanafuata sera, sheria, kanuni na miongozo yote ambayo tumeipanga, ahsante. (Makofi)