Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza:- Je, lini ujenzi wa njia nne kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Kilwa kipande cha Mbagala Rangi Tatu hadi Kongowe utakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Swali langu la kwanza la nyongeza, napenda kujua, ni lini Serikali itakarabati kipande cha barabara toka Somanga hadi Nangurukuru hadi Mbwemkuru ambacho kimechakaa sana?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; miaka ya hivi karibuni Serikali ilitanua barabara za mikoa na barabara kuu katika Mkoa wa Lindi, lakini haijaweza kulipa fidia hadi wakati huu. Ni lini Serikali italipa fidia kwa wananchi walio kando kando ya barabara hizo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii kuu ya Kusini Somanga - Nangurukuru hadi Mbwenkulu hadi Mnazi Mmoja imechoka. Hii barabara sasa hivi inapitisha mizigo mizito sana tofauti na ilivyokuwa awali. Kwa hatua za haraka ni kukarabati yale maeneo yote ambayo yamechakaa sana ili kuhakikisha kwamba hatukwamishi magari. Mpango mkubwa wa sasa hivi, Serikali inatafuta fedha ili kuifanyia ukarabati wa barabara yote kuendana sasa na uzito wa magari ambayo yanapita kwenye hiyo barabara ya Kusini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la pili la Mheshimiwa Mbunge, ni kweli kwamba tulibadilisha sheria kwa maana ya kuongeza upana wa barabara. Wizara ya Ujenzi inachofanya sasa hivi ni kufanya tathmini kwa barabara zote. Kwa kuanzia, pale ambapo tunaanza ujenzi, tunalipa, lakini tunataka tupate gharama nzima kwa barabara zote ambazo zimeongezeka kwa ajili ya kutafuta fedha kuwafidia wananchi ambao barabara imewafuata, na siyo kwa Lindi tu, ni kwa sehemu kubwa ya nchi, ahsante. (Makofi)

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza:- Je, lini ujenzi wa njia nne kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Kilwa kipande cha Mbagala Rangi Tatu hadi Kongowe utakamilika?

Supplementary Question 2

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa kipande hicho cha Mbagala Rangi Tatu hadi Kongowe kinakuwa na msongamano mkubwa wa magari kiasi kwamba ni foleni masaa yote: Je, Serikali ina mpango gani wa muda mfupi kuhakikisha wanapanua ile barabara ili magari yaweze kupita na kuepukana na foleni?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema, tunatambua changamoto ambayo ipo kwenye hii barabara na ndiyo maana tumeiweka kwenye mpango. Serikali itakachofanya ni kuhakikisha kwamba inaanza haraka ujenzi wa kipande hiki ili kuondoa adha ambayo inawakuta wananchi ambao wanatumia hii barabara ikiwa ni pamoja na kupunguza msongamano kwa maana ya kupunguza muda mwingi ambao unatumika katika kipande hiki. Ndiyo maana tayari tumeshaingiza kwenye mpango. Kwa hiyo, cha msingi ni kuanza haraka ujenzi wa barabara hii kwa hizo njia nne, ahsante.

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza:- Je, lini ujenzi wa njia nne kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Kilwa kipande cha Mbagala Rangi Tatu hadi Kongowe utakamilika?

Supplementary Question 3

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Kwa kuwa barabara ya kuingia Singida Mjini, almaarufu kama barabara ya Kibaoni, imekuwa finyu: Ni lini Serikali itaitanua barabara hiyo na kuwa njia nne?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, kinachofanyika ni study ya miji yote ambayo inaendelea kukua na Singida ikiwa mojawapo. Kwa hiyo, tunaendelea kufanya study kwenye miji mbalimbali ambayo tunaona kunahitajika kupanuliwa kwa barabara hasa zinazoingia kwenye miji. Hii ni pamoja na miji kama hii ya Dodoma, Singida ambayo tunaona kadiri kunapokucha magari yanaongezeka.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunaendelea na usanifu wa hizo barabara ili tuone kama zinahitajika njia nne, ama njia sita, ahsante. (Makofi)

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza:- Je, lini ujenzi wa njia nne kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Kilwa kipande cha Mbagala Rangi Tatu hadi Kongowe utakamilika?

Supplementary Question 4

MHE. CHARLES M. KAJEGE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kuna wananchi wengi wa Mwibara uliopisha mradi wa barabara kati ya Bulamba na Kisorya imechukua muda mrefu kweli bila kulipwa. Sasa naomba commitment ya Serikali: Ni lini wananchi hawa watalipwa fidia zao?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu wakati najibu muuliza swali la msingi wananchi ambao bado hawafidiwa ni wale ambao wako kilomita I mean wako mita 7.5 kutoka kwenye barabara na ndiyo maana nilisema tunafanya tathimini ya nchi nzima. Wamepewa kazi hiyo wale Mameneja wa Mikoa kuangalia na kufanya tathimini ili tupate gharama halisi ili wakati Serikali inalipa basi iweze kujua gharama halisi ya fidia ambayo inatakiwa kulipwa ikiwa ni pamoja na wananchi wa Mwibara ambao wamepisha barabara hiyo ya Kisorya ya Bulamba, ahsante. (Makofi)