Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha mradi wa Umwagiliaji wa Kisawasawa – Kilombero?

Supplementary Question 1

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Naishukuru Serikali kwa kututengea fedha kwa ajili ya mradi huu. Kwa kuwa Mkurugenzi wa Umwagiliaji aliahidi kwenda yeye mwenyewe, nataka kujua: Je, Mheshimiwa Naibu Waziri, atamwelekeza lini aende kutembelea mwenyewe mradi huu wa Kisawasawa kwa sababu aliahidi wakati wa Bunge hapa?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Kwa kuwa Kijiji cha Lungongole Tarafa ya Ifakara nako wana eneo linalofaa kwa umwagiliaji hasa wakati wa kiangazi: Je, ukimwagiza aende Kisawasawa, uko tayari kumwagiza aende na Lungongole ili tathmini pia ianze? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nitamwelekeza Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kufika Kilombero mapema kadiri iwezekanavyo. Kuhusu eneo lake la pili, bahati nzuri tulisaini mkataba hapa wa kuajiri Washauri Waelekezi kwa ajili ya kuyapitia mabonde yote nchini likiwemo Bonde la Ifakara - Idete. Kwa hiyo, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari tunayo Kampuni pale ya Clemence na Vibe International Company Limited wako tayari na wako 13% ya kufanya usanifu katika eneo hilo. Kwa hiyo, mradi huo pia utajumuishwa katika skimu ambayo itatengenezwa hapo katika Bonde la Ifakara.