Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kavejuru Eliadory Felix

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha Forodha cha Manyovu?

Supplementary Question 1

MHE. KAVEJURU E. FELIX: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali. Je, lini Serikali italipa fidia kwa wananchi wanaopisha ujenzi wa kituo hicho cha forodha? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri wa Wizara ya Fedha na Mipango yupo tayari kuambatana nami twende Manyovu baada ya Bunge hili ili akaongee na wananchi hao wanaopisha ujenzi wa kituo hicho cha forodha? (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Felix kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze hilo la pili. Niko tayari kuambatana naye kwenda sehemu husika na kuongea na wananchi kule. Swali lake la kwanza, Serikali iko katika hatua za uchambuzi wa fidia hiyo ya wananchi. Namwomba tu Mheshimiwa Mbunge awe na subira. Mara tu taratibu zitakapokamilika, basi wananchi watapata haki yao.