Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Mulungu Jimbo la Muhambwe?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, Ahsante. Nimshukuru Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri. Pamoja na majibu yake nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza. Katika Wilaya ya Buhigwe Kata ya Mkatanga, wananchi wa Kijiji cha Kitambuka waliomba kujengewa kituo cha afya na ombi hilo walilitoa mbele ya Makamau wa Rais Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango, na tayari wanayo matofali.

Je, Serikali iko tayari kutoa pesa ili wananchi waweze kujengewa kituo hicho? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu DC, Kata ya Kagera Nkanda iko umbali mrefu sana kutoka yaliko Makao Mkauu ya Halmasahuri ya Kasulu DC, ambapo ni kilometa 77 kutoka Makao Makuu.

Je, Serikali iko tayari kujenga kituo cha afya katika Kata ya Kagera Nkanda?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nijibu maswali yote mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Genzabuke. Kuhusu Kata hizi za Mkatanga pamoja na Kagera Nkanda nichukue nafasi hii kumwelekeza Mgamga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma kuweza kutembelea katika Kata hizi na Kufanya tathimini ili kuona kama vigezo vile vya kuwa na vituo vya afya vinatimia. Kama vigezo vile vinatimia basi Mganga Mkuu awasilishe taarifa il;e katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili tuweze kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo hivi.

Mheshimiwa Spika, lakini Mheshimiwa Genzabuke amekuwa akifuatilia sana Kituo hiki cha Afya cha Kagera Nkanda muda mrefu na tutakaa nae kuona ni namna gani katika mwaka wa fedha ujao tunaweza tukatenga fedha.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Mulungu Jimbo la Muhambwe?

Supplementary Question 2

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa kuwa Mahongole wana kituo cha afya;

Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa kituo cha Afya Kata ya Mahongole?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, Serikali itamalizia Kituo cha Afya cha Mahongore kadri ya upatikanaji wa fedha.

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Mulungu Jimbo la Muhambwe?

Supplementary Question 3

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Kituo cha Afya cha Ipogolo ni kati ya vituo vikongwe vya afya na vinahudumia zaidi ya wanawake 600 kwa mwezi lakini hakina combined ward.

Je, Serikali inaweza kutusaidia kutujengea combined ward katika kituo hiki ili kupunguza msongamano?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, tutatuma timu kwenda Halmasahuri ya Manispaa ya Iringa kwa ajili ya kufanya tathimini ya kituo hiki cha afya cha Ipogolo na kuona kama eneo linaruhusu kuweza kujenga maeneo haya ambayo Mheshimiwa Mbunge ameomba na kama inaruhusu tutaweka katika mipango yetu ya kutafuta fedha ili kuweza kujenga kituo hiki cha afya ambacho ni kongwe.

Name

Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Mulungu Jimbo la Muhambwe?

Supplementary Question 4

MHE TWAHA A. MPEMBENWE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza. Kwenye kata ya Salale Kijiji cha Nyamisati tuna shida kubwa sana ya kituo cha afya ukizingatia zahanati ya pale inahudumia wilaya mbiliā€¦

SPIKA: Mheshimiwa Twaha, uliza swali.

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE: Mheshimiwa Spika, je, lini Serikali mtatujengea kituo cha afya pale?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, Serikali ina vigezo vyake vya kuanza kujenga vituo vya afya. Hivyo, basi tutauma timu kwa ajili ya kwenda kule katika Kijiji cha Nyamiisati, kata ya Salale, Jimboni Kibiti kuweza kufanya tathimini na kuona kama vigezo vile vimefikiwa vya kuweza kujenga kituo hiki vya afya.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Mulungu Jimbo la Muhambwe?

Supplementary Question 5

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza;

Je, ni lini Serikali itajenga kituo cha Afya Kata ya Sawida wilaya ya Itilima?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, Serikali itajenga kituo hicho cha afya baada ya kufanya tathimini ya kuona uhitaji ulioko pale lakini vile vile kadri ya upatikanaji wa fedha; na tutatenga katika bajeti za miaka ya fedha inayofuata.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Mulungu Jimbo la Muhambwe?

Supplementary Question 6

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Spika, ahsante nami kwa nunipa swali la nyongeza. Kituo cha afya cha Misha katika kata 29 za Tabora kimekamilika lakini bado hakina vifaa vya Afya vya kutosha;

Je, ni lini serikali itapeleka vifaa hivyo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwakasaka kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya hiki Misha kipo pembezoni mwa Manispaa ya Tabora na tayari katika mwaka wa fedha 2022/2023 ambao tunaenda kuumaliza Serikali ilikuwa imetenga fedha kwa ajili ya ununuzi wa vifaatiba katika kituo hiki cha afya, nitakaa na Mheshimiwa Mwakasaka ili tuweze kupitia hivi na kuona tunapeleka hivi vifaa tiba kwa haraka sana.

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Mulungu Jimbo la Muhambwe?

Supplementary Question 7

MHE. CHARLES M. KAJEGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ya Mheshimiwa Rais ya kujenga Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Bunda katika Jimbo la Mwibara?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, tutakaa na wenzetu wa Wizara ya Fedha na kuona, maana yake Ofisi ya Rais, TAMISEMI imefanya compilation ya ahadi zote za viongozi wetu Wakuu wa Nchi na kuziwasilisha Wizara ya Fedha na kuona namna gani tutapata fedha kwa ajili ya utekelezaji wa ahadi hizi. Hivyo basi, nimtoe mashaka Mheshimiwa Kajege kwamba baada ya kukaa na wenzetu wa Wizara ya Fedha na kuona ni namna gani Serikali itapata fedha hizi, tutaanza ujenzi huu wa Hospitali hii.

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Mulungu Jimbo la Muhambwe?

Supplementary Question 8

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kituo cha Afya Mtina kilitengewa milioni 250 katika bajeti tunayoendelea nayo ili kujenga jengo la akinamama na watoto. Je, ni lini pesa hiyo itaenda?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nitakaa na Mheshimiwa Mpakate ili kuona katika mwaka wa fedha huu 2023/2024 tunaoenda kuanza kutekeleza kama Kituo hiki cha Afya cha Mtina kimetengewa fedha na kama hakijatengewa fedha, basi tutaangalia ni namna gani tunaweza tukakiweka katika mipango ya mwaka wa fedha 2024/2025.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Mulungu Jimbo la Muhambwe?

Supplementary Question 9

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipatia nafasi ya swali la nyongeza. Je, ni nini mpango wa Serikali wa kujenga kituo cha afya katika Kata ya Likawage, Jimbo la Kilwa Kusini, kata ambayo iko mbali kutoka sehemu ambayo huduma ya afya inapatikana?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, tutatuma timu kwenda katika Kata ya Likawage kufanya tathmini na kuona kama vile vigezo vya idadi ya watu na kadhalika vimefikiwa eneo walilolitenga wao katika maeneo hayo na kama vigezo vile vimefikiwa, basi tutaweka katika mipango yetu ya kutafuta fedha.

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Mulungu Jimbo la Muhambwe?

Supplementary Question 10

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Nataka kujua tu, ni lini Serikali italeta vifaa tiba katika vituo vyetu vya afya na hospitali ya wilaya?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nitakaa na Mheshimiwa Sima kuweza kupitia katika fedha iliyokuwa imetengwa ya ununuzi wa vifaatiba kwa mwaka wa fedha 2022/2023, kuona Halmashauri ya Manispaa ya Singida imetengewa kiasi gani na kama ilikuwa haijatengewa tutaangalia katika mwaka wa fedha huu tunaoenda kuanza kuutekeleza wa 2023/2024 ili tuweze kuona namna gani fedha hiyo inaenda kwa haraka kupata vifaa tiba hivyo.