Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza:- Je, Serikali inatoa tamko gani kwa mabasi yasiyoingia stendi na ambayo hushusha abiria nje ya stendi?

Supplementary Question 1

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Anachokieleza Naibu Waziri uhalisia kule si kweli kwa sababu mabasi yanayotoka masafa marefu unakuta yana abiria lakini yanasingizia hayana abiria matokeo yake yanawaacha wananchi juu kwa juu. Kwa mfano, pale Igunga maeneo ya mnadani wananchi wanafika wanashushwa tu wanaachwa wanaanza kuhangaika kutafuta bajaji na bodaboda kurudi Mjini.

Je, ipi ni kauli ya Serikali katika hili ili kuepusha adha kwa wananchi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, moja ya mwongozo wa Serikali ni kuhakikisha Halmashauri zetu zinakusanya mapato na Halmashauri nyingi vyanzo vyetu vya mapato ni pamoja na hizi stendi za mabasi lakini mabasi yanatumia kigezo cha kusema hawana abiria lengo wasiingie Halmashauri ili tusipate mapato. Pia naomba kauli ya Serikali katika hili, ahsante. (Makofi)

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Nicholaus Ngassa, Mbunge wa Igunga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama nilivyokwisha kujibu kwenye jibu langu la msingi kwamba Sheria ya Usalama Barabarani, lakini pamoja na wadau, tulikaa na wadau mwaka jana tarehe 24, Mwezi wa Nne 2022, wadau wote wa usafirishaji, tulikubaliana kwamba ili kupunguza gharama kwa abiria ni pamoja na mabasi haya ambayo hayana abiria wa kushusha ndani wala hakuna anayepakia yasiingie ili kupunguza muda wa mabasi hayo kwenda kwa sababu wanasafiri umbali mrefu.

Mheshimiwa Spika, kauli ya Serikali kama kuna basi lolote ambalo limeshusha abiria njiani na wakati eneo hilo kuna kituo cha mabasi kwa mujibu wa Sheria ya Usalama Barabarani Kifungu cha 50 (1) na Sura ya 168 kimeelekeza wazi kwamba dereva huo lazima achukuliwe hatua za kisheria. Kwa hiyo, kwa kushirikiana na jeshi la polisi tutaendelea kusimamia jambo hili ili mabasi haya yafuate utaratibu huu kama ambavyo tulikubaliana.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, kuhusu suala la mapato katika Halmashauri zetu hususan katika vituo hivyi vya mabasi, ni kwamba siyo kila basi kama nilivyokwisha kusema litaingia kwenye kituo, lakini kwa mabasi yale ambayo yataingia kwa masafa mafupi yana wajibu wa kulipa ushuru katika maeneo hayo. Ahsante.

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza:- Je, Serikali inatoa tamko gani kwa mabasi yasiyoingia stendi na ambayo hushusha abiria nje ya stendi?

Supplementary Question 2

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Ninataka kufahamu Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa stendi mpya ya mabasi Bukoba Mjini? Ahsante. (Makofi)

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Neema, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, suala la ujenzi wa stendi katika Mkoa wa Kagera, Bukoba tutawasilina na wenzetu TAMISEMI ambao wanasimamia jambo hili na naamini katika bajeti yao mwaka huu huenda wamepanga fedha kwa ajili ya ujenzi wa stendi hii. Ahsante.