Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA S. MOLLEL (K.n.y. MHE. SABREENA H. SUNGURA) aliuliza:- Kumekuwa na tatizo kubwa la mgawanyo wa fedha za TASAF ambapo wananchi wengi wasio na uwezo, wamekuwa hawapati fedha hizo. Je, Serikali imejipangaje kutatua kero hii kwa wananchi ambao hawapati fedha hizo hususan katika Mkoa wa Kigoma?

Supplementary Question 1

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri na nina maswali mawili ya nyongeza.
Moja, kwa kuwa zoezi hili limeleta malalamiko na kwa kuwa baadhi ya waliochangia utaratibu huu kwenda vibaya na kuandikisha kaya ambazo hazikustahili kupata mgao huu wa TASAF; je, Serikali inawachukulia hatua gani watumishi ambao wamefanya makosa haya na kuwakosesha haki yao ya msingi wale waliostahili kupata mgawanyo huu wa TASAF?
Swali la pili, kwa kuwa baadhi ya walionufaika wanadai kwamba kiasi hiki ni kidogo; je, Serikali haioni kwamba kuna haja ya kuongeza kiasi cha fedha ili kiwanufaishe walengwa? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kutambua kwamba kumetokea udanganyifu kama nilivyosema katika jibu langu la msingi na kwamba takribani kaya 25,446 ni zile ambazo hazikuwa zinakidhi vigezo vilivyoelezwa vya kiwango cha umaskini, lakini wakawekwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali tumechukua hatua mbalimbali za kinidhamu hasa kwa watumishi wale ambao ni wa Halmashauri, kwa sababu kwa kiasi kikubwa zoezi hili linafanywa kwa ushirikiano kati ya Wizara hii na Wizara ya TAMISEMI kwa maana ya watumishi wa Halmashauri.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia kwa wale viongozi wa kuchaguliwa, tutaona hatua nzuri zinazofaa kwao, kwa sababu udanganyifu huu umefanywa mahali pengine ni kwa makusudi na mahali pengine siyo kwa makusudi, ni kwa kukosa vielelezo vya kutosha juu ya hao wanaotakiwa kunufaika na utaratibu huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kiasi hiki anachodai Mheshimiwa Mbunge kwamba ni kidogo na je, hatuoni haja ya kuongeza? Msingi wa kiwango hiki ni kwamba lengo letu ni kuzisaidia, not permanently kaya hizi maskini ili ziweze ku-gain mahali ambapo sasa zinaweza zikajiendesha zenyewe. Vigezo vinavyotumika kama nilivyosema, kwanza kabisa unaangalia kama familia hiyo ina watoto, lakini cha pili, ni kwamba je, hata kama ina watoto je, watoto hao wanaenda shule au wanaenda kliniki?
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana katika mpango huu, baadhi ya maeneo wameamua kuzisaidia hizi familia kuwalipia CHF yaani Mfuko wa Afya ya Jamii ili waweze kuwa na uhakika wa kupata matibabu. Hili tunalitia moyo sana, kwa sababu moja kati ya vitu vinavyoumiza familia masikini ni kutokupata matibabu stahiki. Sasa hili la shule na lishe ni jambo ambalo tumeweka kama vigezo. Sasa kama haya nia yake ni kuikuza familia itoke pale na ifike mahali ambapo itajitegemea, ikiwa ni pamoja na shughuli nyingine za kiuchumi, basi fedha hizi kwa kiwango tulichopanga, tumezingatia hali ya kutosha kwake na hivyo watajenga uwezo kidogo kidogo na baadaye wataweza kujitegemea.
Mheshimiwa Naibu Spika, natoa wito tu kwa watu wanaonufaika na mpango huu kuwa na dhamira ya kujenga kujitegemea na siyo kuendelea kusaidiwa ili baada ya programu hii kuisha, wawe wameshajenga huo uwezo.

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. AMINA S. MOLLEL (K.n.y. MHE. SABREENA H. SUNGURA) aliuliza:- Kumekuwa na tatizo kubwa la mgawanyo wa fedha za TASAF ambapo wananchi wengi wasio na uwezo, wamekuwa hawapati fedha hizo. Je, Serikali imejipangaje kutatua kero hii kwa wananchi ambao hawapati fedha hizo hususan katika Mkoa wa Kigoma?

Supplementary Question 2

MHE. DANIEL N. NSANZUGWAKO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Naomba niulize swali moja dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, muuliza swali msingi wake ulikuwa ni udanganyifu mkubwa uliotokea katika Mkoa wa Kigoma hasa katika Mfuko huu wa TASAF, sasa nilikuwa naomba Waziri anipe comfort hapa kwamba je, haoni kwamba kuna haja ya kufanya uhakiki maalum kwa Mkoa wa Kigoma kama ambavyo Mheshimiwa Sabreena alijielekeza kwenye swali lake?
Mheshimiwa Naibu Spika, udanganyifu kwa Mkoa wa Kigoma ulikuwa ni mkubwa sana katika Wilaya ya Kasulu na Kibondo katika Mfuko huu wa TASAF.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba ni kweli kwamba msingi wa swali ilikuwa hasa ni kujua udanganyifu uliotekea Kigoma; na tunapojibu swali hapa kwa sababu linagusa karibu programu hii ambayo ni ya Wilaya ambapo tumeanza kwa Tanzania Bara karibu Wilaya 151, ni dhahiri kwamba tungepata maswali mengi na ndiyo maana tumekuja na jibu la jumla kwamba yale yaliyotokea Kigoma yametokea pia na maeneo mengine; na udanganyifu umekuwepo na hatua hizo hizo zitakazochukuliwa Kigoma ndizo zitakazochukuliwa na huko sehemu nyingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa taarifa tu ni kwamba kwa utafiti tuliofanya Kigoma ni kwamba kaya ambazo zinaonekana zimefanyiwa udanganyifu ni takribani kaya 1,020 na hizo tumeshaziondoa kwenye orodha na wale watumishi waliofanya udanganyifu huo wanaendelea kuchukuliwa hatua, lakini pia kuna wale wengine ambao ni wa kuchaguliwa maana unavyojua lile zoezi linashirikisha wale Wenyeviti wa Vijiji pale, Mtaa na nini na nini. Sasa unamkuta Mwenyekiti wa Kijiji au Mwenyekiti wa Kitongoji amemweka mke wake au unamkuta mwingine ni mtumishi, ni mwalimu naye yupo kwenye mpango huu. Hao wote tumewaondoa.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kama ni kuchua hatua za kinidhamu dhidi yao pamoja na ile benefit of doubt ya watu kutokufahamu; wengine wamefanya siyo kwa makusudi, lakini kwa wale waliofanya makusudi kusema ukweli hatua zitachukuliwa na kazi hiyo kwa maana ya Mkoa wa Kigoma, tumeifanya vizuri labda tu hapa tuendelee kuchukua hatua ili jambo hili lisijirudie tena. (Makofi)
NAIBU SPIKA: Tunaendelea. Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mheshimiwa Hawa Abdulrahman Ghasia, Mbunge wa Mtwara Vijijini, swali lake litaulizwa na Mheshimiwa Abdallah Chikota.