Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya kupandisha hadhi Mji wa Magugu?

Supplementary Question 1

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mamlaka ya Mji mdogo wa Katesh ni ya muda mrefu na Mji wa Katesh umepanuka sana. Je, Serikali lini itachukua hatua ya kuanzisha Mamlaka kamili ya Mji wa Katesh?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hhayuma, Serikali kwa sasa bado inaweka kipaumbele katika kumalizia ujenzi wa miundombinu kwenye maeneo ambayo ni mapya na maeneo yale ambapo Halmashauri zilihamia kwenye maeneo yale ya kiutawala na pale Serikali itakapomaliza ujenzi wa miundombinu hii muhimu, tutaanza kuangalia tena namna ya kuweza kuanza kupandisha hadhi maeneo mengine ya Mamlaka za Miji.

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya kupandisha hadhi Mji wa Magugu?

Supplementary Question 2

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Mheshimiwa Naibu Waziri Mji mdogo wa Kibaya na Matui imekuwa ipo kwa muda mrefu sana, sasa imewaacha wale siyo wenyeviti siyo Wenyeviti wa Mitaa wame-hang tu kwa muda mrefu.

Je, ni lini Serikali italeta mpango ili suala hili likae vizuri? Ahsante sana.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema hapo awali Serikali kwa sasa imeweka kipaumbele katika umaliziaji wa miundombinu na ujenzi wa miundombinu mingine katika maeneo mapya ya kiutawala ambayo yalianzishwa hivi karibuni na yale maeneo ambapo Halmashauri zilihamia kwenye maeneo hayo ya utawala. Pale ambapo zoezi hili litakamilika la ujenzi wa miundombinu hii tutaanza kuangalia namna gani ya kuanza kupandisha hadhi Miji hii, ikiwemo Kibaya na Matui kule Kiteto.

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya kupandisha hadhi Mji wa Magugu?

Supplementary Question 3

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, mchakato wa kupandisha hadhi Mji wa Kibaha kuwa Manispaa ya Kibaha umefikia hatua gani?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hawa Mchafu Chakoma la kupandisha hadhi Mji wa Kibaha kuwa Manispaa. Ombi hili la Manispaa ya Kibaha la kukidhi vigezo, kwanza walipewa vigezo vya kuweza kufikia ili waweze kupandishwa hadhi ikiwemo idadi ya watu. Waliwasilisha Ofisi ya Rais, TAMISEMI Aprili mwaka huu lile ombi lao la kuweza kupandishwa hadhi na tayari lipo kwenye timu ambayo wanaiangalia kuona kama vigezo vile vimekidhi kwa ajili ya kupandishwa hadhi na kuwa Manispaa ya Kibaha.