Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa soko la mnada wa ng’ombe wa Murusagamba?

Supplementary Question 1

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru sana, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwanza nashukuru Serikali, majibu ni mazuri sana. Sasa swali la kwanza, kwa kuwa ujenzi umefanyika kwa muda mrefu na sasa kuna cracks nyingi zimetokea pale. Je, Wizara iko tayari kwenda kufanya ukarabati eneo lile ili uzinduzi utakapofanyika eneo lile liwe linafaa kwa ajili ya mnada, swali la kwanza.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, naomba kukuuliza Mheshimiwa Waziri uko tayari kuambatana na mimi baada ya Bunge hili twende pale Ngara, Murusagamba tukazindue huo mnada? Ahsante sana. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana; cha kwanza nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba pamoja na kwamba mnada umekamilika na hayo mapungufu machache ambayo Mheshimiwa Mbunge ameainisha tutayarekebisha kabla ya kuzindua na mimi niko tayari kwenda mara baada ya Bunge lako tukufu kuahirishwa, ahsante sana.