Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati zahanati 18 katika Tarafa za Laela, Mpui, Mtowisa na Kipeta?

Supplementary Question 1

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na mkakati wa jumla wa Serikali wa kukarabati zahanati 18 ndani ya Jimbo la Kwela lakini katika Kijiji cha Kavifuti, Kata ya Miangalua na Kijiji cha Kiandaigonda zahanati zake ni kama magofu kabisa zimechakaa. Je, Serikali wana mpango gani wa dharura kunusuru walau wananchi wapate huduma sehemu iliyo salama?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; wananchi wa Kijiji cha Kapewa, Mtetezi, Mumba pamoja na Mtapenda wametumia nguvu kubwa kujenga zahanati ambayo imebaki fedha kidogo kumalizia. Je, Serikali haioni haja ya kupeleka fedha ili wananchi wapate huduma? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Mbunge, kwa kuwa anafanya kazi nzuri sana kuwasaidia wananchi wa Jimbo lake la Kwela hususan katika kufatilia haya masuala ya zahanati. Bahati nzuri maeneo haya ambayo Mheshimiwa Mbunge, anayataja hata mimi binafsi nimewahi kufika na nimeona hiyo changamoto na Ofisi ya Rais, TAMISEMI ilishaahidi kuyafanyia kazi. Katika sehemu ya mpango wa dharura hususan katika maeneo ya Miangalua, maeneo ya Mpui hayo yapo katika mpango wa Serikali. Kwa hiyo kikubwa sasa ni kuendelea kuyafuatilia ili yaweze kutekelezeka.

Mheshimiwa Spika, maeneo ya Mtapewa ambapo kuna nguvu kubwa ya wananchi moja ya mpango wa Serikali ni kuhakikisha maeneo yote ambayo wananchi wameweka nguvu yao, itapeleka fedha kwa ajili ya kumalizia maboma hayo, ahsante sana. (Makofi)

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati zahanati 18 katika Tarafa za Laela, Mpui, Mtowisa na Kipeta?

Supplementary Question 2

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa kuwa afya za wananchi ni muhimu na ni uwekezaji wa Serikali kwa ajili ya nguvu kazi, kumekuwa na jitihada za wananchi kujenga zahanati katika maeneo mbalimbali kwa nguvu zao na kumekuwa na bajeti ndogo kwenye halmashauri baadhi ambazo hazina uwezo. Je, ni nini mkakati wa Serikali kuweza kutenga fedha kwa ajili ya kumalizia zahanati zilizojengwa na wananchi katika maeneo yetu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kama nilivyojibu kwenye swali la pili la nyongeza la Mheshimiwa Deus Clement Sangu, kwamba moja ya mkakati wa Serikali hususan katika maeneo ambayo kuna nguvu za wananchi ni kupeleka fedha na kazi kubwa inayofanywa na Ofisi ya Rais, TAMISEMI ni kutafuta fedha kwa ajili ya kumalizia maeneo ambayo wananchi wameweka nguvu zao. Kwa hiyo katika maeneo ambayo Mheshimiwa Mbunge, ameyaainisha yapo katika mpango ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI, ahsante. (Makofi)