Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza: - Je, ni lini mianya ya majadiliano yanayopelekea rushwa kwenye mfumo wa ukadiriaji wa kodi kwa Wafanyabiashara itaondolewa?

Supplementary Question 1

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Katika taasisi ambazo zinalalamikiwa sana kwa uonevu na kukithiri kwa rushwa ni pamoja na TRA, hili linasababishwa na kujadili kodi ana kwa ana kupitia utaratibu wa sasa. Sasa kwa kuwa taratibu hizi zimekuwepo kwa miaka 22 iliyopita, TRA haioni kwamba inahitaji mabadiliko ya haraka ya kuondoa mawasiliano ya ana kwa ana ili kudhibiti jambo hilo?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; dunia sasa inafanya biashara zaidi kupitia mitandao na imethibitika kwamba TRA bado wanaendesha makadirio yao kianalogia. Ni hatua zipi za haraka ambazo inachukua ili kuweza kukusanya kodi ambayo inapotea kwenye mitandao? (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kanyasu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kuwa ipo changamoto ya mifumo na ipo changamoto hiyo ya kukutana ana kwa ana kati ya Mlipa Kodi na Afisa Kodi. Serikali hatua ambayo imechukua ni kuimarisha mifumo kuhakikisha kwamba Mlipa Kodi na Afisa Kodi hawatokutana ana kwa ana ili kuepusha hiyo mianya ya rushwa.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili. Serikali kupitia Bunge lako Tukufu lilifanya marekebisho ya sheria pamoja na kuanzisha Kitengo Maalum kwa ajili ya kusimamia kodi za biashara, mtandao na kuhakikisha kwamba utambuzi wa mfanyabishara ya kimtandao amesajiliwa na kulipa kodi inayostahiki.