Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ameir Abdalla Ameir

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. AMEIR ABDALLA AMEIR aliuliza: - Je, kwa kiwango gani TEHAMA inatumika kuboresha sekta ya kilimo nchini?

Supplementary Question 1

MHE. AMEIR ABDALLA AMEIR: Mheshimiwa Spika, ahsante sana; kwanza teknolojia hii ya habari na mawasiliano ina mchango mkubwa sana katika kuziba lile pengo la uhaba wa Maafisa Ugani wetu kwa muda mfupi na kwa eneo kubwa, sasa Wizara ina mpango gani sasa wa kuanzisha Apps au mifumo mbalimbali ya TEHAMA, ambayo mifumo hii itawasaidia wakulima wetu wadogo wadogo kupata taarifa kwa wakati na kwa usahihi?

Pili, Wizara sasa haioni kuna umuhimu wa kuyashawishi makampuni mbalimbali ya simu kutoa kifurushi maalum cha huduma za wakulima, ambapo sasa wakulima wetu watakuwa wanapata taarifa hizi wakiwa maeneo mbalimbali? Ahsante. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba nijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge kwa pamoja kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara inatambua matumizi ya teknolojia ambapo ndiyo dunia ya leo inapoelekea, katika kurahisiha utoaji wa huduma kwa wakulima na hasa kupitia Maafisa Ugani, tunao mfumo ambao tunauita N-Kilimo ambao mpaka hivi sasa tumeshasajili Maafisa Ugani 9,725, ambao kazi yao kubwa ni kuhakikisha kwamba tunasambaza taarifa hizi kwa wakulima kupitia programu hii. Pia tunayo call center yetu ya Wizara ya Kilimo ambayo pia wakulima ambao wanapata changamoto mbalimbali wamekuwa wakipiga simu na kupata ufafanuzi na kujibiwa baadhi ya changamoto ambazo wanakabiliaba nazo.

Mheshimiwa Spika, nitoe tu rai na kuwaomba wakulima wote nchini Tanzania kuendelea kuitumia namba yetu ile ya 0733 800 200 kwa ajili ya kuweza kupata huduma mbalimbali za kilimo kupitia teknolojia hii.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili ushauri tunaupokea wa kukaa na kampuni za simu kurahisisha utoaji wa huduma hizi za ugani kwa wakulima wetu. Ushauri huo tumeupokea ni mzuri, tutaona namna ya kuweza kuboresha ili wakulima wetu waweze kupata taarifa kwa wakati. (Makofi)

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMEIR ABDALLA AMEIR aliuliza: - Je, kwa kiwango gani TEHAMA inatumika kuboresha sekta ya kilimo nchini?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa katika taarifa yao ya Wizara ya Kilimo walisema sasa hivi wakulima watakuwa wanapimiwa udongo kupitia Maafisa Ugani kwa vishkwambi. Elimu hiyo sasa wakulima wanayo maana yake nimeona bado hawajaanza kutumia hiyo teknolojia ya kupimiwa udongo katika mashamba yao?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, ni mkakati wa Serikali kuhakikisha tunapima afya ya udongo ya ikolojia zote saba nchi nzima ili wakulima wawe na taarifa sahihi za afya ya udongo katika maeneo yao.

Mheshimiwa Spika, hivi sasa Serikali kupitia Maafisa Ugani tumewapatia scanners za kwenda kupima afya ya udongo ambayo itasaidia kutoa taarifa kwa wakulima. Vilevile katika mwaka wa fedha unaokuja tutakwenda kununua mobile lab ambazo zitakuwa pia zinapita kwa ajili ya kuwapimia afya ya udongo wakulima. Kwa hiyo, tutakuwa tunao uwezo wa kupima afya ya udongo kupitia maabara na kupitia katika magari pamoja na kit ambacho tumewapa Maafisa Ugani ambapo mkulima akipimiwa afya yake ya udongo hapo hapo akiwa shambani atapata cheti chake ambacho kitaonesha katika udongo huo kuna nutrients za aina gani na anahitaji nini kupanda zao gani na atumie mbolea ya namna gani, ambayo itakuwa ni ukombozi mkubwa kwa wakulima wa nchi yetu ya Tanzania. (Makofi)