Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itafungua Zahanati iliyopo Kijiji cha Nyakashengi Kata ya Businde ili iweze kutoa huduma kwa wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipatia nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Tatizo lililopo Kyerwa linafanana kabisa na tatizo lililoko Mtwara Vijijini. Kata ya Mpapura Kijiji cha Nanyani tokea Julai, 2017 ujenzi wa zahanati ulishakamilika. Mpaka leo ninapozungumza takribani ni miaka minne. Ni lini sasa Serikali itakwenda kufungua zahanati hiyo ili wananchi waweze kupata huduma kwa sababu wamesubiri kwa muda mrefu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Shamsia Mtamba, Mbunge wa Mtwara Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimejibu kwa kutoa agizo la jumla kwa Wakurugenzi wote wa Halmashauri na Ma-DMO kuhakikisha wanatuletea taarifa Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa ajili ya zahanati zote ambazo zimeshakamilika na zinahitaji usajili ili ziweze kufunguliwa na sisi tuweze kujua namna bora ya kuchukua hatua za kuzifungua mapema.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itafungua Zahanati iliyopo Kijiji cha Nyakashengi Kata ya Businde ili iweze kutoa huduma kwa wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa nami niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mtaa wa Mpamaa ambao uko Kata ya Miyuji katika Jiji la Dodoma wananchi wamejenga zahanati, lakini hadi sasa zahanati ile haifanyi kazi. Nini kauli ya Serikali katika kuifanya zahanati hii ifanye kazi ili wananchi wapate huduma ya afya? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Fatma Toufiq, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ameainisha eneo la Mpamaa kwamba kuna zahanati ambayo imejengwa na bado haijafanya kazi. Nitoe kauli ya jumla kwa Serikali kwamba maeneo yote ambayo zahanati zimekamilika tungeomba tupate taarifa, ziletwe Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili tuweze kufanya tathmini ya jumla kwa ajili ya usajili, vifaa tiba pamoja na wauguzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itafungua Zahanati iliyopo Kijiji cha Nyakashengi Kata ya Businde ili iweze kutoa huduma kwa wananchi?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona. Ni lini Serikali itafungua zahanati katika Kijiji cha Pomelini Kata ya Ng’uruhe Jimbo la Kilolo kwa sababu wananchi walichangia na Serikali imeshamalizia kile kituo kwa muda mrefu; na wananchi wanakuwa wakifuata matibabu umbali mrefu sana?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Ritta Kabati, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge, kwa swali hili ambalo ameliuliza nitamwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kilolo pamoja na DMO waende wakafanye tathmini ili watuletee ili ifanyiwe usajili na ili tuweze kuifungua.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itafungua Zahanati iliyopo Kijiji cha Nyakashengi Kata ya Businde ili iweze kutoa huduma kwa wananchi?

Supplementary Question 4

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kata ya Itela ina zahanati mbili; Itera pamoja na Chanya. Zahanati hizi zimekamilika kila kitu lakini bado hazijasajiliwa. Ni lini zitasajiliwa ili wananchi waweze kupata huduma?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili: Tarafa ya Nkwenda ina kata saba na ina kituo kimoja cha afya na ina zaidi ya wakazi 150,000; na msongamano umekuwa mkubwa katika kituo kile cha afya, lakini tulileta ombi Wizarani la kujenga kituo kingine cha afya katika Kata ya Songambele: Je, ni lini Serikali italeta pesa ili tuweze kujenga kituo cha afya ili kuondoa msongamano uliopo? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Innocent Sebba Bilakwate, Mbunge wa Jimbo la Kyerwa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, hizo zahanati mbili ambazo zimekamilika katika eneo la Itera ambalo Mheshimiwa Mbunge ameliainisha, nimwakikishie tu kwamba zipo katika mchakato wa usajili na usajili utakapokamilika manake na sisi tutapeleka wahudumu ili zianze kutoa huduma. Kwa hiyo, nimwondoe shaka kwenye hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, kuhusu Tarafa ya Ikwenda ambayo walileta maombi ya kuongezewa kituo cha afya kingine, nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba jukumu la kwanza la Serikali ilikuwa ni kuhakikisha tarafa zote tunazipelekea vituo cha afya. Jambo hilo tumelifanya na sasa hivi ujenzi unaendelea. Jukumu la pili la Serikali ni kuhakikisha kwamba maeneo yote yenye uhitaji kulingana na umbali na ukubwa wa maeneo tutapeleka vilevile vituo vya afya ikiwemo katika Tarafa yake ya Ikwenda.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.