Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU M. ZODO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Daraja la Bweni Wilayani Pangani?

Supplementary Question 1

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Ni lini Serikali itajenga Daraja la Itunundu kwenda Igodikafu Jimbo la Isimani ambako wananchi wanapata shida sana hasa wakati wa masika? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimwakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba daraja alilolitaja litajengwa kama lilivyoainishwa kwenye ilani na hasa baada ya kufanyiwa usanifu wa kina.

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU M. ZODO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Daraja la Bweni Wilayani Pangani?

Supplementary Question 2

MHE. MWANTUMU M. ZODO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa katika majibu ya Naibu Waziri amesema wako kwenye hatua za mwisho kwenda kusaini mkataba wa ujenzi wa daraja hilo: Nataka kujua je, ni lini hasa mkataba huo unatarajiwa kusainiwa?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili: Kwa kuwa ujenzi wa daraja la Bweni Pangani unakwenda sambamba na ujenzi wa barabara ya Tanga - Pangani kilometa 50; na kwa kuwa ujenzi wa barabara hiyo uko asilimia 37: Je, ni upi mkakati wa Serikali wa kuhakikisha kuwa daraja hilo litakwenda kukamilika kwa wakati baada ya mkataba huo kusainiwa? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwantumu Mzamilu Zodo, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba muda wowote kabla ya mwisho wa mwezi huu tuna uhakika mkataba huu utakuwa umesainiwa na daraja hili ujenzi wake unafadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia barabara aliyoitaja tuna uhakika itakwenda sambamba na ndiyo maana kwa sababu ya ukubwa wa hili daraja ilipewa lot yake, ni barabara ambayo inajitegemea, ina lot yake. Kwa hiyo, tuna uhakika kwa kuwa ina lot yake na mkandarasi atakayekuwa amepatikana atasimamia hilo daraja tu na barabara za maungio wakati mkandarasi mwingine anaendelea kujenga barabara, kwa hiyo, tuna uhakika wakati mkandarasi anakamilisha barabara, daraja pia litakuwa linakamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. MWANTUMU M. ZODO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Daraja la Bweni Wilayani Pangani?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa hii nafasi. Katika Jimbo la Manyoni Mashariki, tuna araja la Sanza ambalo tayari upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ulishafanyika na hilo daraja liliingizwa kwenye bajeti hii inayoishia. Sasa nini kauli ya Serikali kwamba ni lini ujenzi wa hili daraja utaanza?

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Chaya, Mbunge wa Manyoni, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, daraja hili ni kati ya madaraja makubwa ambayo yameainishwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi, nasi kama Wizara, daraja hili tayari limeshapata kibali cha kuanza kujengwa pamoja na barabara zake za maingilio.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. MWANTUMU M. ZODO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Daraja la Bweni Wilayani Pangani?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Wizara ya Ujenzi kupitia TANROADS ilitenga Shilingi milioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa Daraja la Sangatini eneo la Tundwi Songani kule Pemba Mnazi katika mwaka wa fedha 2021/2022 hadi sasa ujenzi ule haujaanza: Ni lini ujenzi wa daraja Sangatini utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Ndugulile, Mbunge wa Kigamboni, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Daraja la Sangatini lilishatengewa fedha na fedha ipo. Tender ilitangazwa lakini ali-tender mtu mmoja na akawa ame-tender bei ya juu na tumeshalitangaza tena. Nataka nimwakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tender zitafunguliwa wiki hii na baada ya hapo daraja hili litaanza kujengwa kwa bajeti ya mwaka huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.