Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha kilimo cha Mpunga katika Mkoa wa Morogoro?

Supplementary Question 1

MHE. ABUBAKAR D. ASENGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba kwa kuzingatia kuwa Mkoa wa Morogoro ni ghala la Taifa na katika Jimbo letu la Kilombero kuna miradi mingi ya umwagiliaji; Mradi wa Kisawasawa, Mkula na Sanje inasuasua. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri atakuwa tayari kuambatana na mimi angalau weekend moja akajionee kusuasua kwa miradi hii ili Serikali ichukue hatua haraka za kuinusuru?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Abubakar Asenga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, niko tayari kuongozana naye, tutakwenda kuangalia ili tuone namna ya kuweza kukamilisha miradi hii.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha kilimo cha Mpunga katika Mkoa wa Morogoro?

Supplementary Question 2

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Wakulima wa mpunga wa Wilaya ya Nkasi pamoja na Bonde la Ziwa Rukwa changamoto yao kubwa ni skimu za umwagiliaji pamoja na soko la uhakika. Nini mkakati wa Serikali kwa kuzingatia msimu wa safari hii mavuno sio mazuri sana ili wapate soko la uhakika?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Aida Khenani, Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, moja kati ya mikakati ambayo tumeiweka katika kuongeza uzalishaji wa zao la mpunga ni kuzikamilisha skimu nyingi za umwagiliaji ambazo zinagusa maeneo aliyoyasema Mheshimiwa Mbunge. Bahati nzuri mimi mwenyewe nimekwenda kama kule Mwamapuli na maeneo mengine Kata ya Kilida kuangalia uwezekano pia kuongeza skimu hizi ili kuongeza tija katika zao letu la mpunga.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimwondoe hofu na kwamba tumejipanga vyema ili kuongeza uzalishaji na ukiangalia mpunga hivi sasa ndiyo unatutangaza vizuri nje ya mipaka ya Tanzania na uzalishaji umeongezeka sana. Kwa hiyo katika maeneo ambayo tutawapa priority ni pamoja pia na skimu za umwagiliaji katika maeneo ambayo wanalima mpunga ikiwemo katika mkoa ambao Mheshimiwa Mbunge ameusema.

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha kilimo cha Mpunga katika Mkoa wa Morogoro?

Supplementary Question 3

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa wananchi wa Mkoa wa Njombe wengi wao ni wakulima wa zao la chai. Nataka kuuliza wizara mmejipanga vipi kwa kushirikiana na Wizara ya TAMISEMI kuhakikisha kwamba mnaboresha miundombinu katika mashamba ya chai ili tuweze kupata chai nyingi zaidi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Neema Mgaya Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Njombe kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tuna changamoto katika baadhi ya maeneo ya uzalishaji kutokuwepo kwa miundombinu Rafiki lakini tunayo miradi ambayo tunaendelea kuitekeleza kupitia Agree connect ambayo pia imejihusisha na utengenezaji wa miundombinu. Nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba tutashirikiana na TAMISEMI kuhakikisha maeneo yote ya uzalishaji yanapitika kiurahisi ili tuweze kuimarisha na kukuza zao letu la chai katika Mkoa wa Njombe.

Name

Aleksia Asia Kamguna

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha kilimo cha Mpunga katika Mkoa wa Morogoro?

Supplementary Question 4

MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA: Mheshimiwa Naibu Spika, nina maswali madogo mawili ya nyongeza. Je, Serikali ina mkakati gani wa kufanya kilimo cha zao la mpunga la umwagiliaji katika maeneo ya Malinyi, Ulanga, Mlimba, Kilombero na Kilosa kuwa endelevu badala ya kutegemea msimu wa mvua?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha soko kuu la mpunga katika Wilaya ya Kilombero?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Aleksia Asia Kamguna Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli ya kwamba tunatambua kilimo cha umwagiliaji ndio suluhu katika kuboresha na kuimarisha kilimo cha mpunga katika Mkoa wa Morogoro. Nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge ya kwamba katika bajeti hii inayokuja yako mabonde makubwa na miradi mingi ya umwagiliaji ambayo itatekelezwa katika Mkoa wa Morogoro ambao pia utagusa katika maeneo ambayo ameyataja.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili la kuhusu soko kuu ni wazo zuri, wazo jema tumelichukua na tutakwenda kuchakata ndani ya Serikali kuona uwezekano wake.

Name

Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha kilimo cha Mpunga katika Mkoa wa Morogoro?

Supplementary Question 5

MHE. GHATI Z. CHOMETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa nafasi, kama ilivyo katika zao la mpunga, kahawa aina ya Arabica inalimwa Mkoani Mara katika Wilaya ya Tarime na hasa Tarime Vijijini. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwawezesha wakulima wale ili waweze kuongeza uzalishaji katika zao hilo ili kuinua uchumi wao na uchumi wa nchi yetu.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, moja kati ya mikakati tuliyonayo na kukuza zao la kahawa mojawapo ni uzalishaji na usambazaji wa miche bora ya kuwafanya wakulima wengi waweze kuzalisha kwa tija.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka huu tumejipanga kuzalisha miche milioni 20 kuwafikia wakulima wengi kadri iweekanavyo na hivyo pia tutawagusa wakulima wa Mkoa wa Mara.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha kilimo cha Mpunga katika Mkoa wa Morogoro?

Supplementary Question 6

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa wananchi wa Jimbo la Hai wamehamasika sana kulima zao la kahawa na kwa kuwa tumepewa taarifa pale TaCRI miche ya kahawa imekwisha. Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha wananchi wa Jimbo la Hai msimu huu wanapata miche ya kahawa?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Saashisha Mafuwe, Mbunge wa Hai, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema katika majibu ya swali la kahawa ambalo limeulizwa humu ndani, pamoja na changamoto aliyosema Mheshimiwa Mbunge, lakini tumeamua kuzishirikisha pia sekta binafsi ili tuwe tuna uhakika wa uzalishaji wa miche hii kwa maana ya TaCRI pamoja na sekta binafsi. Naomba nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba zoezi hilo linaendelea na usambazaji wa miche hii kama ambavyo Serikali imeahidi utafanyika na wakulimna watanufaika na miche hii.

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha kilimo cha Mpunga katika Mkoa wa Morogoro?

Supplementary Question 7

MHE. ABBAS G. TARIMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Napenda niiulize Serikali, kwenye upande wa kuhamasisha na kuleta wawekezaji wakubwa katika ukulima mkubwa kwa maana ya large scale farming hasa katika ngano. Ni nini mtazamo wa Serikali katika zao hili? Ahsante.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Abbas Tarimba, Mbunge wa Kinondoni, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni dhamira ya Serikali kuhakikisha tunakuza kilimo cha nchi yetu ya Tanzania na ni ukweli ulio dhahiri kwamba ili kukuza kilimo chetu lazima tukubali kwamba dunia ya leo inahitaji uwekezaji mkubwa. Kwa sasa mlango uko wazi kwa ajili ya majadiliano na kuwakaribisha wawekezaji na Mheshimiwa Mbunge yeyote ambaye anaona kuna wawekezaji wanakuja kuwekeza nchini na kuna tija, tuko tayari kuwasikiliza na kuweza kuwasaidia ili jambo hili liweze kukamilika.