Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Watumishi wa Kada ya Afya Wilayani Kalambo kwa kuzingatia upungufu uliopo?

Supplementary Question 1

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda nielekeze swali langu katika Mkoa wa Simiyu Wilaya ya Busega: Ni lini Serikali itapeleka mashine ya X-Ray katika Wilaya ya Busega? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Minza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa sasa hivi tuko katika mchakato wa kufanya manunuzi ya vifaa tiba, ninaamini mara baada ya mchakato huu kukamilika, basi tutalizingatia hilo nao tutawapatia hiyo X-Ray.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Watumishi wa Kada ya Afya Wilayani Kalambo kwa kuzingatia upungufu uliopo?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Utakubaliana nami kwamba katika jibu ambalo limetolewa na Serikali, wanaongelea suala la kuajiri watumishi 7,612; na kitakachoenda kufanyika ni kugawa kwa kuzingatia quality na siyo equity. Katika swali langu la msingi nimeongelea juu ya upungufu mkubwa wa watumishi wa kada ya afya katika Halmashauri yetu. Hivi karibuni wamehama watumishi 33 na wakahamishiwa watumishi watatu tu: Je, Serikali katika mgao huu itaenda kuzingatia equity badala ya equality?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa watumishi ambao wamekuwa wakipelekwa katika maeneo yanayoonekana kama ya pembezoni wanaenda kuishi kule kama kupata confirmation na kupata ukuu wa idara na baadaye kuhama; je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba watumishi wote ambao wanapangwa katika maeneo hayo wanaenda kuishi kwa kipindi chote?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Josephat Sinkamba Kandege, Mbunge wa Jimbo la Kalambo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, baada ya kumaliza mchakato wa ajira, maana yake kitakachofuata ni kugawanya katika Halmashauri zote nchini na tutagawa kulingana na mahitaji katika maeneo husika. Kwa hiyo, hatutakuwa na ile namba kwamba tutagawa Halmashauri zote kwa usawa, Hapana, tutagawa kulingana na mahitaji. Tunatambua kabisa kwamba katika maeneo kama Kalambo kuna uhitaji mkubwa, kwa hiyo, tutawapa kulingana na hiyo idadi.

Mheshimiwa Spika, la pili, kwenye suala la kuhusu kuhama watumishi baada ya kwenda katika maeneo ya pembezoni, moja, ya utaratibu ambao tumeweka sasa, mtumishi haruhusiwi kuhama siyo chini ya miaka mitatu, lazima afanye kazi katika eneo alilopangiwa na baada ya hapo, labda kuwe na sababu za msingi sana ambazo zinapelekea mtu huyo apaswe kuhama. Kwa sasa ni kwamba tunafunga na wote wanakuwa na commitment letter ya kuhakikisha wanabaki katika maeneo hayo, ahsante. (Makofi)

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Watumishi wa Kada ya Afya Wilayani Kalambo kwa kuzingatia upungufu uliopo?

Supplementary Question 3

MHE. AYSHROSE N. MATTEMBE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mkoa wa Singida unakabiliwa na upungufu mkubwa wa wauguzi ambako zaidi ya wauguzi 800 wanahitajika: Je, ni lini Serikali itatuletea wauguzi wa kutosha ili kusaidia mkoa wangu kutoa huduma za afya na hususan kusaidia huduma ya mama na mtoto?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Aysharose Mattembe, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Singida, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali tunaajiri kulingana na bajeti na mapato kadri ambavyo tunapata na mahitaji yaliyoko. Kwa hiyo, tutakavyoajiri ikiwemo ajira 7,612 maana yake katika ule mgawanyo na Singida nao tutawapatia, ahsante.

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Watumishi wa Kada ya Afya Wilayani Kalambo kwa kuzingatia upungufu uliopo?

Supplementary Question 4

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali moja la nyongeza. Kwa kuwa Serikali kwa kushirikiana na wananchi wa Jimbo la Babati Vijijini wamekamilisha ujenzi wa zahanati za Guse, Hayamango na Yasanda, lakini zahanati hizo zimeshindwa kufunguliwa kwa sababu ya upungufu wa watumishi wa afya: Je, Serikali sasa ina mpango gani wa kuwapeleka watumishi ili zahanti hizo ziweze kufunguliwa na kuhudumia wananchi wetu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Daniel Sillo, Mbunge wa Babati Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, natambua kwamba kuna zahanati nyingi hazijafunguliwa kwa sababu ya kukosa watumishi, nasi kama Serikali tunalijua hilo na katika watumishi ambao tutawapeleka, tutawaagiza Wakurugenzi wawapangie katika zile zahanati ambazo zimekamilika ili ziweze kutoa huduma, ahsante.

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Watumishi wa Kada ya Afya Wilayani Kalambo kwa kuzingatia upungufu uliopo?

Supplementary Question 5

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe ina changamoto kubwa sana ya watumishi hasa kada ya afya na elimu: Je, ni lini Serikali itapeleka walimu katika Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe ili kukabiliana na changamoto kubwa sana ya watoto wetu kukosa elimu na elimu kushuka? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Furaha Matondo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa ajira ziko katika hatua za mwisho na hizi ajira ni pamoja na kada ya afya na elimu, kwa hiyo, katika ule mgawanyo Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe vilevile tumeizingatia na itapata katika ule mgawanyo wa walimu pamoja na kada ya afya, ahsante.

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Watumishi wa Kada ya Afya Wilayani Kalambo kwa kuzingatia upungufu uliopo?

Supplementary Question 6

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Nikiwa Mbunge wa Kawe, tumejenga hospitali kubwa sana ya mfano kupitia fedha za Halmashauri eneo la Mabwepande ambayo sasa hivi iko katika hatua za mwisho kabisa: Je, katika mchakato wa kugawa watumishi wa kada ya afya, Serikali mtazingatia hospitali hii kubwa ambayo itasaidia Wilaya za Bagamoyo na Kawe? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Halima Mdee, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, katika sehemu ya ajira ambazo tutazipanga na kupeleka katika Hospitali ya Mabwepande ni pamoja na hizi ajira mpya ambazo tutazitoa, ahsante. (Makofi)