Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza:- Je, ni lini Mradi wa Umwagiliaji wa Kijiji cha Arusha Chini utatengewa fedha ili uanze kutekelezwa?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, kwanza niishukuru Serikali kwa kutenga fedha kwa ajili ya kufanya usanifu kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Mheshimiwa Spika, swali langu la kwanza kwa kuwa ekari zilizoorodheshwa hapa kwenye jibu la msingi ni 120 lakini kuna eneo kubwa ambalo linazunguka Kijiji cha Ngonja, Arusha Chini na Arusha Juu.

Je, Serikali ipo tayari kujumuisha eneo hilo wakati wa kufanya usanifu? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini swali langu la pili, je, Naibu Waziri yupo tayari kuambatana na mimi baada ya kuahirisha Bunge hili la Bajeti ili akajionee uhalisia wa Mradi huu? Nakushukuru.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Abdallah Dadi Chikota, Mbunge wa Nanyamba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tupo tayari kutoa maelekezo kwa timu yetu ambayo itafanya usanifu kuhakikisha kwamba inaligusa eneo kubwa kadri iwezekanavyo, kwa sababu ni maelekezo ya Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi kwamba ifikapo mwaka 2025 tuwe tuna eneo ambalo linamwaagiliwa la hekta 1,200,000. Kwa kuongezeka kwa eneo ni sehemu ya tija ya uzalishaji kwetu pia, kwa hiyo wataalam wetu pia wataangalia eneo ambalo halijajumuishwa liweze kujumuishwa.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, niko tayari Bunge hili likifikia ukomo wake kwa maana ya vikao hivi vya Bajeti, kuongozana na Mheshimiwa Mbunge kwenda kuangalia uhalisia wa Mradi husika.

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza:- Je, ni lini Mradi wa Umwagiliaji wa Kijiji cha Arusha Chini utatengewa fedha ili uanze kutekelezwa?

Supplementary Question 2

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Katika Mkoa wa Morogoro eneo la Chita kuna hekari 12,000 zenye miundombinu ya umwagiliaji ambapo sasa hivi zinamilikiwa na JKT, lakini kwa uwezo wao wameweza kulima ekari 2,500. Je, ni lini Serikali itawekeza nguvu yake pale ili kuweza kusaidia usalama wa chakula na kuongeza pato la Taifa? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Felista Njau kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika Fungu Namba 05 la Tume ya Umwagiliaji katika Randama ukiangalia Jedwali la Nne limeainisha moja kati ya miradi ambayo tutakwenda kuitekeleza katika mwaka ujao wa fedha ni mradi wa JKT – Chita. Kwa hiyo, nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge mradi upo katika mpango na utatekelezwa katika bajeti inayokuja.

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza:- Je, ni lini Mradi wa Umwagiliaji wa Kijiji cha Arusha Chini utatengewa fedha ili uanze kutekelezwa?

Supplementary Question 3

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa nafasi hii ya swali dogo la nyongeza.

Kwa kuwa, skimu ya umwagiliaji wa Ilemba usanifu wa kina umekamilika kwa asilimia 100. Je, ni lini Serikali mtaanza ujenzi wa skimu hii ambayo ni muhimu sana kwa uchumi wa wananchi wa Kata ya Ilemba?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Deus Sangu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mradi ambao Mheshimiwa Mbunge ameusema upo katika utekelezaji wa mwaka wa fedha unaokuja, nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba mradi huo utatekelezwa.

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza:- Je, ni lini Mradi wa Umwagiliaji wa Kijiji cha Arusha Chini utatengewa fedha ili uanze kutekelezwa?

Supplementary Question 4

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Serikali kwa muda mrefu sana imeahidi kuhusu ujenzi wa bwawa kwenye Bonde la Mto Mkomazi. Je, ni lini ahadi hii sasa itaanza kutekelezwa rasmi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Timotheo Mnzava, Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli utekelezaji wa mradi wa Bonde la Mto Mkomazi umekuwa ni wa muda mrefu na Mheshimiwa Mbunge amekuwa akifuatilia sana, nataka nimhakikishie mbele ya Bunge lako Tukufu ya kwamba ifikapo mwezi wa Saba taratibu za awali za kumpata mshauri mwelekezi zitafanyika ili kazi ya usanifu na upembuzi yakinifu uanze na baada ya hapo tutaanza utekelezaji wa mradi huu mkubwa ambao wananchi wa Korogwe wanausubiri kwa hamu kwa sababu unagusa zaidi ya Kata 11 na una manufaa makubwa sana. Nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge tutaanza mwezi wa Saba mapema kabisa kumpata mshauri mwelekezi. (Makofi)

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza:- Je, ni lini Mradi wa Umwagiliaji wa Kijiji cha Arusha Chini utatengewa fedha ili uanze kutekelezwa?

Supplementary Question 5

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Kijiji cha Kidoka na Takwa wanayo miradi maarufu ya umwagiliaji lakini mpaka leo Serikali haijawekeza chochote. Naomba kujua commitment ya Serikali katika kuwekeza kwenye miradi ya vijiji hivyo, ahsante.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mohamed Monni Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nimekuwa nikirudia mara nyingi kusema ya kwamba tumedhamiria kuyagusa maeneo mengi ambayo yanafaa kwa ajili ya umwagiliaji ili kuongeza uzalishaji wa mazao katika nchi yetu ya Tanzania, hatua ambayo inafanyika hivi sasa ni kwamba timu yetu imeendelea kuyapitia maeneo yote kufahamu status ya kila maeneo ambayo yanafaa kwa ajili ya umwagiliaji. Katika eneo ambalo Mheshimiwa amelitaja la Kidoka mimi na yeye tutatafuta muda hapa katikati tutaongozana pamoja na wataalam kwenda kulitembelea na kuona uwezekano wa kufanya uwekezaji katika eneo hilo. (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza:- Je, ni lini Mradi wa Umwagiliaji wa Kijiji cha Arusha Chini utatengewa fedha ili uanze kutekelezwa?

Supplementary Question 6

MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona na kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa, Serikali imeongeza kwa kiwango kikubwa bajeti ya umwagiliaji kutoka Shilingi Bilioni 46 mpaka Bilioni 361 na kwakuwa Wilaya yetu ya Bagamoyo tunayo skimu ya umwagiliaji - Ruvu inaitwa Chauru yenye wanachama zaidi ya 900 lakini inayo changamoto kubwa ya uchakavu wa miundombinu.

Je, Serikali inatoa ahadi gani kwa wanachama wa skimu hii ya umwagiliaji Chauru katika ukarabati wa miundombinu? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Subira Mgalu Mbunge, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Spika, mradi huo tunaufahamu na changamoto iliyopo, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba katika miradi ambayo Tume imepanga kuifanyika kazi katika bajeti inayokuja mradi huo pia umeainishwa, kwa hiyo wakulima wa eneo hilo watapata nafasi ya kuweza kufaidika na uboreshaji wa miundombinu hasa baada ya kuanza utekelezaji kupitia bajeti inayokuja.